Rais ajaye arudishe operation wahujumu uchumi

mdukuzi

JF-Expert Member
Jan 4, 2014
15,862
35,192
Nakumbuka enzi za mwalimu Nyerere kulikuwa na operation kabambe ya kukamata wahujumu uchumi na kutaifisha mali zao, watu walimwaga pesa mtoni kuepuka kukamatwa na wengine walitoroka nchi na mali zao kutaifishwa ,naomba rais ajaye arudie hili zoezi.
 
No prob, ombi lako nimelifikisha mezani kwake!. Hili ni jambo la muhimu sana, haswa pale inapotokea serikali ya kifisadi, iliyoingia madarakani kwa ufisadi, na inayoongozwa na mafisadi, huku ukiulea ufisadi kama njia pekee ya kubakia madarakani, ambapo mwakani tutaichagua tena kwa kishindo ili ianzishe operation wahujumu!.

Pasco
 
Athari za ile operation bado zipo hadi leo na bado zitaendelea kwa muda mrefu ujao. Unataka kuanzisha kidonda kingine juu ya kidonda cha zamani ambacho hakijapona?
 
Nakumbuka enzi za mwalimu Nyerere kulikuwa na operation kabambe ya kukamata wahujumu uchumi na kutaifisha mali zao, watu walimwaga pesa mtoni kuepuka kukamatwa na wengine walitoroka nchi na mali zao kutaifishwa ,naomba rais ajaye arudie hili zoezi.

Sheria ya kushughulikia wahujumu uchumi ipo tofauti na wakati wa nyerere ambapo mtu alikuwa akionyesha kidole tu kuwa yule ni mhujumu uchumi basi watu wanaanza kukimbiza mtu wa watu barabarani na maporini kama kibaka kuwa ni mhujumu uchumi.

Sasa hivi ukiwa na ushahidi kuwa mtu ni mhujumu uchumi anapelekwa mahakamani kuhukumiwa hahukumiwi barabarani kama wakati wa nyerere.Sasa hivi nchi inaongozwa na sheria sio mihemuko ya kisiasa,hisia na mob justice.
 
Sheria ya kushughulikia wahujumu uchumi ipo tofauti na wakati wa nyerere ambapo mtu alikuwa akionyesha kidole tu kuwa yule ni mhujumu uchumi basi watu wanaanza kukimbiza mtu wa watu barabarani na maporini kama kibaka kuwa ni mhujumu uchumi.

Sasa hivi ukiwa na ushahidi kuwa mtu ni mhujumu uchumi anapelekwa mahakamani kuhukumiwa hahukumiwi barabarani kama wakati wa nyerere.Sasa hivi nchi inaongozwa na sheria sio mihemuko ya kisiasa,hisia na mob justice.
umejibu vema mkuu
 
Nakumbuka enzi za mwalimu Nyerere kulikuwa na operation kabambe ya kukamata wahujumu uchumi na kutaifisha mali zao, watu walimwaga pesa mtoni kuepuka kukamatwa na wengine walitoroka nchi na mali zao kutaifishwa ,naomba rais ajaye arudie hili zoezi.

Hilo hakuna analiweza zaidi ya EL,ndio mtu pekee anayeweza sema na kutenda,so tumuombee MUNGU huyu ndugu CCM impitishe na tuweze kuwa na RAIS makini na mwenye focus hawa wengine kiukweli mimi binafsi sijaona bado kwani itakuwa business as usual
 
Nakubaliana na wewe kwenye hili kunawatu wanahitajika kushughurikiwa sana siyo polepole.
 
Hilo hakuna analiweza zaidi ya EL,ndio mtu pekee anayeweza sema na kutenda,so tumuombee MUNGU huyu ndugu CCM impitishe na tuweze kuwa na RAIS makini na mwenye focus hawa wengine kiukweli mimi binafsi sijaona bado kwani itakuwa business as usual
EL ataweza kweli hapo maana na yeyey yanasemwa semwa .......
 
Nakumbuka enzi za mwalimu Nyerere kulikuwa na operation kabambe ya kukamata wahujumu uchumi na kutaifisha mali zao, watu walimwaga pesa mtoni kuepuka kukamatwa na wengine walitoroka nchi na mali zao kutaifishwa ,naomba rais ajaye arudie hili zoezi.

Hapo labda kubadili chama lakini ni ndani ya CCM hakuna atakaechaguliwa kuwa Rais asiwe amepita bila kuhonga wapiga kura, akishahonga hatakuwa na courage ya kusema wahujumu uchumi wafilisiwe. Mfano Lowassa hawezi kupanda jukwaani akakemea watu wasile rushwa, watamshangaa sana akikemea rushwa
 
Uhujumu uchumi umeisaidia nini nchi yetu zaidi ya kuwakimbiza wafanyabiashara nje ya nchi na sisi wananchi mpaka leo tunaiona athari yake.Uganda mpakaleo inawaita wafanyabiashara waliotaifishiwa mali zao waje warudishiwa wamestarehe huko waliko.Huwezi kumnyanganya mtu mali yake na ukampa mtu hahusiki nayo.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom