Kennedy
JF-Expert Member
- Dec 28, 2011
- 49,016
- 54,299
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania, Leo Atafanya Ziara Wilayani Kisarawe Kuzindua Mradi Mkubwa Wa Maji. Ambao Utawanufaisha Wakazi Wa Kisarawe Hadi Maeneo Ya Ukonga, Pugu
Bila Shaka Tutaaambiwa Mapya Mengi Kuhusu Maendeleo Ya Nchi Yetu. Pia Wakazi Wa Pembezoni Mwa Barabara Atakayopita Wategemee Neema, Hata Mradi Hautapita Kijiji Chochote Bila Wananchi Kupata Maji
Chanzo Cha Taarifa, TBC
===
Katika tukio hilo la ukaguzi wa Mradi wa maji Wilayani Kisarawe Rais Magufuli alifika sehemu ya uzinduzi ili kupata malelezo ya kina ya mtaalamu ili kujua namna mradi huu utakavyofanya kazi na maeneo mbalimbali ambayo mradi huo utahudumu.
Aidha, baada ya kupokea maelezo hayo Rais Magufuli moja kwa moja amelekea katika kuzindua rasmi mradi huo ikiwa pamoja na kujaribu namna maji yanavyotoka katika mradi huo.
Mwisho, Rais Magufuli alipiga picha ya pamoja na na viongozi na Wakandarasi wa mradi huo na kuondoka kuelekea uwanja wa Mkutano.
Mkutano huu umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo Mawaziri wa Sekta mbalimbali, Viongozi wa DAWASA pamoja na viongozi wa Wilaya ya Kisarawe.
Hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jaffo
Amemshukuru Rais kwa kumpa dhamana ya kuhudumu katika Ofisi yake pamoja na kuwashukuru Wanakisarawe kwa kumpa nafasi kama Mbunge wao.
Zaidi ya hayo, Mh. Jaffo amemshukuru Rais kwa kufanya Uzinduzi wa maji wenye thamani ya shilingi Bilioni 10.6 ambao anaeleza utasaidia kutatua kero ya maji Kisarawe shida iliyokuwapo kwa muda mrefu pamoja na ujenzi wa vituo vya afya na kazi zote kubwa ambazo Rais amezifanya.
Zaidi ya hayo, Mh. Jaffo amewashukuru na kuwasifu Watendaji wa Dawasa kwa jitihada kubwa waliyofanya katika kuhakikisha mradi huo unatimia vizuri.
Zaidi, Viongozi wengine waliopata nafasi ya kuzungumza ni pamoja na Profesa Kabudi na Waziri wa utalii Dr Hamis Kigwangwala ambao wote wamempongeza Rais kwa kazi kubwa na miradi aliyoifanikisha katika eneo la Kisarawe na mikoa ya Pwani.
HOTUBA YA RAIS MAGUFULI
Rais ameanza kwa kuwashukuru Viongozi kwa kumualika katika tukio hili muhimu la Uzinduzi pamoja na Kuwashukuru Wananchi wa Wilaya ya Kisarawe kumchagua mwaka 2015.
Rais Magufuli ameeleza kuwa mnamo tarehe 21 Juni 2017 alipokwenda Mlandizi kuzindua mtambo wa maji wa Ruvu Juu wa kuhudumia Kibaha na Jiji la Dar es Salaam alisema aliona Mradi ule usiishie khudumia Kibaha peke yake bali ufike mpaka Kisarawe kwa sababu aliona kuwa Wilaya hiyo Kongwe yenye Miaka zaidi ya 103 ilistahili kufikiwa na maji.
Aidha, katika hili Rais Magufuli amemshukuru Waziri, Naibu Waziri, Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu na Watendaji wengine wa Dawasa kwa kazi kubwa waliyoifanya kuhakikisha kuwa mradi huo mkubwa unafanikiwa. Kwa hili Rais ametoa rai kuwa Maslahi ya Wafanyakazi wa Dawasa yaangaliwe vizuri kwani hata Mapato yameongezeka.
Aidha, Rais amemsifu Mh. Jafo kwa juhudi alizozifanya kuhakikisha pesa ya mradi huo inapatikana kwani anaeleza wakati anaahidi jambo hilo bado alikuwa hajapata pesa hizo.
Zaidi ya hayo, Rais Magufuli amewapongeza Wana Kisarawe wote kwa mradi huu pamoja na kuzidi kuwa pongeza Dawasa kwa kujiongeza na kuufikisha mradi huo mpaka Pugu mahali ambapo Baba wa Taifa anahistoria napo.
Aidha, Rais Magufuli ameelaza kuwa moja ya ahadi kubwa walizozitioa kwenye ilani ya uchaguzi ilikuwa ni kuboresha miradi ya maji Mijini na Vijijini anafarijika kuona kuwa wametekeleza miradi hiyo kwa vitendo katika sehemu mbalimbali nchini yenye thamani ya Trilioni 3.
Akifafanuza zadi suala hili, Rais Magufuli amesema "Tumeweza kutekeleza miradi mbalimbali ya maji nchini yanye thamani zaidi ya trilioni 3, hii imefanya upatikanaji wa maji safi na salama uongezeke kutoka asilimia 47% ya mwaka 2015 kwa Vijijini na kufikia asilimia 70.1 kwa mwaka huu lakini pia Mijini kutoka asilimia 74% mpaka asilimia 84% kwa sasa."
Rais Magufuli anaeleza kuwa katika kipindi cha Miaka mitano wametekeleza miradi mbalimbali katika mkoa wa Pwani ambayo kwa ujumla wake ni miradi 45.
Zaidi ya hayo, Rais Magufuli ameeleza kuwa ukiacha mradi huu wa maji walioutekeleza katika Mkoa huu pia wametekeleza miradi mingine mingi ya Afya, umeme na barabara. Mathalani, katika mradi wa Afya Rais Magufuli ameeleza kuwa katika miaka 5 iliyopita wameleta takribani bilioni 12.8 kwa ajili ya kujenga na kukarabati hospitali za Wilaya tano na vituo vya afya 18 vikiwamo vinne vilivyopo katika wilaya hii ya Kisarawe pamoja na magari ya Wagonjwa 12 na kufanya Mkoa wa Pwani kuwa na magari ya Wagonjwa 36.
Sambamba na hilo, Rais Magufuli ameeleza kuwa Wameongeza idadi ya Watumishi wa afya na kuongeza dawa na kufanya upatikanaji wake uongezeke na kufikia asilimia 96%.
Katika sekta ya Elimu Rais Magufuli ameeleza juhudi mbalimbali ambazo Serikali yake imezifanya kuhakikisha kuwa elimu inakuwa katika mazingira mazuri. Rais ameeleza kuwa miongoni mwa juhudi hizo ni pamoja na kuwekeza pesa zaidi ya bilioni 30 na kuboresha mbalimbali.
Vilevile, Rais Magufuli ameeleza jitihada za Serikali yake Mkoani pwani katika sekta ya umeme na miundo mbinu mbalimbali ikiwamo kukubali ombi la Mkuu wa Mkoa juu ya ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami.
Rais Magufuli ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka 5 iliyopita Mkoa wa pwani umeongoza kwa kujenga viwanda ambapo umejenge viwanda vipatavyo 797 na hivyo kuufanya mkoa huu kuwa na viwanda 1192 kutoka viwanda 395 vilivyokuwapo mwaka 2016 ambapo kati ya viwanda vilivyopo katika mkoa huu vikubwa ni 69 vya kati ni 88 vidogo ni 216 na vidogo sana ni 819 hivyo wanaongoza Tanzania nzima kwa kujenga viwanda vingi.
Zaidi ya hayo, Rais amewasisitiza Wanakisarawe kuutunza mradi huu ili udumu. Amewaonya kukatakata mabomba chini pamoja na kutokuacha maji yakamwagika hovyo.
Rais Magufuli Amtengua DAS wa Kisarawe na kumteua Mwanana Msumi kuwa DAS mpya
Rais Magufuli ametengua uteuzi wa DAS wa Kisarawe, Mtela Mwampamba kwa kuwa na tuhuma zisizoenda na kazi yake ikiwemo kutembea na wake za watu. Rais ameeleza kuwa aliisha muonya lakini hakuonyeka.
Katika hili Rais Magufuli amemteua Mwanamama Mwanana Msumi kuwa DAS mpya wa Kisarawe. Awali Mwanana alikuwa Afisa Tawala. Uteuzi huu umetokana na pendekezo alilopewa hapo hapo na Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
Mwisho, Rais Magufuli amewashukuru Wananchi wote waliohudhuria Mkutano huo pamoja na kuvishukuru vikundi vya sanaa na Wasanii wote kwa kumtumbuizia na kumuimbia nyimbo mbalimbali.
Bila Shaka Tutaaambiwa Mapya Mengi Kuhusu Maendeleo Ya Nchi Yetu. Pia Wakazi Wa Pembezoni Mwa Barabara Atakayopita Wategemee Neema, Hata Mradi Hautapita Kijiji Chochote Bila Wananchi Kupata Maji
Chanzo Cha Taarifa, TBC
===
Katika tukio hilo la ukaguzi wa Mradi wa maji Wilayani Kisarawe Rais Magufuli alifika sehemu ya uzinduzi ili kupata malelezo ya kina ya mtaalamu ili kujua namna mradi huu utakavyofanya kazi na maeneo mbalimbali ambayo mradi huo utahudumu.
Aidha, baada ya kupokea maelezo hayo Rais Magufuli moja kwa moja amelekea katika kuzindua rasmi mradi huo ikiwa pamoja na kujaribu namna maji yanavyotoka katika mradi huo.
Mwisho, Rais Magufuli alipiga picha ya pamoja na na viongozi na Wakandarasi wa mradi huo na kuondoka kuelekea uwanja wa Mkutano.
Mkutano huu umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo Mawaziri wa Sekta mbalimbali, Viongozi wa DAWASA pamoja na viongozi wa Wilaya ya Kisarawe.
Hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jaffo
Amemshukuru Rais kwa kumpa dhamana ya kuhudumu katika Ofisi yake pamoja na kuwashukuru Wanakisarawe kwa kumpa nafasi kama Mbunge wao.
Zaidi ya hayo, Mh. Jaffo amemshukuru Rais kwa kufanya Uzinduzi wa maji wenye thamani ya shilingi Bilioni 10.6 ambao anaeleza utasaidia kutatua kero ya maji Kisarawe shida iliyokuwapo kwa muda mrefu pamoja na ujenzi wa vituo vya afya na kazi zote kubwa ambazo Rais amezifanya.
Zaidi ya hayo, Mh. Jaffo amewashukuru na kuwasifu Watendaji wa Dawasa kwa jitihada kubwa waliyofanya katika kuhakikisha mradi huo unatimia vizuri.
Zaidi, Viongozi wengine waliopata nafasi ya kuzungumza ni pamoja na Profesa Kabudi na Waziri wa utalii Dr Hamis Kigwangwala ambao wote wamempongeza Rais kwa kazi kubwa na miradi aliyoifanikisha katika eneo la Kisarawe na mikoa ya Pwani.
HOTUBA YA RAIS MAGUFULI
Rais ameanza kwa kuwashukuru Viongozi kwa kumualika katika tukio hili muhimu la Uzinduzi pamoja na Kuwashukuru Wananchi wa Wilaya ya Kisarawe kumchagua mwaka 2015.
Rais Magufuli ameeleza kuwa mnamo tarehe 21 Juni 2017 alipokwenda Mlandizi kuzindua mtambo wa maji wa Ruvu Juu wa kuhudumia Kibaha na Jiji la Dar es Salaam alisema aliona Mradi ule usiishie khudumia Kibaha peke yake bali ufike mpaka Kisarawe kwa sababu aliona kuwa Wilaya hiyo Kongwe yenye Miaka zaidi ya 103 ilistahili kufikiwa na maji.
Aidha, katika hili Rais Magufuli amemshukuru Waziri, Naibu Waziri, Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu na Watendaji wengine wa Dawasa kwa kazi kubwa waliyoifanya kuhakikisha kuwa mradi huo mkubwa unafanikiwa. Kwa hili Rais ametoa rai kuwa Maslahi ya Wafanyakazi wa Dawasa yaangaliwe vizuri kwani hata Mapato yameongezeka.
Aidha, Rais amemsifu Mh. Jafo kwa juhudi alizozifanya kuhakikisha pesa ya mradi huo inapatikana kwani anaeleza wakati anaahidi jambo hilo bado alikuwa hajapata pesa hizo.
Zaidi ya hayo, Rais Magufuli amewapongeza Wana Kisarawe wote kwa mradi huu pamoja na kuzidi kuwa pongeza Dawasa kwa kujiongeza na kuufikisha mradi huo mpaka Pugu mahali ambapo Baba wa Taifa anahistoria napo.
Aidha, Rais Magufuli ameelaza kuwa moja ya ahadi kubwa walizozitioa kwenye ilani ya uchaguzi ilikuwa ni kuboresha miradi ya maji Mijini na Vijijini anafarijika kuona kuwa wametekeleza miradi hiyo kwa vitendo katika sehemu mbalimbali nchini yenye thamani ya Trilioni 3.
Akifafanuza zadi suala hili, Rais Magufuli amesema "Tumeweza kutekeleza miradi mbalimbali ya maji nchini yanye thamani zaidi ya trilioni 3, hii imefanya upatikanaji wa maji safi na salama uongezeke kutoka asilimia 47% ya mwaka 2015 kwa Vijijini na kufikia asilimia 70.1 kwa mwaka huu lakini pia Mijini kutoka asilimia 74% mpaka asilimia 84% kwa sasa."
Rais Magufuli anaeleza kuwa katika kipindi cha Miaka mitano wametekeleza miradi mbalimbali katika mkoa wa Pwani ambayo kwa ujumla wake ni miradi 45.
Zaidi ya hayo, Rais Magufuli ameeleza kuwa ukiacha mradi huu wa maji walioutekeleza katika Mkoa huu pia wametekeleza miradi mingine mingi ya Afya, umeme na barabara. Mathalani, katika mradi wa Afya Rais Magufuli ameeleza kuwa katika miaka 5 iliyopita wameleta takribani bilioni 12.8 kwa ajili ya kujenga na kukarabati hospitali za Wilaya tano na vituo vya afya 18 vikiwamo vinne vilivyopo katika wilaya hii ya Kisarawe pamoja na magari ya Wagonjwa 12 na kufanya Mkoa wa Pwani kuwa na magari ya Wagonjwa 36.
Sambamba na hilo, Rais Magufuli ameeleza kuwa Wameongeza idadi ya Watumishi wa afya na kuongeza dawa na kufanya upatikanaji wake uongezeke na kufikia asilimia 96%.
Katika sekta ya Elimu Rais Magufuli ameeleza juhudi mbalimbali ambazo Serikali yake imezifanya kuhakikisha kuwa elimu inakuwa katika mazingira mazuri. Rais ameeleza kuwa miongoni mwa juhudi hizo ni pamoja na kuwekeza pesa zaidi ya bilioni 30 na kuboresha mbalimbali.
Vilevile, Rais Magufuli ameeleza jitihada za Serikali yake Mkoani pwani katika sekta ya umeme na miundo mbinu mbalimbali ikiwamo kukubali ombi la Mkuu wa Mkoa juu ya ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami.
Rais Magufuli ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka 5 iliyopita Mkoa wa pwani umeongoza kwa kujenga viwanda ambapo umejenge viwanda vipatavyo 797 na hivyo kuufanya mkoa huu kuwa na viwanda 1192 kutoka viwanda 395 vilivyokuwapo mwaka 2016 ambapo kati ya viwanda vilivyopo katika mkoa huu vikubwa ni 69 vya kati ni 88 vidogo ni 216 na vidogo sana ni 819 hivyo wanaongoza Tanzania nzima kwa kujenga viwanda vingi.
Zaidi ya hayo, Rais amewasisitiza Wanakisarawe kuutunza mradi huu ili udumu. Amewaonya kukatakata mabomba chini pamoja na kutokuacha maji yakamwagika hovyo.
Rais Magufuli Amtengua DAS wa Kisarawe na kumteua Mwanana Msumi kuwa DAS mpya
Rais Magufuli ametengua uteuzi wa DAS wa Kisarawe, Mtela Mwampamba kwa kuwa na tuhuma zisizoenda na kazi yake ikiwemo kutembea na wake za watu. Rais ameeleza kuwa aliisha muonya lakini hakuonyeka.
Katika hili Rais Magufuli amemteua Mwanamama Mwanana Msumi kuwa DAS mpya wa Kisarawe. Awali Mwanana alikuwa Afisa Tawala. Uteuzi huu umetokana na pendekezo alilopewa hapo hapo na Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
Mwisho, Rais Magufuli amewashukuru Wananchi wote waliohudhuria Mkutano huo pamoja na kuvishukuru vikundi vya sanaa na Wasanii wote kwa kumtumbuizia na kumuimbia nyimbo mbalimbali.