Raia wa Kenya wanaoishi Tanzania wahakikishiwa Usalama na kuhimizwa kufuata Sheria za nchi

Raia wa Kenya wanaoishi Tanzania wahakikishiwa Usalama na kuhimizwa kufuata Sheria za nchi

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,943
Reaction score
2,981
Ubalozi wa Kenya jijini Dar es Salaam umeihakikishia raia wa Kenya wanaoishi nchini Tanzania kuhusu usalama wao, kufuatia machafuko yaliyotokea baada ya uchaguzi mkuu

Kupitia taarifa iliyotolewa Novemba 5, 2025, Ubalozi huo ulisema kuwa ustawi wa Wakenya walioko Tanzania unabaki kuwa kipaumbele chake kikuu, na kwamba mazungumzo yamefanyika na mamlaka za Tanzania ili kuhakikisha ulinzi wao unadumishwa.

Ubalozi unawahimiza Wakenya walioko Tanzania kuendelea na shughuli zao za kawaida kwa mujibu wa sheria,” ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo

Ubalozi huo uliongeza kuwa umeanza tena shughuli zake za kawaida baada ya kufutwa kwa amri ya kutotoka nje usiku na vizuizi vilivyowekwa Oktoba 29, wakati wa uchaguzi uliofuatwa na maandamano.

Aidha, raia wa Kenya wamehimizwa “kubaki watulivu, waangalifu, na kuzingatia sheria za nchi,” huku wakitakiwa kuripoti mara moja changamoto zozote za kiusalama kwa Ubalozi kupitia namba za simu +255 22 2668285/6.

Hali ya Siasa Tanzania

Rais Samia Suluhu Hassan, licha ya machafuko na kuzimwa kwa mtandao wa intaneti baada ya maandamano ya uchaguzi, aliapishwa kushika madaraka mnamo Oktoba 3 katika Ikulu ya Dodoma, akiwa na Naibu wake Emmanuel Nchimbi.

Ushindi wake umekumbwa na upinzani mkali kutoka chama kikuu cha upinzani, CHADEMA, ambacho kilizuiwa kushiriki uchaguzi huo na sasa kinataka uchaguzi mpya, kikidai kuwa uchaguzi wa Oktoba 29 ulikuwa “udanganyifu mkubwa.”

Tume ya Uchaguzi ilitangaza kuwa Rais Samia alipata asilimia 98 ya kura zote.

Waangalizi wa uchaguzi na watetezi wa haki za binadamu wametaja uchaguzi huo kuwa na kasoro nyingi, wakimtuhumu Rais Samia kwa kuamuru mauaji ya vijana waliokuwa wakishiriki maandamano.

Ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) uliripoti kuwa wajumbe wake walikumbana na vitendo vya unyanyasaji, na walibaini kasoro nyingi katika mchakato wa uchaguzi huo.

Asasi za kiraia zikiwemo Muungano wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) zimelaani mauaji ya waandamanaji, zikisema matukio hayo yameharibu taswira ya taifa na kudhoofisha imani ya umma kwa serikali

Source: Citizen Kenya
 
Back
Top Bottom