Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,556
- 29,646
Watanzania wenzangu tunashuhudia namna ambavyo nchi yetu inavyoendeshwa hovyo-hovyo ambapo hali za wananchi kimaisha zinazidi kuwa mbaya na kutisha.
Rais wetu, yeye yupo 'bize' katika kuimarisha chama na kukesha kutengeneza strategies za kupambana na vyama pinzani badala ya kutumia nguvu hizo hizo kuondoa ama kupunguza matatizo ya nchi.
Mfumuko wa bei, Wanasiasa kufanya biashara kwenye ofisi za umma, Wizi na usimamizi mbovu wa mali za umma, mikataba ya kipuuzi, madudu ya forodha dhidi ya watanzania ni sehemu ndogo ya matatizo makubwa yanayoikabili Tanzania.
Kupitia hotuba yake ya Mkutano mkuu wa CCM, alitamka kwamba wanaCCM wasitegemee tena kusaidiwa na polisi kupambana na CHADEMA (ndo adui yao mkubwa kuliko ufisadi), ni wazi kwamba shughuli kubwa inayofanywa na jeshi la polisi ya kusigina Katiba ya nchi kwa kunyonga haki za binadamu kwenye utekelezaji wa kazi zao ni baraka kutoka JUU (ninaposema juu ninamaanisha uongozi wa juu wa CCM naam EC!).
Pamoja na mengine mengi, hivi sasa CCM imeamua kuwatumia watumishi wa uuma (mawaziri) kwenye mikutano ya kuimarisha chama mikoani ambapo ni dhahiri kwamba serikali nzima inapiga siasa badala ya kufanya kazi za umma. Kauli za wakuu wa vyombo vya usalama Jeshi (Rtd- Shimbo) na polisi dhidi ya upinzani nchini ni ushahidi wa namna rais anavyoongoza nchi kisiasa.
Matamshi ya Waziri Wassira dhidi ya upinzani hususani aliposema kuwa CHADEMA wataisambaratisha ni mwendelezo wa mbinu za ofisi kuu ya nchi kufanya siasa badala ya kazi. Tumeshuhudia wachumia tumbo wengi wanaojitokeza na kujipendekeza kwake wanavyoinuliwa na kuwekwa nafasi za juu kiutawala kwa sababu ni wanasiasa (wachochezi) hodari.
Tulitegemea Rais awe mlezi na msimamizi mweledi wa Katiba, sheria na kanuni zilizopo lakini yeye na Vyombo vyake wanaamua kufanya siasa inapelekea imani za raia kwake kuporomoka.
Ndugu zangu, kuna hatari kubwa endapo tutaendelea kushangilia mwenendo wa rais wetu huyu wa kuamua kuweka shughuli za kisiasa ktk vipaumbele vya kwanza badala ya kuutumikia umma kama Katiba inavyomtaka.
Washauri wake mnapaswa kumsaidia kutekeleza majukumu yake ya kiofisi zaidi ya kisiasa. Chuki ya umma inavyozidi kuongezeka kwa kutojali kwake na namna anavyowakumbatia MAFISI wanaolitafuna taifa (mf. Kinana, Rostam, Jeetu Patel, EL. n.k.) itapelekea mlipuko utakaoitikisa nchi.
Kuendekeza siasa badala ya kazi za umma ni upungufu wa maono na hekima
Rais wetu, yeye yupo 'bize' katika kuimarisha chama na kukesha kutengeneza strategies za kupambana na vyama pinzani badala ya kutumia nguvu hizo hizo kuondoa ama kupunguza matatizo ya nchi.
Mfumuko wa bei, Wanasiasa kufanya biashara kwenye ofisi za umma, Wizi na usimamizi mbovu wa mali za umma, mikataba ya kipuuzi, madudu ya forodha dhidi ya watanzania ni sehemu ndogo ya matatizo makubwa yanayoikabili Tanzania.
Kupitia hotuba yake ya Mkutano mkuu wa CCM, alitamka kwamba wanaCCM wasitegemee tena kusaidiwa na polisi kupambana na CHADEMA (ndo adui yao mkubwa kuliko ufisadi), ni wazi kwamba shughuli kubwa inayofanywa na jeshi la polisi ya kusigina Katiba ya nchi kwa kunyonga haki za binadamu kwenye utekelezaji wa kazi zao ni baraka kutoka JUU (ninaposema juu ninamaanisha uongozi wa juu wa CCM naam EC!).
Pamoja na mengine mengi, hivi sasa CCM imeamua kuwatumia watumishi wa uuma (mawaziri) kwenye mikutano ya kuimarisha chama mikoani ambapo ni dhahiri kwamba serikali nzima inapiga siasa badala ya kufanya kazi za umma. Kauli za wakuu wa vyombo vya usalama Jeshi (Rtd- Shimbo) na polisi dhidi ya upinzani nchini ni ushahidi wa namna rais anavyoongoza nchi kisiasa.
Matamshi ya Waziri Wassira dhidi ya upinzani hususani aliposema kuwa CHADEMA wataisambaratisha ni mwendelezo wa mbinu za ofisi kuu ya nchi kufanya siasa badala ya kazi. Tumeshuhudia wachumia tumbo wengi wanaojitokeza na kujipendekeza kwake wanavyoinuliwa na kuwekwa nafasi za juu kiutawala kwa sababu ni wanasiasa (wachochezi) hodari.
Tulitegemea Rais awe mlezi na msimamizi mweledi wa Katiba, sheria na kanuni zilizopo lakini yeye na Vyombo vyake wanaamua kufanya siasa inapelekea imani za raia kwake kuporomoka.
Ndugu zangu, kuna hatari kubwa endapo tutaendelea kushangilia mwenendo wa rais wetu huyu wa kuamua kuweka shughuli za kisiasa ktk vipaumbele vya kwanza badala ya kuutumikia umma kama Katiba inavyomtaka.
Washauri wake mnapaswa kumsaidia kutekeleza majukumu yake ya kiofisi zaidi ya kisiasa. Chuki ya umma inavyozidi kuongezeka kwa kutojali kwake na namna anavyowakumbatia MAFISI wanaolitafuna taifa (mf. Kinana, Rostam, Jeetu Patel, EL. n.k.) itapelekea mlipuko utakaoitikisa nchi.
Kuendekeza siasa badala ya kazi za umma ni upungufu wa maono na hekima