Rais asiingiliwe uteuzi wa Mawaziri-Ikulu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Hata kama anawateua mafisadi au wenye uwezo finyu katika utendaji basi Watanzania tunyamaze tu!? Sasa naona mnataka kuleta udikteta wa kuwafunga midomo Watanzania

Rais asiingiliwe uteuzi wa Mawaziri-Ikulu

2008-05-14 10:34:55
Na Mashaka Mgeta

Ikulu jijini Dar es Salaam, imesema Rais Jakaya Kikwete, hapaswi kushinikizwa kuhusu idadi ya mabadiliko anayoyafanya katika Baraza la Mawaziri.

Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Bw. Salva Rweyemamu, aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana.

Hivi karibuni, kumeibuka hisia miongoni mwa jamii, huku wakiwepo baadhi ya watu wanaohoji fursa za ufanisi zinazopatikana kutokana na mabadiliko ya mara kwa mara ya Baraza hilo.

Rais Kikwete, ameshafanya mabadiliko na uteuzi wa mawaziri mara nne, kutokana na matukio mbalimbali yaliyotokea nchini kwa vipindi tofauti.

Matukio hayo ni pamoja vifo vya waliokuwa Mawaziri, marehemu Juma Akukweti (Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu aliyeshughulikia Bunge) na marehemu Salome Mbatia (Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto).

Mabadiliko mengine yalifanywa kutokana na kujiuzulu kwa mawaziri, Bw. Edward Lowassa (Waziri Mkuu), Dk. Ibrahim Msabaha (Afrika Mashariki) na Bw. Nazir Karamagi (Nishati na Madini).

Mawaziri hao walijiuzulu mwaka huu, kutokana na kashfa ya mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura, uliosainiwa kati ya serikali na kampuni ya Richmond.

Aidha, wiki iliyopita, Rais Kikwete ambaye yupo madarakani kwa takribani miaka miwili na nusu sasa, alitangaza Baraza jipya la mawaziri, kufuatia hatua ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge.

Bw. Change, alijiuzulu wadhifa huo kutokana na kashfa ya kuhifadhi dola milioni moha za Kimarekani kwenye benki moja huko Jersey, nchini Uingereza.

``Nadhani tumuache Rais afanye mabadiliko ya mawaziri kwa jinsi anavyoona inafaa, lengo ni kuleta ufanisi na kuwatumikia wananchi?tumpe nafasi afanye kazi zake,`` alisema Bw. Rweyemamu.

Bw. Rweyemamu, alisema mabadiliko yanayofanywa na Rais Kikwete, hayana athari zozote kisheria, kwa vile hakuna kifungu cha Katiba kinachoelezea ukomo wa mabadiliko yanayopaswa kufanywa katika Baraza hilo.

Bw. Rweyemamu, alisema mawaziri waliopo wanapaswa kuungwa mkono kwa vile, pamoja na mambo mengine, wanafanya kazi katika mazingira magumu ambayo hata hivyo, hakuyafafanua.

SOURCE: Nipashe
 
wanashindwa kuelewa kuwa vitendo vya rais vinapaswa kuhojiwa kama vitendo vya mtu mwengine.
rais hayupo above everything. japo kuwa hatuwezi kumshinikiza kufanya mabadiliko, lakini tutayaongelea mpaka iwe bughudha kwake alete yenye manufaa nasi
 
Bw. Salva Rweyemamu, ni mwandishi wa habari (naamini hivyo), anajua vizuri uhuru wa mtu kutoa maoni na uhuru wa vyombo vya habari kutoa taarifa ikiwa ni pamoja na zile zisizowapendeza wakubwa. Hivi Rweyemamu atafurahi kuona manunguniko, maoni, maswali au hisia za wananchi haziandikwi magazetini? Hivi Rweyemamu haoni kama habari hizo zinamsaidia Rais? Kwa mfano wananchi walilalamika kuhusu ukubwa wa Baraza la Mawaziri, Rais akaitikia kwa kupunguza baraza, haya si ndo mafanikio ya habari?

Rweyemamu asisaliti taaluma yake, anapaswa kutetea uhuru wa maoni. Ni haki ya mwananchi kuhoji maamuzi ya Serikali au Rais na ni wajibu wa Serikali kujibu au kutolea maelezo siyo kuwafumba mdomo wananchi.
 
Rweyemamu ana-strike first kujibu email yangu niliyomwandikia kuhoji ukubwa wa baraza la mawaziri. Sasa hataki hata watu wajadili baraza la mawaziri wa JK.


Kazi kwelikweli!
 
JK amewewekwa hapo na wananchi...kwa hiyo asijisahau kuwa ni haki yetu kuhoji....Halafu huyu Salva huwa anjitokezea kwenye nosense issues....mbona haelezei kuhusu mafisadi? na inaonekana JK siku hizi hana sura mbele yetu
 
Kwani JK huko ikulu alienda tu kama mtu anaenda nyumbani kwake? au wanachi wa wa-tz ndio walimpa kura zilizompeleka huko? Sasa kama waliompa kura wanaona anatupeleka porini tusiseme kuwa eti anaingiliwa?? au Salva kupata ukurugenzi wa habari ikulu anadhani ndio njia ya kutaka kuwapumbaza watu?? Nadhani kama ana akili angetulia katiba inaturuhusu kutoa maoni kama hawayapendi sisi ndio tumewapa ajira huko ikulu huenda bwana Salva hajui hilo...

Muda mfupi mmeshajiona miungu watu kuwa watu wasihoji hata kama mnafanya madudu?? Tunawasubiri 2010 tuone...Majitu ya hovyo kabisa au ndio njia ya kubembeleza ajira iendelee kuwepo?? Kazi ziko nyingi mkuu salva hata ukitoka huko JF huwa kuna nafasi za kazi hutangazwa unaweza kuomba tu watoto wako wajue kuwa baba bado yupo lakini acha watanzania waseme yale wanayoona ni mambo ya hovyo mnayofanya..Taifa letu wote hili mkituingiza porini tuna-lost wote sasa kwani tusiepushe shari mapema??
 
Back
Top Bottom