Rais aagiza gereza la Songwe lihamishwe ili kuchimbwa madini ya bati

Ochu

JF-Expert Member
May 13, 2008
975
47
Na Hawa Mathias, Mbeya

RAIS Jakaya Kikwete ameitaka serikali mkoani Mbeya kufanya uwezekano wa kuhamisha gereza la Songwe na kulibomoa ili kuanza uchimbaji wa madini ya alminium ambayo yamebainika kuwepo katika ardhi ya gereza hilo.

Kikwete alisema hayo juzi katika ikulu ndogo mkoani Mbeya mara baada ya kutoka katika ziara ya kutembelea kata ya Ilembo mkoani humu.

Alisema ni kitu kisichowezekana kama uchumi wa wananchi kushuka wakati kuna rasilimali nyingi za madini ambayo yanaweza kuinua uchumi wa wananchi wa mkoa huo, hivyo wafungwa waliopo wahamishwe katika magereza mengine na kutafuta eneo la kujenga gereza hilo.

''Ni muhimu viongozi wa serikali ya mkoa kuchukua jukumu la haraka kutekeleza hili na si kuacha rasilimali za kukuza uchumi zikakaa bila kuzalisha na kubaki kwenye ardhi,'' alisema Kikwete.

Aliongeza kuwa; ''Kwa sasa tunapaswa kufanya mikakati ya kubomoa gereza la Songwe na kujenga eneo lingine kisha kuanza uchimbaji rasmi kutokana na eneo hilo kuonekana kuwa na madini mengi ambayo yanaweza kuongeza pato la nchi na kukuza uchumi''.

Aidha alimwagiza Mkuu wa Mkoa , John Mwakipesile kuanzisha mradi wa matunda aina ya 'apple' yanayolimwa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini na si kutegemea yanayozalishwa kutoka nje wakati nchi ina uwezo wake binafsi.

Wakati huo huo Rais Kikwete alisema serikali imesitisha ununuzi wa magari na badala yake fedha hizo zitatumika kununua vifaa vya kilimo ili kuboresha sekta hiyo.
 
Madini yaliyopo pale ni madini yenye thamani sana na hutumika kama raw materials za kujenga ndege. Ni madini adimu sana na hupatikana Australia tu. Kampuni ya Afrika Kusini ndio yenye leseni pale Songwe. Wamefanikiwa kumshawishi Rais kuhamisha gereza?..................... haya tusubiri tuone!
 
Madini yaliyopo pale ni madini yenye thamani sana na hutumika kama raw materials za kujenga ndege. Ni madini adimu sana na hupatikana Australia tu. Kampuni ya Afrika Kusini ndio yenye leseni pale Songwe. Wamefanikiwa kumshawishi Rais kuhamisha gereza?..................... haya tusubiri tuone!

Mh. Zitto,

Kwa nini wasema wamefanikiwa kumshawishi Rais? Kuna nini hapo? Kwa nini useseme wamefanikiwa kushawishi serikali?
 
Madini yaliyopo pale ni madini yenye thamani sana na hutumika kama raw materials za kujenga ndege. Ni madini adimu sana na hupatikana Australia tu. Kampuni ya Afrika Kusini ndio yenye leseni pale Songwe. Wamefanikiwa kumshawishi Rais kuhamisha gereza?..................... haya tusubiri tuone!


Mkuu wa idara Zito,

Wakati tunasoma pale MBY tulikuwa tunaambiwa kuwa chini ya gereza la Songwe kuna madini ya Uranium na Mwalimu Nyerere aliuwa anatambua hilo ndo maana akaamua kujenga Gereza ili kuyalinda hayo madini! ahaa sasa ndo tunapata ukweli kumbe ni Aluminium sio Uranium!. Tuone basi ni jinsi gani nchi yetu itakavyonufaika basi.

Amani.
 
hizo ni porojo tu !!! Aluminium ni madini yanayo chimbwa sehemu nyingi tu duniani !!! gabon ndo inayoongoza kwa uzalishaji... hapa tanzania yapo mbeya,na tanga lushoto....je kunafaida gani kuukalia uchumi wakati wananzengo wanatokomea kwa umasikini ?? do not be negative for verything guys!!!!


Tanzania will never develop under ccm
 
Madini yaliyopo pale ni madini yenye thamani sana na hutumika kama raw materials za kujenga ndege. Ni madini adimu sana na hupatikana Australia tu. Kampuni ya Afrika Kusini ndio yenye leseni pale Songwe. Wamefanikiwa kumshawishi Rais kuhamisha gereza?..................... haya tusubiri tuone!

Zitto,

Kwa hiyo unachosema inayopatikana pale si Aluminum? Maana kama ni Aluminum mbona ipo sehemu nyingi tu? Unasema hatupewi habari yote?
 
nahisi kuna uranium ila wanaficha ukweli......JK aangalie asiingie kwenye viatu vya mkapa vya kuuza raslimali.
 
Madini yaliyopo pale ni madini yenye thamani sana na hutumika kama raw materials za kujenga ndege. Ni madini adimu sana na hupatikana Australia tu. Kampuni ya Afrika Kusini ndio yenye leseni pale Songwe. Wamefanikiwa kumshawishi Rais kuhamisha gereza?..................... haya tusubiri tuone!

Khaaa yaani leseni imetolewa wakati gereza liko pale...duuh kweli rais tunaye
 
hizo ni porojo tu !!! Aluminium ni madini yanayo chimbwa sehemu nyingi tu duniani !!! gabon ndo inayoongoza kwa uzalishaji... hapa tanzania yapo mbeya,na tanga lushoto....je kunafaida gani kuukalia uchumi wakati wananzengo wanatokomea kwa umasikini ?? do not be negative for verything guys!!!!


Tanzania will never develop under ccm

hujui unachoongea wewe
 
Mh. Zitto,

Kwa nini wasema wamefanikiwa kumshawishi Rais? Kuna nini hapo? Kwa nini useseme wamefanikiwa kushawishi serikali?

Kasema hayo kwa kuwa wana access na Rais na ni yeye ana waachia wanaua watu kuanzia Tarime nk na sasa gereza lina hamishwa , gharama kuhamisha na kujenga jipya mchumi JK kaziona ?
 
Laini mimi kwa maoni yangu kuchimba siyo tatizo tatizo ni mikataba ambayo haizingatii maslahi ya wananchi/nchi. Namshauri JK kabla hawa watu hawajachimba basi wajenge sekondari za hadhi 5, shule za msingi za hadhi 10, wajenge hospitali kubwa 1 mjini mbeya na ndogo hapo hapo songwe, wahakikishe umeme wa gridi unaletwa eneo hilo na wajenge bara bara za lami maeneo yote ya mbeya.

Haya mambo lazima yawe kwenye mkataba
 
Kasema hayo kwa kuwa wana access na Rais na ni yeye ana waachia wanaua watu kuanzia Tarime nk na sasa gereza lina hamishwa , gharama kuhamisha na kujenga jipya mchumi JK kaziona ?

kwa nini hao waliopewa leseni wasijenge gereza jipya kwa pesa yao?? Hivi kweli JK anatumia akili?? iweje anayetaka madini asiingie gharama ya kujenga hilo gereza na badala yake kodi zetu ndo zijenge???

Naungana na mtu aliye sema Tanzania will never, ever get economic development under CCM
 
hujui unachoongea wewe

Kigogo,

Pengine wewe ndio hujui unachoongea, mimi nakubaliana na Mzee wa Usafi.

Soma haya maneno kutoka website ya Alcoa, one of the leading mining companies. Aluminum= American spelling of Aluminium.

http://www.alcoa.com/ingot/en/info_page/making_mining.asp

Aluminum is one of the most plentiful metals in the earth's crust.
It is naturally found in the form of bauxite, an ore containing aluminum oxide, or alumina. We surface mine bauxite from reserves in Australia, Brazil, Suriname, Jamaica and other parts of the world, processing most of it into alumina. In 2003, Alcoa consumed 30.8 million metric tons (mt) of bauxite from its own reserves, 6.9 million mt from related third parties and 1.9 million mt from unrelated third parties.

Zaidi ya hizi sehemu zilizotajwa hapa mimi najua kuna machimbo Guinea na Canada (British Columbia) haya madini yapo katika kila continent la dunia hii, kwa hiyo kama tunaongelea Aluminum hii habari ya kwamba inapatikana Australia tu inabidi isahihishwe.

Labda kama mnaongelea madini mengine, which will essentially amount to saying the president is not giving the full story and hence carry the connotation of accusations of sleaze.

Mtu anayejulikana kama Mbunge kaja na huu mchongo.

Zitto, tueleze vizuri hapa.Unaongelea Aluminum na umeteleza tu kusema kwamba inapatikana Australia tu au kuna lingine ambalo wananchi hatulifahamu?

Zaidi ya yote, tungependa kujua mipango ya kimazingira itakayohakikisha uchimbaji hauathiri afya na maendeleo ya wananchi wa eneo hilo.Vile vile tungependa kujua mpango wa kumaintain na ku restore mazingira katika machimbo hayo.

One has to only look at ""You will know them by their trail of death" a Human Eye film on mining and its detrimental effects to indigeneous peoples to get spooked by these projects.I am not opposing mining, I just want everything to be done in a sustainable way. We should have picked up a lesson from North Mara.
 
Mimi nauliza kwamba JK aliondoka kwenda Mbeya akisema ziara kumbe ana lake jambo . Je ndilo hilo tu kuubw alilimpeleka kuwaha kikishia wazungu kwamba nitaenda na kutolea tamko huko ?

Jamani udhalilishwaji utamkwe wazi maana jamaa wana dhalilisha mno watu wetu .
 
Kigogo,

Pengine wewe ndio hujui unachoongea, mimi nakubaliana na Mzee wa Usafi.

Soma haya maneno kutoka website ya Alcoa, one of the leading mining companies. Aluminum= American spelling of Aluminium.

http://www.alcoa.com/ingot/en/info_page/making_mining.asp



Zaidi ya hizi sehemu zilizotajwa hapa mimi najua kuna machimbo Guinea na Canada (British Columbia) haya madini yapo katika kila continent la dunia hii, kwa hiyo kama tunaongelea Aluminum hii habari ya kwamba inapatikana Australia tu inabidi isahihishwe.

Labda kama mnaongelea madini mengine, which will essentially amount to saying the president is not giving the full story and hence carry the connotation of accusations of sleaze.

Mtu anayejulikana kama Mbunge kaja na huu mchongo.

Zitto, tueleze vizuri hapa.Unaongelea Aluminum na umeteleza tu kusema kwamba inapatikana Australia tu au kuna lingine ambalo wananchi hatulifahamu?

Zaidi ya yote, tungependa kujua mipango ya kimazingira itakayohakikisha uchimbaji hauathiri afya na maendeleo ya wananchi wa eneo hilo.Vile vile tungependa kujua mpango wa kumaintain na ku restore mazingira katika machimbo hayo.

One has to only look at ""You will know them by their trail of death" a Human Eye film on mining and its detrimental effects to indigeneous peoples to get spooked by these projects.I am not opposing mining, I just want everything to be done in a sustainable way. We should have picked up a lesson from North Mara.

Mkuu uko sahihi, ili ni kosa ambalo wengi huwa wanafanya. si kosa la Zitto tu, wametaja Aluminium kwa sababu may be ni familiar

Kuna compound(muunganiko), Aluminium ni mojawapo pamoja na madini mengine, yote yanaweza yakawa na thamani. Kutokana na kutokujua basi inapelekea wengi kutaja jina la aina moja tu ya madini ambayo yanajulikana.

is very common mistake, ndio ikaleta hata yale matatizo ya mchanga kupelekwa Asia, watu hawajui , wanajua dhahabu, kumbe kuna madini mengi ndani yake, ambayo hayawezi kusafishwa hapa Tz.

Nitaleta jina lake soon, kwanza nicheki
 
Back
Top Bottom