Urassa sunday
Member
- Jan 30, 2020
- 28
- 121
Nimetumia masaa karibu 8 siku ya jumamosi tarehe 25/1/2020 kumpa ushauri wa kisaikolojia, rafiki yangu ambaye ijumaa ya tar 24/1/2020 alimfumania mkewe Gesti majira ya saa 1 jioni hapa Morogoro.
Mkewe aliaga anakwenda msibani amefiwa na mtoto wa binamu yake, hivyo siku ya kwanza alishinda humo mpk jioni. Ila siku ya pili yake ambayo ni ijumaa, mkewe aliaga anaenda kusaidia shughuli msibani lkn kumbe alifika asubuhi na kuzuga kufanya vishughuli vya hapa na pale kisha akaenda kwa jamaa fulani hiv ambaye ni mchepuko wake.
Mke wa jamaa alionekana akiwa anaingia gesti iliyopo mitaa ya Kihonda hapa Morogoro hivyo inasemekana kuna mtu aliyekuwa anamfahamu alivujisha taarifa kwa mumewe. Jamaa mwenye mke alikuwa mbali wilaya nyingine hivyo alichelewa kufika eneo la tukio mida ya saa 1jioni. Alipofika gesti alikuta jamaa ameshaondoka na mkewe alikuwa anamalizia kuvaa nguo.
Hivyo jamaa alimpiga sana mkewe mpk watu waliopo karibu walivamia chumbani na kuamua ugomvi. Hivyo jambo hili limemuuma sana jamaa kwani mpaka sasa amekuwa ni mtu wa mawazo na kulewa sana. Mke wake hajulikani alipokimbilia.
Wanawake tafadhalini sana heshimuni ndoa zenu!
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkewe aliaga anakwenda msibani amefiwa na mtoto wa binamu yake, hivyo siku ya kwanza alishinda humo mpk jioni. Ila siku ya pili yake ambayo ni ijumaa, mkewe aliaga anaenda kusaidia shughuli msibani lkn kumbe alifika asubuhi na kuzuga kufanya vishughuli vya hapa na pale kisha akaenda kwa jamaa fulani hiv ambaye ni mchepuko wake.
Mke wa jamaa alionekana akiwa anaingia gesti iliyopo mitaa ya Kihonda hapa Morogoro hivyo inasemekana kuna mtu aliyekuwa anamfahamu alivujisha taarifa kwa mumewe. Jamaa mwenye mke alikuwa mbali wilaya nyingine hivyo alichelewa kufika eneo la tukio mida ya saa 1jioni. Alipofika gesti alikuta jamaa ameshaondoka na mkewe alikuwa anamalizia kuvaa nguo.
Hivyo jamaa alimpiga sana mkewe mpk watu waliopo karibu walivamia chumbani na kuamua ugomvi. Hivyo jambo hili limemuuma sana jamaa kwani mpaka sasa amekuwa ni mtu wa mawazo na kulewa sana. Mke wake hajulikani alipokimbilia.
Wanawake tafadhalini sana heshimuni ndoa zenu!
Sent using Jamii Forums mobile app