Filosofia ya Rorya
JF-Expert Member
- Sep 20, 2021
- 3,214
- 3,587
Nyanja: Utawala Bora/Uwajibikaji.
Mheshimiwa Rais Chokambaya Bin Mwaminifu wa Jamhuri-ya-Mazuzu amefanya uamuzi mgumu kwa nia ya kuokoa fedha za serikali yake katikati ya upinzani mkali wa wadau wa sekta ya ukandarasi. Katika kikao cha Baraza la Mawaziri, alitangaza uamuzi wake huo kama ifuatavyo:-
Ili kudhibiti matumizi ya rasilimali-fedha za serikali na kuwapa wananchi fursa ya kufuatilia mienendo ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye maeneo yao; kama namna ya kudhihirisha nguzo za dhana ya Utawala Bora za uwazi na uwajibikaji hususan kwenye eneo la matumizi ya rasilimali-fedha, serikali sasa ama itarekebisha au itatengeneza sheria au kanuni itakayomlazimisha mkandarasi wa mradi wa maendeleo kuandika thamani ya pesa ya mradi, muda wa mradi na hatua iliyofikiwa (Project Phase) kwenye ama jiwe la msingi la uzinduzi wa ujenzi wa mradi au kwenye bango la ujenzi/ukandarasi (Project Billboard) inayosimikwa kwenye sehemu ya wazi kuelezea aina ya mradi, wakandarasi na mnufaika. Aidha, thamani ya mradi itaandikwa kwa lugha-rafiki (rahisi) na kwa maneno na tarakimu vinavyosomeka kwa wazi (human legible).
Hii itaondoa ubabaishaji wa wakandarasi wanapotosha hesabu za miradi ya maendeleo kwenye ziara za viongozi na kwenye mikutano ya hadhara inayofanywa na viongozi hao, lakini pia sheria hiyo au kanuni hiyo itawapa wananchi (walipa kodi ambao ndiyo wanufaikaji wa miradi) mamlaka ya kuhoji utekelezaji wa miradi husika ama kama mtu mmoja mmoja au kama kundi. Sambamba na hilo, Mheshimiwa Rais Chokambaya Bin Mwaminifu wa Jamhuri-ya-Mazuzu ameamuru mabango yote ya miradi kwenye safu ya chini ya bango yaandikwe maneno yafuatayo:
|
|
Mfano wa bango-pendekezwa la mradi wa maendeleo (Proposed Project Billboard)
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
| |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|