Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,428
Wakati fulani wanasiasa hulazimika kufanya mambo tete, ila mara nyingi hata wao wenyewe wanakuwa hawayapendi, hayawafurahishi na yanawakosesha usingizi ila inawapasa kufanya na kuigiza kama wanafurahia kwa sababu ya 'Customer needs'.
Mwanasiasa ni sawa na mtoa huduma mwingine yoyote tu, huwezi kutoa huduma kama haina wahitaji, hata iwe nzuri kiasi gani utakwama na mwishowe utajikuta ukilazimika kuacha kutoa huduma unayotoa au kutafuta huduma ambayo mteja wako anataka ndio ummpe (hata kama ni mbaya).
Kama mteja wako anasuuzika roho yake akiona unamdhalilisha mtu mwingine kwa mfano, kama unataka kumfurahisha mteja, inabidi utafute mtu umdhalilishe na mteja ajue umefanya hivyo. Usipofanya hivyo utapotea kwenye ‘game’
Kama mteja anataka kusikia majungu , na wewe unataka kumshika, mpe majungu, vinginevyo tafuta kazi nyingine yakufanya.
Kama mteja anataka kudanganywa, mdanganye, vinginevyo hatakukubali, na kama lengo lako ni kukubalika utakuwa umekwama. N.k
Mtiririko huu unaendelea hivyo kwenye kila jambo na mwishowe kusababisha mzunguko wa tatizo “Problem cycle” Mwananchi anasema yupo alivyo kwa sababu wanasiasa si watu wazuri, mwanasiasa anasema anafanya afanyavyo kwa sababu ya wananchi.
Wakuu,Watanzania wengi tuna mitizamo hasi karibu kwenye kila kitu na hapo ndio msingi wa shida nyingine zote unapoanzia. Matatizo mengi katika nchi yanasababishwa na raia na sio viongozi wa kisiasa. Kiongozi ni sawa na dereva ambaye kakodishwa anaenda wanakoenda abiria (haijalishi sana kama anapenda kwenda huko au laa).
Mara nyingi wanasiasa husoma upepo wa raia wanavyofikiri na kuenda nao. Kwa hiyo kitu pekee kinachoweza kuleta uhakika wa kesho iliyo bora, ni raia kubadili mitizamo na tabia kwenye mambo ya msingi vinginevyo, hakuna namna ya kukomesha mzunguko unaotajwa hapo juu.
Mwanasiasa ni sawa na mtoa huduma mwingine yoyote tu, huwezi kutoa huduma kama haina wahitaji, hata iwe nzuri kiasi gani utakwama na mwishowe utajikuta ukilazimika kuacha kutoa huduma unayotoa au kutafuta huduma ambayo mteja wako anataka ndio ummpe (hata kama ni mbaya).
Kama mteja wako anasuuzika roho yake akiona unamdhalilisha mtu mwingine kwa mfano, kama unataka kumfurahisha mteja, inabidi utafute mtu umdhalilishe na mteja ajue umefanya hivyo. Usipofanya hivyo utapotea kwenye ‘game’
Kama mteja anataka kusikia majungu , na wewe unataka kumshika, mpe majungu, vinginevyo tafuta kazi nyingine yakufanya.
Kama mteja anataka kudanganywa, mdanganye, vinginevyo hatakukubali, na kama lengo lako ni kukubalika utakuwa umekwama. N.k
Mtiririko huu unaendelea hivyo kwenye kila jambo na mwishowe kusababisha mzunguko wa tatizo “Problem cycle” Mwananchi anasema yupo alivyo kwa sababu wanasiasa si watu wazuri, mwanasiasa anasema anafanya afanyavyo kwa sababu ya wananchi.
Wakuu,Watanzania wengi tuna mitizamo hasi karibu kwenye kila kitu na hapo ndio msingi wa shida nyingine zote unapoanzia. Matatizo mengi katika nchi yanasababishwa na raia na sio viongozi wa kisiasa. Kiongozi ni sawa na dereva ambaye kakodishwa anaenda wanakoenda abiria (haijalishi sana kama anapenda kwenda huko au laa).
Mara nyingi wanasiasa husoma upepo wa raia wanavyofikiri na kuenda nao. Kwa hiyo kitu pekee kinachoweza kuleta uhakika wa kesho iliyo bora, ni raia kubadili mitizamo na tabia kwenye mambo ya msingi vinginevyo, hakuna namna ya kukomesha mzunguko unaotajwa hapo juu.