Rais atwambie lini ataweka mikataba ya madini hadharani,na atupe dondoo za mjadala na Acacia

iparamasa

JF-Expert Member
Nov 14, 2013
13,438
14,916
Nimeshangaa waandishi wa habari wa Tanzania leo ikulu hawakumuuliza Rais ni lini ataweka mikataba ya madini hadharani kama alivyoahidi,na vizuri angetaja tarehe na mwezi

Maana inaonekana watanzania tumeshasahau hii kauli.

Na pia atupe dondoo za mjadala wake na acacia,na watakachokubaliana pia kitangazwe hadharani,isiwe siri na iwe commitment ya wazi kabisa

Ni lini tutapewa mikataba hii?

Waandishi huwa mnaenda ikulu na ajenda au ni whisky tu?

Wabunge mna fursa ya maswali kila alhamis,kwa waziri mkuu,muulizeni lini wataweka mikataba wazi
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom