Raia Mwema hatarini kufungiwa makala 'kila awamu ina rekodi ya kuua', mtego kwa JK

Tina

JF-Expert Member
Jul 9, 2007
572
579
Leo nilipita hapa Dar Wizara ya Habari kwa mambo binafsi, nikakutana na taarifa kwamba gazeti la Raia Mwema limeandikiwa barua kutishiwa kufungiwa. Nikadodosa, nikaambiwa ni kuhusu makala isemayo, "KILA AWAMU INA REKODI YA KUUA, Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete...." nikanunua gazeti na kuisoma na kuona ni nzuri na imeandikwa kitaalamu sana na mwandishi "Msomaji Raia" ambaye alipotea sana akielezwa kuwa nje ya nchi kwa matibabu kabla ya kurejea na kuanza kuandika na hii ilikuwa makala yake ya kwanza tokea augue.

Kabla hata ya kusoma na kuondoka Wizara ya Habari, nikasikia mmoja wa maofisa akisema maneno haya, "unajua hii ni hatari sana, maana itakuwa ni sawa na kuisambaza hiyo makala na si kuizuia. Hata wale ambao hawakuisoma sasa wataitafuta na kuisoma. Raia Mwema limekuwa makini katika kutushambulia na limetusaidia sana katika vita ya ufisadi, lakini sasa tukigombana nao, tutakuwa tunamharibia Rais (JK) badala ya kumsaidia, na kwa kutumia jina lake badala ya majina ya marais wote waliotajwa, tutazidi kumchonganisha na wananchi na hata na hao wastaafu na familia zake na tutaonekana ni wabinafsi na Rais ataonekana mbinafsi na anajitetea mwenyewe. Tumefanya kosa kuwaandikia barua, tungawaita tu tukazungumza nao."..... mzungumzaji huyo naona hakupata support yoyote na wenzake walioendelea na kazi zao hadi naondoka eneo hilo na kwenda kusima makala husika.


Nimemuomba mshikaji wangu wa Maelezo nakala ya barua akinipa nitairusha hapa. Wahusika hata ndani ya maelezo naomba watusaidie kuweka barua hiyo hapa kama hawatojali. Nasikia kosa lao ni kusema JK CCM itamfia mikononi kwa kukuthiri kwa ufisadi ndani ya CCM tokea mchakato wa 2005 na ndio maana anapata kigugumizi kuwashughulikia.

Maoni yangu;

Ni kweli kwamba gazeti la Raia Mwema limekua likiegemea sana upande wa JK hasa katika vita inayoendelea ndani ya CCM kati yake na mafisadi na sitoshangaa kusikia kwamba huo ni mkakati wa mafisadi kulidhibiti ama kulichonganisha na JK na hapo watakuwa wamefanikiwa mambo yao, kwani vyombo vingi wameshavishika ama kupandikiza watu. Sitoshangaa maana hata TBC iko mikononi mwa mafisadi na mambo yao huwa yanaenda kiulaini kuliko hata watawala.

letter(1).jpg
 
Kwa nini serikali isimfungulie huyo mwandishi kesi ya jinai kama vile yule wa T. Daima, pamoja na mhariri na mchapishaji?
 
Kwa nini serikali isimfungulie huyo mwandishi kesi ya jinai kama vile yule wa T. Daima, pamoja na mhariri na mchapishaji?

Inawezekana ndio lengo, ila ni kwa kuwa hawamfahamu ndio maana anaitwa kwanza Mhariri
 
Msomaji Raia hajulikani! Makala zake huwa nyingi ni za kumshambuli Rais. Twende nbele turudi nyuma jamaa huwa anaandika. Huyu namfananisha na Ukitaka Unaacha. Au ukitaka unaacha ndiye Msomaji Raia?
 
Binafsi naona serikali inaogopa kivuli chake tu. Jana kwenye taarifa ya habari itv polisi wameua raia wa3 bila kosa na wengine kujeruhiwa. Lakini mkuu wa wilaya ya Ulanga anatoa majibu mepesi kabisa eti hiyo ni ajali kama ajali zingine. Je nani mchochezi kati ya msomaji raia na maneno yanayotolewa na viongozi kama huyu mkuu wa wilaya na Chagonja kule Songea? Ni uwendawazimu kuminya haki za waandishi
 
Kwa sasa ni lazima busara itumike badala ya ubabe. Hii si ishara nzuri hata kidogo kwa fani ya uandishi wa habari. Tuwe makini sana.
 
Kwa sasa ni lazima busara itumike badala ya ubabe. Hii si ishara nzuri hata kidogo kwa fani ya uandishi wa habari. Tuwe makini sana.

Ukimsoma Msomaji raia, utagundua kuwa ni mtu yuko kwenye inner circle, makala ya juzi ilikuwa ni ya kwanza baada ya kuwa nje muda mrefu kwa matibabu, je huyu jamaa ni nani?
 
Bora Johson Mbwambo anayemkosoa hadharani kwa kumfananisha JK na Paul Kagame, kuhusu utawala wao au makala aliyoandika Kwa nini Kikwete hawaambii mawaziri hawa finito? kwani haamini hata Lowassa km alijiuzulu kwa utashi wake
Mimi ni msomaji wa Raia mwema nakubaliana kabisa sasa wanaikosoa Serikali ni sawa ni haki yao lakini sio kuwalazimisha waTZ matakwa yao ya wahariri, Habari za Kolimba, Katiba nk
 
Wajaribu kulifungia waone moto utakavyowawakia. Tanzania ya sasa inabadilika kwa kasi kubwa sana
 
Chonde chonde waandishi na wadau wa sekta hii tuungane kwa pamoja kuondoa(kupitia mabadiliko ya katib ayajayo) kifungu hiki cha sheria ya magazeti kinachompa waziri uwezo wa kufungia gazeti pindi 'akijisikia'.Waziri nchimbi akitumia hiki kipengele analifunga hili gazeti.

Byabato
 
nimesoma hii barua
lakini katika uandishi wa habari kwa lengo la kutafuta mlengo wa mwandishi huwezi kuhukumu makala kuwa imechochea au vinginevyo kwa kutumia aya moja katika makala nzima

lazima tutazame logic ya makala nzima.hapa ndipo wanasheria wanapaswa kusimamia !
 
Mimi nikifikri zaidi na zaidi.......
Wala makala hii si sababu, sababu ni Ulimwengu. Siku hizi ameanza kurusha makombora ya hapa na pale kwa JK, mengine yanaonekana kama kumdharirisha kabisa kwa mfano hivi karibuni aliandika kuwa raisi wa sasa ni kama anaomba Mungu kipindi chake kiishe tu maana hana kabisa mbinu yoyote ya kuiendeleza nchi!

Mhh! tusubiri!
 
Duh! Yaani jamaa makala yake ya kwanza tu toka atoke kwenye matibabu, mkwara mzito kutoka HUM. Hapa kuna kitu zaidi ya habari ya kichochezi.
 
Back
Top Bottom