Raia Mwema: Makonda Kibarua kizito, wengine wajitokeza kumshitaki

Katiba ya Tanzania hairuhusu Makonda kushtakiwa kwa sababu ili ufanikiwe kumshtaki Makonda lazima serikali iridhie/ikubali/ipitishe mashtaka hayo kupitia DPP.

Hii maana yake ni kwamba kama serikali haitaki umshtaki Makonda basi hutaweza kumshtaki makonda hata kama alifanya makosa ya wazi na makubwa kiasi gani.Maana yake serikali imehodhi haki za watu.

Kama Serikali ilikuwa haitaki Sabaya ashtakiwe basi hadi leo Sabaya angekuwa uraiani.Aliemshtaki na kumfunga Sabaya ni Serikali na siyo mtu mwingine yoyote yule.Kama siyo Serikali hapakuwa na wa kumshtaki wala kumgusa Sabaya.

Lakini baya zaidi ni kwamba Serikali ina uwezo wa kumshtaki yoyote yule na kumweka ndani bila dhamana(kwa makosa yasiyo na dhamana) hata kama mtu huyo hajatenda makosa haya na hakuna ambae anaweza kuizuia serikali katika hilo.

Nafikiri sasa unaweza kuona ni kwa nini tunahitaji katiba mpya.
Ukweli ni kwamba siku atakapofikishwa kizimbani mtaona atakavyoshambuliwA na wananchi. SERIKALI ITAPIMA UPEPO UTAKAVYOKUA..KAMA ITAONA WATU WENGI WANAMWELEKEO KWAMBA JAMAA AFUNGWE BASI, kesi haitafutw ili kukidhi haja ya wananchi. Kumbukeni Sirikali ikishakutumia kukutupa jalalani pia ni rahisi. Hvyo Hii kesi ni fifty fifty. Subilini!!
 
View attachment 2031158

Gazeti la Raia Mwema limeripoti kuwa watu wengine wamejitokeza kumshitaki aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Mfanyabiashara mmoja amenukuliwa na gazeti hilo akisema "Makonda ametufanyia mambo mengi kinyume na sheria za nchi. Kuna wakati baadhi yetu, tulijaribu kumshitaki, lakini tukatishwa na baadhi ya waliojitambulisha kuwa maofisa wa Serikali hivyo tukalazimika kurudi nyuma"
Mkuu ,gazeti la raia mwema usilifuate unapoteza MDA mkuu
 
Sasa akishitakiwa atashitakiwa kama nani? Akiruka akasema yeye si makonda bali ni bashite na vyeti akawa anavyo mbona anashinda kesi mapema tu.
 
Katiba ya Tanzania hairuhusu Makonda kushtakiwa kwa sababu ili ufanikiwe kumshtaki Makonda lazima serikali iridhie/ikubali/ipitishe mashtaka hayo kupitia DPP.
Tunaomba kifungu cha katiba mkuu ambacho kinachompa Makonda kinga ya kutoshitakiwa.

Ama tumpe elimu ni kwa vipi hawezi kushitakiwa.
 
Back
Top Bottom