Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Mmommose yuko New York na ujumbe wake toka Bunge la Tanzania
Shibuda na Ujumbe wake wakiwa Jamhuri ya Dominika pamoja na ujumbe wake. siku chache zilizopita.
Misafara si ya Kikwete tu ila hata wabunge wanatakiwa kupunguza safari za nje zinaigharaimu mno serikali. Kwangu binafsi sioni manufaa ya safari hizo wakati wanaporudi toka safarini hakuna mabadiliko yanayoonekana kutokana na kujifunza walikoenda, ni sawa na kwamba wanatalii tu.
Wabunge pamoja na kupata mishahara minono na posho za malaki kwa siku lakini bado wanang'ang'ania misafara ya nje ili kuongeza vitambi wakati mfanyakazi wa kawaida anakosa hata chai na chapati asubuhi anapoenda kazini.