Rais anakazana kupata mikopo na misaada lakini mifumo ya ukusanyaji kodi, tozo na mapato mengine imetoboka sana

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
873
4,065
Unaweza kujenga Imani Kwa wageni kuja kuwekeza nchini Kwa wingi; wageni wakafika Kwa wingi na kutumia fursa Ila usinufaike na kuwepo Kwa wageni hao.

Juhudi za Mhe. Rais zinaweza zisizaie matunda Kwa Sababu aliowaamini kwamba wanaweza kukusanya na kuhifadhi mapato yatokanayo na uwekezaji wa Kigeni pamoja na utalii hawapo serious kuifanya kazi Yao.

Naomba niwakumbushe taasisi zifuatazo umuhimu wa kumuunga Rais Mkono tuweze kulipa madeni tunayodaiwa na kuendesha Serikali.

1. IDARA INAYOSIMAMIA AJIRA KWA WAGENI; Wapo wageni wengi Sana katika makampuni na taasisi mbalimbali wanaofanya KAZI Bila vibali.. waajiri wanatambua gharama za vibali na mchango wake Kwa uchumi wa nchi yetu. Lakini pia hakuna mwajiri anayependa kulipa fedha ya serikali Bila kusukumwa. Idara ya KAZI ikiweka sheria Kali na faini kubwa Kwa wageni wanaoishi na kufanya KAZI Bila vibali hakutakuwepo usumbufu wala udanganyifu WA kukwepa mapato ya serikali.

2. UHAMIAJI; Mnaporuhusu wageni kuingia nchini jitahidini kufuatilia wanafanya nini nchini. Mnapoboresha huduma mipakani mkaacha ufuatiliaji wa ndani ya nchi mnafanya vijana wa Kitanzania kukosa ajira na wageni kupewa ajira bila kuwa na sifa.

Maviwanda yaliyopo mkoa wa Mwanza sekta ya uvuvi, viwanda vilivyopo mkuranga na eneo lote la Pwani ikiwemo Dar es salaam, mahoteli na Mashamba yalipo Arusha kuna vibarua wengi wasio Watanzania na hakuna anayelipa Kodi, anayelipa vibali.

Watu wanaofanya kazi na wachina wanaweza kueleza namna ambavyo hawa ndugu zetu wanaweza kutumia kitambulisho kimoja hata watu Kumi Bila kukamatwa. Chukieni hatua makampuni haya Yanamchezea Mhe. Rais.

3. Mifuko ya Jamii: Hawa watu wamekaa ofisini wakisubiri waajiri wapeleke Makato ya wafanyakazi. Nani kawaambia makampuni ya Kigeni yanaweza Acha kazi zao wawapelekee idadi ya waajiriwa. Kodi kubwa inapotea katika eneo hili.

4. Taasisi za fedha; trend inaonyesha mabenki yetu yameshindwa kabisa kutoa huduma za kimataifa. Hapa pameibuka ufunguaji na utumiaji WA mabenki ya nje kufanya biashara za kimataifa. Natambua BOT wapo macho Ila nataka niseme kwenye eneo hili la udhibiti wa fedha kupitia Benki za Kigeni mamlaka zimeshindwa kabisa. Fedha nyingi zinapita kwenye haya mabenki.

5. Economic Intelligence Unit- Sijui kama tuna watu wanaofanya jukumu hili hapa nchini. Kwa mambo yanavyokwenda NI kama tumewekeza Sana kwenye intelijensia ya jinai na siasa kuliko uchumi. Naamini BOT kama Wana unit kama hii basi wanapaswa kuipanua ifanye kazi yakunusa fursa na kuzitangaza wakati huo ifanye jukumu la kuona mianya na kuiziba bila kuleta taharuki ya kamatakamata.

6. TRA - punguzeni au ikiwezekana ondoeni kabisa ujeshi na upolisi kwenye kukusanya Kodi. Mkiwa rafiki wa wananchi mkaweka na bonasi Kwa yeyote atakayefichua ukwepaji Kodi ntaona kazi yenu itakavyokua nyepesi.

Badilikeni. Tengeni muda wenu kukaa na jamii
 
Uko sahihi kwa 90% lakini naamini kwa katiba hii kiongozi mkuu anajua kila kitu na nani mwenye ujasiri wa kimdanganya? Binafsi nitamkubali kiongozi atakaekubali katiba mpya nzuri na ngumu itakayoonesha uwajibikaji wa kila sector/mtu na sio madarakani yote kwa mtu mmoja
 
Badala ya kukazania mikopo tu.

Ingekuwa vyema zaidi kuimarisha makusanyo ya kodi ili tuwe na uhuru na fedha zetu.

Kama ikihitajika kukopa iwe ni kwa jambo muhimu tu na iwe ni dharura.
 
TRA inafanya kazi nzuri sana makusanyo yameongezeka sana, Isipokuwa bado hayatoshi kutokana na wingi na ukubwa wa miradi inayoitaji kuimalizia ambayo iliachwa ikiwa chini ya 20%,miradi lazima imaliziwe, madarasa lazima yajengwe, tunashuhudia mabarabara yakijengwa mitaani, hivyo vyote hivi lazima viende kwa pamoja.
 
TRA inafanya kazi nzuri sana makusanyo yameongezeka sana, Isipokuwa bado hayatoshi kutokana na wingi na ukubwa wa miradi inayoitaji kuimalizia ambayo iliachwa ikiwa chini ya 20%,miradi lazima imaliziwe, madarasa lazima yajengwe, tunashuhudia mabarabara yakijengwa mitaani, hivyo vyote hivi lazima viende kwa pamoja.
Mbona hujasema na Uwezo wa Wananchi kulipa KODI umefika mwisho kutokana na Umasikini walionao?
 
20230120_073036.jpg
 
Hii katuni ndio inaendana na heading ya mtoa mada ila content yake inazungumza kingine kabisa..

Mtoa ameongelea madhaifu ya mfumo wa kukusanya Kodi..

Na Mimi namuongezea,tenda zote inazotoa serikali hususani za ujenzi huko wanapoteza Kodi za waajiriwa na pia nssf
Mara nyingi tenda mbali mbali ndiyo njia kuu ya kupoteza fedha, NAPENDEKEZA MFUMO WA TENDA USOGEZWE KWENYE OFISI YA MAKAMU WA RAIS / KUZIBA LEAKAGE ENDAPO KAMA ZIPO! SI JAMBO BAYA TUKAMUONGEZEA MAALUMU HUYU KAZI HII YA UDHIBITI.
Hili haliwezi kuwapenda wengi lakini linamsaada kwa kazi nzito anayoifanya rais wetu.
 
Umeandikaka jambo la msingi sana..

tunakwenda kukopakopa huku matobi na mianya ya ufujaji hela ipo yakutosha.

tunakwenda kukopakopa huku tunaweza kubanana na kuset mifumo itakayoweza kutupa mapato mengi na makubwa tukaacha kabisa au kupunguza kukopa.
 
Umeandikaka jambo la msingi sana..

tunakwenda kukopakopa huku matobi na mianya ya ufujaji hela ipo yakutosha.

tunakwenda kukopakopa huku tunaweza kubanana na kuset mifumo itakayoweza kutupa mapato mengi na makubwa tukaacha kabisa au kupunguza kukopa.
Ipende nchi yako bainisha mianya hiyo kuwa mzalendo!
 
Mara nyingi tenda mbali mbali ndiyo njia kuu ya kupoteza fedha, NAPENDEKEZA MFUMO WA TENDA USOGEZWE KWENYE OFISI YA MAKAMU WA RAIS / KUZIBA LEAKAGE ENDAPO KAMA ZIPO! SI JAMBO BAYA TUKAMUONGEZEA MAALUMU HUYU KAZI HII YA UDHIBITI.
Hili haliwezi kuwapenda wengi lakini linamsaada kwa kazi nzito anayoifanya rais wetu.
Haiwezekani hicho unachoongea na sijui unamaanisha nini kusema mfumo usogezwe ofisi ya VP.
 
Ipende nchi yako bainisha mianya hiyo kuwa mzalendo!

Mianya mingi inajulikana na hata mtoa maada alichobainisha ni kile kile tu tunarudia, SHIDA NI WATENDAJI WASIOWAAMINIFU KILA MAHALA KUANZIA JUU MPAKA CHINI..

Ziwekwe taratibubna sheria ngumu, Rais na wote walio ngazi za maamuzi wawe wakali, CCM iiache serikali mbali na siasa zake.
 
Matobo au mianya inayozungumziwa hapa ni Ile ya taasisi kushindwa kusimamia vyema majukumu yake na kufanya mapato yaliyokusudiwa kutobaki nchini badala yake wageni kukusanya nakuondoka kwenda kusisimua uchumi kwao.

Wageni wanapokuja Tanzania wanapaswa kubanwa wasipate mwanya wakukwepa Kodi au kukwepa gharama yoyote yakuwepo nchini.

Mifumo ya taasisi nilizotaja haionyeshi kuwa makini kulinda upotevu wa makusanyo. Ikumbukwe Bila makusanyo ya ndani hakuna namna tunaweza kulipa madeni wala kuhudumia Watanzania.

Kama mgeni anatakiwa kulipia visa alipe, anatakiwa kulipia kufanya kazi nchini alipe, kama anapaswa kuajiri Watanzania basi tusimamie aajiri Watanzania, kama anapaswa kuwalipia waajiriwa wake michango ya mifuko ya kijamii afanye hivyo, kama anapaswa kutumia Benki za ndani hasa kwenye Forex basi tuwasimamie wafanye hivyo.

Mataifa makubwa Dunia yamewekeza kulinda upotevu wa mapato yatokanayo na uwekezaji wa Kigeni Kwa Sababu ukishindwa kulinda basi tegemea wageni kutorosha mapato na kwenda kuwekeza kwao.

Tumuunge mkono Mhe. Rais Kwa kumsaidia kulinda upotevu wa mapato yanayopaswa kuzalishwa na wawekezaji pamoja na watalii....tukilala tumetumia na tukumbuke hii siyo kazi ya Mhe. Rais ,ni kazi ya taasisi zilizopewa dhamana.

Wapo wageni wengi Sana wanafanya biashara Kwa mwamvuli wa Utanzania aidha wakijifanya wameona, wamepewa au Wana ubia........ukifuatilia uhalisia hadhi za kuoa au ubia zinawekwa kwenye nyaraka kukwepa Kodi. Hakuna ndoa wala ubia ulioainishwa kwenye makaratasi.


Hii ndiyo mianya.....watoa huduma wawe serious na ikiwezekana ikibainika kuna watu wanachamgia kutoa huduma Kwa kuidanganya serikali wafukuzwe kazi waajiriwe watu wapya....tunao Vijana wengi Sana wanaotafuta ajira.
 
Mianya mingi inajulikana na hata mtoa maada alichobainisha ni kile kile tu tunarudia, SHIDA NI WATENDAJI WASIOWAAMINIFU KILA MAHALA KUANZIA JUU MPAKA CHINI..

Ziwekwe taratibubna sheria ngumu, Rais na wote walio ngazi za maamuzi wawe wakali, CCM iiache serikali mbali na siasa zake.
TRA wanaomba msaada wako, tafadhali onyesha mahali udhaifu upo ili uzibwe, kuwa mzalendo!
 
Ipo kampuni moja ya Logistics inajaza wahindi raia wa kenya hawana vibali halisi, na wahindi wengine, Mtu intern anatoka ulaya na anapewa kibali cha kazi kwa sheria ipi na misingi ipi. Interns wanatakiwa watoke katika vyuo vya Tanzania kwa vigezo maalum lakini wanapewa special permit.

Kuna shida kubwa hata ya ku contol wazungu wengi hawako qualified mfano Logistics manager sheria na ilisimamiwa wakati wa magufuli lazima TCU na Bodi ya ugavi wathibitishe competence yake, hivyo hivyo kwa credit controlller au Finance manage ni lazima Nbaa wathibitishe uhalali wa qualification zake ndio apewe kibali kama expert kuanza kazi na kampuni ya kigeni.

Wenzetu wenye mamlaka hawajali kwamba ni lazima ajira na waliostahili kazi kwanza wapatikane watanzania ndio mruhusu kampuni ilete foreigner. Kuna waganda wanapewa client service manager kazi zilitakiwa zifanywe na watanazania.

Mama tafdhali tumbua huko TIC, labour na migration naona wamelala sana.
 
Heading na content ni vitu 2 tofauti.

Taja mfuko mmja au onesha mfuko uliotoboka vinginevyo ni uropokaji na uzushi usio na Tija.
Acha unazi wa kishamba, kwani ni uongo kuwa fedha za umma zinaibiwa kila mara?Huwa usikii CAG kila mwaka anaripoti madudu juu ya udhaufu wa taasisi zetu?
 
Tatizo tunachoshana mnajitoa kulipa Kodi mnazuia mianya kumbe mnatajirisha wana siasa na viongozi wa kubwa. AFRICA PANACHOSHA SANA we una kuta waziri tu ana maghorofa ndani na nje ya nchi
 
Back
Top Bottom