Raha ya Maisha ni nin?

Gagurito

JF-Expert Member
Feb 11, 2011
5,600
803
Salamu tele toka kwangu ziwafikie popote mlipo wanaJF/MMU! Ni matumaini yangu tu salama na twasonga mbele ktk shughuri na majukumu yetu ya kila siku.

Leo ninajambo moja nitakalo lijadiliwe kwa pamoja, swala hili ni juu ya RAHA YA MAISHA NI NINI? wapendwa kuna watu wanaweza shangaa juu ya hili bt lengo langu kama mwanzisha thread ni kupata kufahamu Experience za watu juu ya maisha, just kushauriana hapa na pale juu ya maisha kwani nijuavyo mimi si sote tupatao raha, pia vitupavyo raha hutofautiana!

BINAFSI uwepo wa marafiki na upendo na ushirikiano nipatao toka kwa ndugu na Jamaa hunipa faraja na raha ya ajabu, napata kujisikia mtu katika watu, pia kinipacho raha kingine ni Afya na ulinzi nipatao toka kwa Mungu, kifupi ninaimani kubwa sana kwake!

Mmh! Sasa ni zamu yako, jaribu kuwa huru na muwazi, usione aibu na kuwa ruksa kusema chochote. JE NI NINI KIKUPACHO RAHA MAISHANI?
 
Je unaamini katika ile falsafa ya PESA NDIO KILA KITU? kwa nini? Kivipi?
 
Raha ni kitu ambacho kila mwanadamu anapenda asikie.... But Mungu alivo wa ajabu kaumba kila mwanadamu tofauti... hivo kumfanya kila mwanadamu awe na kile ambacho kinamkuna zaidi na kumpa raha.... Kile ambacho ni raha kwako ni karaha kwa mwingine na vice versa... Hivo basi Gagurito Raha ya Maisha hutofautiana kati ya mmoja na mwingine....

Sasa hapo kidogo umenichanganya kwenye post ya pili.... Ujue hio ni mada nayo independent kabisa na paana....
 
Umemjibu vyema Ashadii maana kitu kinaweza kuwa raha kwangu wakati kwako ni kero
Na kila mmoja ana kitu au mambo yanayomfanya awe na raha au huzuni ambayo kwa mwingine yanaweza kuwa vise versa
Ni the way unavyofanya kitu na wewe unavyojihisi
Pesa sio kila kitu bana u can have money na ukawa na huzuni maisha yako yote
U cannot buy happiness wala raha haiuzwi kwa pesa
 
Salamu tele toka kwangu ziwafikie popote mlipo wanaJF/MMU! Ni matumaini yangu tu salama na twasonga mbele ktk shughuri na majukumu yetu ya kila siku.<br />
<br />
Leo ninajambo moja nitakalo lijadiliwe kwa pamoja, swala hili ni juu ya RAHA YA MAISHA NI NINI? wapendwa kuna watu wanaweza shangaa juu ya hili bt lengo langu kama mwanzisha thread ni kupata kufahamu Experience za watu juu ya maisha, just kushauriana hapa na pale juu ya maisha kwani nijuavyo mimi si sote tupatao raha, pia vitupavyo raha hutofautiana! <br />
<br />
BINAFSI uwepo wa marafiki na upendo na ushirikiano nipatao toka kwa ndugu na Jamaa hunipa faraja na raha ya ajabu, napata kujisikia mtu katika watu, pia kinipacho raha kingine ni Afya na ulinzi nipatao toka kwa Mungu, kifupi ninaimani kubwa sana kwake!<br />
<br />
Mmh! Sasa ni zamu yako, jaribu kuwa huru na muwazi, usione aibu na kuwa ruksa kusema chochote. JE NI NINI KIKUPACHO RAHA MAISHANI?
Raha ni utamu.
 
Umemjibu vyema Ashadii maana kitu kinaweza kuwa raha kwangu wakati kwako ni kero
Na kila mmoja ana kitu au mambo yanayomfanya awe na raha au huzuni ambayo kwa mwingine yanaweza kuwa vise versa
Ni the way unavyofanya kitu na wewe unavyojihisi
Pesa sio kila kitu bana u can have money na ukawa na huzuni maisha yako yote
U cannot buy happiness wala raha haiuzwi kwa pesa

Kwasababu wengi matatizo yao ni tokana na hali mbaya ya maisha
kuto kimilisha yale wapendayo ndio maana wengi hufikiri pesa is everything,
kwa mwenye kubahatika na kuzipata anakuta kumbe sivo....
 
Raha ni kitu ambacho kila mwanadamu anapenda asikie.... But Mungu alivo wa ajabu kaumba kila mwanadamu tofauti... hivo kumfanya kila mwanadamu awe na kile ambacho kinamkuna zaidi na kumpa raha.... Kile ambacho ni raha kwako ni karaha kwa mwingine na vice versa... Hivo basi Gagurito Raha ya Maisha hutofautiana kati ya mmoja na mwingine....

Sasa hapo kidogo umenichanganya kwenye post ya pili.... Ujue hio ni mada nayo independent kabisa na paana....

Asha Dii,

Kuna raha moja sote twaipenda na twaiweza hata kwa vipato vyetu tafauti.......tutaifuatilia hadi tuipate
 
Raha ya maisha ni kupata kitu roho inapenda,usiwe na stress wala kunyanyaswa.
 
Hii inategemea na mtu mwenyewe lakini kwangu mimi raha ya maisha ni pale roho yangu inapokuwa imeridhika basi hapo ndipo ilipo amani ya nafsi yangu na ndipo ilipo furaha yangu!!
 
Kwasababu wengi matatizo yao ni tokana na hali mbaya ya maisha
kuto kimilisha yale wapendayo ndio maana wengi hufikiri pesa is everything,
kwa mwenye kubahatika na kuzipata anakuta kumbe sivo....

Yeah this is very true
Ila uhalisia sio huo kuna watu hawana pesa wala hawategemei sana hizo ila wana raha za ajabu
 
Asha Dii,

Kuna raha moja sote twaipenda na twaiweza hata kwa vipato vyetu tafauti.......tutaifuatilia hadi tuipate


Amini usiamini hio raha unayoisema hapa... kwa wengine hi kero hasa wanawake walozaliwa frigid ama kufanyiwa genital Mutilation....
 
Yeah this is very true
Ila uhalisia sio huo kuna watu hawana pesa wala hawategemei sana hizo ila wana raha za ajabu


Haswa!! Ndio maana yangu.. saingine UPENDO ni msingi wa raha, mara nyingi ukizungukwa na wapenzi wako ndugu na jamaa yenye amani na upendo... hata unapopata matatizo hioni karaha saana - hivo yaweza kua part ya raha....
 
Haswa!! Ndio maana yangu.. saingine UPENDO ni msingi wa raha, mara nyingi ukizungukwa na wapenzi wako ndugu na jamaa yenye amani na upendo... hata unapopata matatizo hioni karaha saana - hivo yaweza kua part ya raha....

nakubaliana na wewe
Ukiwa miongoni wa uwapendao na wakiw ana real lo-ve isiyochakachuliwa na bila unafiki unapata raha sana regardless yapo mambo mengi amnayo ni kikwazo kwenu ila kuna raha yake bana
Mambo mengine ni matokeo ya hapo maana bila upendo wa kweli hakuna raha
 
Back
Top Bottom