Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Hii ni nchi ya ajabu sana ambayo kila kukicha inakuja na mikakati ya kufukarisha raia wake kwa visingizio vya wapishe maendeleo kama vile raia siyo sehemu ya hayo maendeleo............................. Matokeo yake raia husukumwa nje ya maendeleo kwa maana ya huduma muhimu na kupunjwa fidia ya thamani khalisi ya mtaji aliouwekeza kwenye shughuli zake kama vile nyumba, shamba na maendeleo mengineyo........................ La ajabu kabisa huyo mwekezaji anayepishwa huwa halazimishwi na sera/sheria kuwafidia waathirika wake kwa hasara ya kunyimwa kivuno cha matarajio yajayo ya waathirika......athariza kimazingira, uchumi, afya n.k hujitokeza....zikiwemo hasara ya kukosa huduma muhimu ambazo sasa yabidi wazifuate mbali na gharama nyinginezo ambazo sasa zinakuwa zimebinafsishwa kwa huyu mwekezaji....................na kuwa faida ambayo mwekezaji hata anakuwa hajaipanda..... kwa hiyo huvuna asichopanda wala kustahili.....na mwaathirika huwa amesahaulika kabisa!!!!!!!!!!!!!!!! Ushauri Tunahitaji sera ambazo zitamtambua raia mwathirika kama sehemu ya huo uwekezaji mpya ili aendelee kuvuna na kumpunguzia makali ya kupisha maendeleo......kumtambua apewe hisa naye awe sehemu ya umiliki wa huo uwekezaji na kwahiyo hajapisha maendeleo bali naye amekuwa sehemu ya maendeleo kama kweli yapo! Tusipofanya hivyo kwa kuwapa hisa watu wetu kwenye mitaji ya maendeleo tajwa...ina maana baada ya miaka kama 20 hivi ijayo sehemu kubwa ya raia wetu watakuwa wakimbizi wa kiuchumi ndani ya nchi yao................ Kwa minajili ipi tuaafiki na khali hiyo?