Rai kwa vijana wenzangu wa UVCCM baada ya kukosa UDC

Pagan Amum

JF-Expert Member
Aug 28, 2015
1,932
4,395
Ni jambo lililo wazi kuwa tumepigwa. Tumeisoma namba kweli kweli. Matarajio yetu katika uteuzi wa wakuu wa wilaya hayakuwa haya. Haiwezekani ndani ya jumuiya uchukue watu 2 tu kuwa wakuu wa wilaya. Lazima tukubali tumepigwa... Mpaka sisi vijana 46 tuliopiganiaa chama kwenye mitandao katika uchaguzi mkuu tumeisoma namba. Kwa kweli tumepigwa!

Pamoja na hayo yote, naomba nitoe Rai yangu kwa vijana wenzangu wa UVCCM, tusikate tamaa, tuendelee kukipigania chama. Bado kuna nafasi na fursa nyingi sana, naomba tusikate tamaa, tuzidi kukipigania chama na jumuiya. Najua mmekwazika, na hata jana nimeona kwenye groups nyingi za whatspp left zimekuwa nyingi. Tafadhali msikate tamaa..

Mwisho, pamoja na kutokata tamaa, ni vyema tukajua Rais wetu wa sasa anapenda wasomi hivyo twendeni shule tupige kitabu, hapo ndipo tutaona matunda ya hii miaka 10...
 
....chama feki,wanachama feki,kumbe kelele zote mnazopiga huku huwa mnatetea matumbo yenu?!, na wala sio mapenzi yenu kwa nchi?!, ndio maana mkija kupewa ulaji na nyie mtageuka mafisadi kama wazee wenu!
Poor you!
Pole Lizaboni & Co!

Endeleeni kuisoma namba huku mkimwaga povu jf!
 
Msikate tamaa muongeze bidii ya kujitoa ufahamu zaidi jifunzeni kwa mwenzenu Makonda aliyeamua kumpiga makofi mzee Warioba na kupata u DC leo ni mkuu wa Mkoa.
 
Back
Top Bottom