Rais awateua Prof. Maboko kuwa Mwenyekiti wa Bodi TBS, Omar Amir Naibu Mkurugenzi mamlaka ya Uvuvi

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,483
54,853
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Makenya Abraham Honoratus Maboko kuwaa Mwenyekiti wa bodi ya Shirika Ia Viwango Tanzania(TBS).

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 23 Juni, 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi inasema uteuzi huu umeanza tarehe 21 Juni, 2016.

Prof. Makenya Abraham Honoratus Maboko anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Prof. Cuthbert Mhilu ambaye amemaliza muda wake.

Prof. Maboko ni Mhadhiri wa Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Dares salaam (UDSM).

Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Omari Ali Amir kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu.

Kabla ya uteuzi huo Dkt. Omari Ali Amir alikuwaa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi inasema uteuzi wa Dkt. Omari Ali Amir umeanza tarehe 21 Juni, 2016.

Utaratibu wa kujaza nafasi ya Mkurugenzi Mkuu na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uvuvi wa bahari kuu ni wa kubadilishana kila baada ya miaka mitatu kati ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar, ambapo Mkurugenzi Mkuu akitoka upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania basi Naibu Mkurugenzi Mkuu hutoka upande mwingine wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kinyume chake.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam


ClpE4gUWMAE0v-C.jpg

 

Attachments

  • ClpRt1pWEAAgY9O.jpg
    ClpRt1pWEAAgY9O.jpg
    4.7 KB · Views: 101
Hivi tbs Ina majukumu gani maana kila Leo vitu bandia Na visivyo Na ubora vinaongezeka....???
 
Daaa Prof.Maboko prof Mkandala prof Mgaya wazee wa UDSM tuliwaita triple M, wakikuita ujuwe wee ni kwenu Hamna mjadala. Hongera Prof
 
MABOKO , MGAYA , MUKANDALA. (MMM)3 wazee wa idarani hao wana access na mkuu 24/7. Wacha kabisa.
 
Kumbe unawakumbuka hao jamaa ila Mgaya alikua na msimamo kuwazidi hao wengine. Mgaya Ni mtaalamu wa aquatic, makenya ni bingwa wa geology while sympo ni mwanasiasa.

Daaa Prof.Maboko prof Mkandala prof Mgaya wazee wa UDSM tuliwaita triple M, wakikuita ujuwe wee ni kwenu Hamna mjadala. Hongera Prof
 
C ujira umesitishwa na mkulu had hapo badae au ni kwa sis wenye vibachela mh?
 
Hivi tbs Ina majukumu gani maana kila Leo vitu bandia Na visivyo Na ubora vinaongezeka....???
TBS ni shirika la viwango, wanaandaa viwango na kuvisimimamia. kuwepo kwa bidhaa hafifu inchini kunasababishwa na mim na wew. tbs sio police kulinda kila bidhaa inayoingia, ama kutengenezwa vichochoroni. tuungane mim na wew kuikataa bidhaa fake, tutafanikiwa kuitokomeza.[/QUOTE]
 
Sijaelewa! Amemteua naibu katibu mkuu kuwa mkurugenzi? Sio demotion hiyo? .....naona amerudi one step down!
 
Profesa Maboko pamoja na Dr. Mporogomyi walishitumiwa katika kipindi ambacho Profesa Ndalichako alituhumiwa kwa kashfa flani hadi akafukuzwa. Inamaanisha Maboko alikuwa sahihi katika kusimamia standards kipindi hicho. Hongera zake.
 
We acha tu, alisema hizi ni zama za vijana, nashangaa anaendekeza hivi vizee
Tena kwa upande wa udsm tu hiv vyuo vingine wanasomeshwa namba kwenye teuz au uprosery na udokta wamepata kw kuunga unga
 
Hii ni awamu ya Maprofessor na Madokta,tu.sisi wa chet,dip na bachelor tuzisome namba
 
Siamini kwenye mwanazuoni kuwa mtendaji. Wengi wana nadharia lakini kama waliwahi kufanyia vitendo/mazoezi taaluma zao mtaani mi nawapongeza.
 
Profesa Maboko pamoja na Dr. Mporogomyi walishitumiwa katika kipindi ambacho Profesa Ndalichako alituhumiwa kwa kashfa flani hadi akafukuzwa. Inamaanisha Maboko alikuwa sahihi katika kusimamia standards kipindi hicho. Hongera zake.
KUmbeeee, nakumbuka kundi flani lilikuwa na ushawishi mkubwa hapo magogoni so wakatumia loop hole hiyo hadi NECTA hadi mama Ndalichako akaenda "masomoni"
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom