fikirikwanza
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 7,452
- 3,065
Kwa vile nchi sio mali ya mtu, na kwa vile cheo ni dhamana tu, na kwa vile CCM na serikali yake ni wasikivu, na kwa vile bunge limekwishajadili na kutoa maazimio yake, na kwa vile ni haki ya waTZ kujua nini kinaendelea sakata la ESCROW.
Uhuru na maadhimisho ya siku ya UHURU wa Tanganyika ni siku mwafaka kwa Rais na amri jeshi mkuu kutoa minongono ktk maisha ya watz kwa kuongea kwa kina suala hilo na pengine kuchukua hatua kwa wahusika.
Najiuliza tu rais bila kusema escrow na kutekeleza maazimio ya bunge ni nini atawambia watz wamshangilie? au atanunua watu wenye njaa ya akili kumshangilia na kuhadaa umma kuwa anashangiliwa? au wataleta story za ajabu kama kiuengua wagombea wa UKAWA zaidi ya mia tano wakizani amani inapatikana kwa kunyonga haki, tena mchana kweupe?
Rais atasema nini iwapo kesho itafika bado watuhumiwa wa escrow wakitumia magari na mali za umma?? Maswi, Tibaijuka, Werema, Muhongo, Masele, Saada, Mwigulu, Kigoda, Mawe matatu??
Uwezo na uelewa wa JK sasa kwenye mizani tena pana sana. Wananchi wako nyuma ya bunge, kweli inafahamika bunge linawakilisha wananchi wala sio mahakama. Wananchi wanataka kuona kwa vitendo kuwa rais sio mtu wa kupuuza mambo makubwa ya taifa, rais sio shwaiba wa waharifu wa aina yoyote.
Je rais ameona nini na raha gani kukaa na suala hili zaidi ya wiki mbili sasa???
UHURU bila majibu japo kwa maazimio ya bunge ni fedheha nyingine wa umma.
Nawasilisha
Uhuru na maadhimisho ya siku ya UHURU wa Tanganyika ni siku mwafaka kwa Rais na amri jeshi mkuu kutoa minongono ktk maisha ya watz kwa kuongea kwa kina suala hilo na pengine kuchukua hatua kwa wahusika.
Najiuliza tu rais bila kusema escrow na kutekeleza maazimio ya bunge ni nini atawambia watz wamshangilie? au atanunua watu wenye njaa ya akili kumshangilia na kuhadaa umma kuwa anashangiliwa? au wataleta story za ajabu kama kiuengua wagombea wa UKAWA zaidi ya mia tano wakizani amani inapatikana kwa kunyonga haki, tena mchana kweupe?
Rais atasema nini iwapo kesho itafika bado watuhumiwa wa escrow wakitumia magari na mali za umma?? Maswi, Tibaijuka, Werema, Muhongo, Masele, Saada, Mwigulu, Kigoda, Mawe matatu??
Uwezo na uelewa wa JK sasa kwenye mizani tena pana sana. Wananchi wako nyuma ya bunge, kweli inafahamika bunge linawakilisha wananchi wala sio mahakama. Wananchi wanataka kuona kwa vitendo kuwa rais sio mtu wa kupuuza mambo makubwa ya taifa, rais sio shwaiba wa waharifu wa aina yoyote.
Je rais ameona nini na raha gani kukaa na suala hili zaidi ya wiki mbili sasa???
UHURU bila majibu japo kwa maazimio ya bunge ni fedheha nyingine wa umma.
Nawasilisha