Rais ajaye, tunaomba upunguze gharama ya kununua units za kutumia maji ya bomba

PAZIA 3

JF-Expert Member
Jan 30, 2018
1,070
1,842
Hii ni turufu nzuri kwa mwanasiasa, natamani kusikia Mgombea yeyote wa Urais akilizungumzia hili, licha ya baadhi ya maeneo kukosa maji, haiwezi kuhalalisha maeneo yenye maji ya bomba kuuziwa Tsh 1200/= kwa unit ilhali tukijua maji ni uhai lazima yatumike Kila muda. Rais ajae alimulike hili kwani kuna maeneo fulani watu wamefungia bomba za maji na wakazi wa maeneo Yale hawaishi kulumbana na kuuziana maji kwa Bei kubwa.

Kitu kingine kwa kuongeza, Rais ajae arekebishe mfumo wa matumizi na ugawaji wa hela za TASAF. Sijawahi kuunga mkono namna ya utoaji wa pesa za TASAF kwa kuwapa pesa mkononi wananchi maskini.

Kwa kuhitimisha, nashauri Raisi ajae, akatae mfumo wa ukandamizaji wa TCU kwa wahitimu was fomu 6 kuomba kuchaguliwa kujiunga na vyuo vikuu kwa kulipia Tsh 10000/=kwa Kila chuo unachoomba. Kuna vijana mpaka Sasa wametumia zaidi ya elfu 70 kuomba kuchaguliwa kujiunga na chuo kikuu. Hili silisikii likizungumziwa na wanasiasa kabisa.

Naomba kuwasilisha
 
Asante kwa mawazo yako, Bavicha sio muda wanayachukua na kuyafikisha mahali husika....
 
Hivi kuna mtu amenote kuwa gharama za maji mwezi huu wa uchaguzi bili imekuja takriban mara mbili ya gharama za miezi ya kawaida?

Hawa watu wa mamlaka za maji inaelekea wameongeza gharama kimya kimya Je huenda serikali inatafuta hela kinguvu? .

Mamlaka za maji nchini zitoe maelezo
 
Gharama ya maji ya serikali ni kubwa sana.nadhani Kama sh 1700 kwa unit kwa DAWASA.halafu sijui wanapigaje units hizo.nadhani hata zile mita zao zina walakini.nadhani kuna haja ya kuzihakiki kama zinafanya kazi sawa sawa, nazitilia mashaka.maana kuna wakati maji yanakatika karibu siku 4 kwa wiki lakini units unaziona nyingi sana.
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Kupata maji ya uhakika serikali ingejenga reservoirs katika majimbo. Reservoirs zikusanye maji ya mvua pamoja na ya mito.

Kuwe na kampuni binafsi zipate tenda ya kusambaza mabomba. Bill iwe flat rate mfano kila nyumba 30,000 kwa mwezi.
 
Kupata maji ya uhakika serikali ingejenga reservoirs katika majimbo. Reservoir zikusanye maji ya mvua pamoja na ya mito.

Kuwe na kampuni binafsi zipate tenda ya kusambaza mabomba. Bill iwe flat rate mfano kila nyumba 30,000 kwa mwezi.
Flat rate, naunga mkono hoja. Hii ifanyike baada ya tathmini ya matumizi ya maji ya angalau ya miezi 6 ili kuweka uwiano sawa wa gharama za uendeshaji na matumizi ya maji.

Kusema kuwa bei iliyopo sasa ni kubwa, hapana. Tsh 1600 kwa lita 1000 na maji yanachezewa haswa, ingekuwa hata tsh 3000 kwa lita 1000 ili tujenge nidhamu ya kuyatumia.

Lakini pia, tuwe na mfumo wa kuyarudisha maji taka yote(yawe ya choo, bafu, kufulia n.k) kwenye baadhi ya matumizi baada ya kuyachakata na kuyafanya salama tena, angalau kwa matumizi ya mashamba, bustani, fire fighting system, na matumizi mengine yasiyohitaji maji safi na salama sana.

Wale wanaofisadi, wafilisiwe, mali ziingie kwenye miradi ya maji.
 
Kupata maji ya uhakika serikali ingejenga reservoirs katika majimbo. Reservoirs zikusanye maji ya mvua pamoja na ya mito.

Kuwe na kampuni binafsi zipate tenda ya kusambaza mabomba. Bill iwe flat rate mfano kila nyumba 30,000 kwa mwezi.
Elfu 30 bado ni nyingi
Wananchi wangepewa elimu ya kusave maji na bili ziwe halisi watu wasibambikwe bili za uwongo
Wananchi waelimishwe jinsi ya kusoma mita za maji mwezi unapoisha mtu anajua katumia unit ngapi na anadiwa kiasi gani
Unit 1 =dumu 50 kuzimaliza hizi kwa siku labda Kama una shamba unamwagilia
Ambapo kwa 1200 unit itakucost 36000 kwa mwezi
Kama unatumia dumu 25 kwa siku kwa mwezi utalipa elfu 18000
Dumu 16 ni elfu 9 mwezi
Sasa wengi wetu hatuna matumizi haya na tunalipa zaidi ya hapo ni nn shida
Shida nadhani sio bei ya maji
Ni watumishi na wananchi kutokuwa na elimu

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Serikali inatumia maji kama chanzo cha mapato. Gharama kubwa ya maji inapunguza matumizi kwa mwananchi. Kwa bei hizi mtu unasita kumwagilia hata mashina matatu ya mchicha au spinach.
 
Back
Top Bottom