Rafiki yangu mpendwa amemuoa kipenzi changu wa sekondari

Dezoizo52

JF-Expert Member
Jan 30, 2017
514
1,043
Tulimaliza wote shule ya msingi pale majengo Nachingwea. Mimi na rafiki yangu hakika tulishibana na mungu akatujaalia tukafaulu Nachingwea day. Tukiwa form one nikapendana kwa dhati na bibie Zubeda, hakika tulipendana na rafiki yangu mpendwa alimuheshimu na kumjali. Wakati wa kurudi shule niliwapakia mpenzi wangu Zubeda na kwenye kitako alikaa rafiki yangu mpendwa.

Mwaka 1999 nilihamishwa shule nikahamia Ndanda sec hapa nikalazimika kuishi mbali na Zubeda daah hakika ilikuwa ni machungu mnoo. Nilimuaga rafiki yangu akae vizuri na nitakuja kila likizo kumuona Zubeda na rafiki yangu.Tuliendelea kuwasiliana kwa barua na kuonana hadi tulipomaliza shule 2001.

Nikasota na maisha ya ulimwengu na hatimae nikapata kazi mwaka 2003 na mwaka uliofuata nikatembelea nachingwea nikiwa nafuraha tele kwenda kumuona Zubeda tena nikiwa niko vizuri kama kijana nipo na gari ndogo corolla ae100. Nikaonana na Zubeda akalia sana kwani muda ulipita hatukuonana nikamuuliza kama ameshaolewa akanijibu hapana.

Tulifurahi tukaagana kwa miadi ya kuonana siku inayofuata. Siku ya pili nilianza kumtafuta rafiki yangu mpendwa tangu shule ili nimsalimie na nimpe michapo ya jana yake nilivyokutana na Zubeda na makiss tuliyofanya.

Nikaonana naye tukafurahi nikamuuliza kama ameshaoa akanijibu amemzalisha tuu mwanamke mmoja na kwa sasa yupo tuu. Nikaanza kumuhadithia juu ya nilivyokutana na Zubeda tulivyokiss na mambo mengi tuliyoahidiana lakini niliona kwa mbali rafiki yangu akiwa amebadilika na macho yakimuiva na kuwa mekundu basi nikawa sielewi nini kimemsibu nikaaga nikaelekea zangu bar moja hivi inaitwa the ganners.

Nikafika bar nikapiga moja moto na moja baridi baadae nataka kutoka nikaitwa jina langu kugeuka heee classmate wangu kasidi basi tukakumbushiana story za shule nikamwambia sasa ninamchuma na naelekea kwa miadi nikakutane na Zubeda. Kasidi alishangaa na akaniambia Zubeda amekwisha olewa na rafiki yangu mpendwa ambaye muda mfupi uliopita nimetoka kuongea nae akawa anawiva macho kwa story zangu kuhusu Zubeda.

Nimehadithia hii kwa kuwa muda umepita na nimewakumbuka sana rafiki yangu pamoja na Zubeda nawatakia waishi salama.
 
Ucmlaumu sana swahiba wako, maisha yana mengi sana ya kucmulia na huwezi jua nn kilitokea katika miaka yote ulokuwa mbali....
 
mkuu hapa nshakula castle 3 kwa hiyo story kama hizi zinanifanya niwaze mbaali coz we are sailing on the same boat
Ha haa! Wewe umekula kwa sababu zako binfasi. Ukitoka hapo asubuhi uende gym. Kitambi ni janga jingine katika ndoa za vijana wa kizazi hiki, hasa sababu ya ulevi na chips...
 
Pole sn mkuu ila nna iman ulishapata mwenza na una familia tayari,.
Cpati pcha baada ya kumcmulia rafk ako khs ulvyokis na zubeda cjui atakua alimpga au alimnunia jomoniii, ulimsababishia mararizo
 
Tulimaliza wote shule ya msingi pale majengo Nachingwea. Mimi na rafiki yangu hakika tulishibana na mungu akatujaalia tukafaulu Nachingwea day. Tukiwa form one nikapendana kwa dhati na bibie Zubeda, hakika tulipendana na rafiki yangu mpendwa alimuheshimu na kumjali. Wakati wa kurudi shule niliwapakia mpenzi wangu Zubeda na kwenye kitako alikaa rafiki yangu mpendwa.

Mwaka 1999 nilihamishwa shule nikahamia Ndanda sec hapa nikalazimika kuishi mbali na Zubeda daah hakika ilikuwa ni machungu mnoo. Nilimuaga rafiki yangu akae vizuri na nitakuja kila likizo kumuona Zubeda na rafiki yangu.Tuliendelea kuwasiliana kwa barua na kuonana hadi tulipomaliza shule 2001.

Nikasota na maisha ya ulimwengu na hatimae nikapata kazi mwaka 2003 na mwaka uliofuata nikatembelea nachingwea nikiwa nafuraha tele kwenda kumuona Zubeda tena nikiwa niko vizuri kama kijana nipo na gari ndogo corolla ae100. Nikaonana na Zubeda akalia sana kwani muda ulipita hatukuonana nikamuuliza kama ameshaolewa akanijibu hapana.

Tulifurahi tukaagana kwa miadi ya kuonana siku inayofuata. Siku ya pili nilianza kumtafuta rafiki yangu mpendwa tangu shule ili nimsalimie na nimpe michapo ya jana yake nilivyokutana na Zubeda na makiss tuliyofanya.

Nikaonana naye tukafurahi nikamuuliza kama ameshaoa akanijibu amemzalisha tuu mwanamke mmoja na kwa sasa yupo tuu. Nikaanza kumuhadithia juu ya nilivyokutana na Zubeda tulivyokiss na mambo mengi tuliyoahidiana lakini niliona kwa mbali rafiki yangu akiwa amebadilika na macho yakimuiva na kuwa mekundu basi nikawa sielewi nini kimemsibu nikaaga nikaelekea zangu bar moja hivi inaitwa the ganners.

Nikafika bar nikapiga moja moto na moja baridi baadae nataka kutoka nikaitwa jina langu kugeuka heee classmate wangu kasidi basi tukakumbushiana story za shule nikamwambia sasa ninamchuma na naelekea kwa miadi nikakutane na Zubeda. Kasidi alishangaa na akaniambia Zubeda amekwisha olewa na rafiki yangu mpendwa ambaye muda mfupi uliopita nimetoka kuongea nae akawa anawiva macho kwa story zangu kuhusu Zubeda.

Nimehadithia hii kwa kuwa muda umepita na nimewakumbuka sana rafiki yangu pamoja na Zubeda nawatakia waishi salama.
Hahaha marafik si watu wa sipoti sipoti asee
 
Tulimaliza wote shule ya msingi pale majengo Nachingwea. Mimi na rafiki yangu hakika tulishibana na mungu akatujaalia tukafaulu Nachingwea day. Tukiwa form one nikapendana kwa dhati na bibie Zubeda, hakika tulipendana na rafiki yangu mpendwa alimuheshimu na kumjali. Wakati wa kurudi shule niliwapakia mpenzi wangu Zubeda na kwenye kitako alikaa rafiki yangu mpendwa.

Mwaka 1999 nilihamishwa shule nikahamia Ndanda sec hapa nikalazimika kuishi mbali na Zubeda daah hakika ilikuwa ni machungu mnoo. Nilimuaga rafiki yangu akae vizuri na nitakuja kila likizo kumuona Zubeda na rafiki yangu.Tuliendelea kuwasiliana kwa barua na kuonana hadi tulipomaliza shule 2001.

Nikasota na maisha ya ulimwengu na hatimae nikapata kazi mwaka 2003 na mwaka uliofuata nikatembelea nachingwea nikiwa nafuraha tele kwenda kumuona Zubeda tena nikiwa niko vizuri kama kijana nipo na gari ndogo corolla ae100. Nikaonana na Zubeda akalia sana kwani muda ulipita hatukuonana nikamuuliza kama ameshaolewa akanijibu hapana.

Tulifurahi tukaagana kwa miadi ya kuonana siku inayofuata. Siku ya pili nilianza kumtafuta rafiki yangu mpendwa tangu shule ili nimsalimie na nimpe michapo ya jana yake nilivyokutana na Zubeda na makiss tuliyofanya.

Nikaonana naye tukafurahi nikamuuliza kama ameshaoa akanijibu amemzalisha tuu mwanamke mmoja na kwa sasa yupo tuu. Nikaanza kumuhadithia juu ya nilivyokutana na Zubeda tulivyokiss na mambo mengi tuliyoahidiana lakini niliona kwa mbali rafiki yangu akiwa amebadilika na macho yakimuiva na kuwa mekundu basi nikawa sielewi nini kimemsibu nikaaga nikaelekea zangu bar moja hivi inaitwa the ganners.

Nikafika bar nikapiga moja moto na moja baridi baadae nataka kutoka nikaitwa jina langu kugeuka heee classmate wangu kasidi basi tukakumbushiana story za shule nikamwambia sasa ninamchuma na naelekea kwa miadi nikakutane na Zubeda. Kasidi alishangaa na akaniambia Zubeda amekwisha olewa na rafiki yangu mpendwa ambaye muda mfupi uliopita nimetoka kuongea nae akawa anawiva macho kwa story zangu kuhusu Zubeda.

Nimehadithia hii kwa kuwa muda umepita na nimewakumbuka sana rafiki yangu pamoja na Zubeda nawatakia waishi salama.
Mkuu,kila niliposoma kisa chako nimetaman kujua nin kimetokea mbele.
Bas malizia nin kiliendelea ulipopata hiyo taarifa hapo the ganners
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom