Rafiki yangu akisikia mziki anaoupenda anaucheza bila kujali eneo, je ni pepo?

Jamaa sio mnafiki, anafanya ile mwili wake unataka na si kuangalia binadamu wa pembeni.Sio kwamba wewe hutaki kucheza ukisikia kamuziki unakokapenda ila kinachokufanya usicheze ni ile watanionaje.
Ni kweli lakini inakuwa kama utoto sasa,
 
Bora yy ana open hisia zake anywhere any time ,kuliko ukawa unataman kitu alafu una ogopa watu watasemaje...
kuna vitu vingine kujisitiri ni muhimu, unaweza ukawa na uwezo wa kupiga sahani tatu lakini inabidi ujivunge kidogo kwenye baadhi ya matukio ili usionekane mlafi
 
Huyu ni rafiki yangu tangia zamani na mpaka leo tupo karibu, tunafanya nae kazi shirika moja na ni moja ya marafiki zangu wachache ambao tumejuana muda mrefu.

Sasa huyu rafiki yangu anapenda sana muziki kuucheza tangu sekondari, huko chuo ndio kabisa alikuwa mzee wa disco sana, na hata nilipofatilia historia yake hata huko shule ya msingi alikuwa hivi hivi.

Yaani iwe ni barabarani, kwenye hafla, gari la matangazo lipite, iwe ni hafla 9kasoro misiba) n.k Akisikia mziki anaoupenda atacheza tu, Kumzua ni kazi sana.

Pia ukizingatia na umri umeenda saizi ni 31 anaingia kiukweli inakuwa taabu kidogo, Leo tulikuwa tumetoka kazin watu wanne hivi kwenda ofisi ya nje ya mji kidogo kikazi, Tulipofika huko kwenye tulipokelewa vizuri mziki si ukapiga bwana, eh mwenzetu aliona sehemu ambayo tupo nae ni kama hakuna uwazi, alienda mbele nafasi ya wazi kidogo akaanza kujitumbuiza kwa kucheza muziki, kiukweli hata wageni wengine walishangaa, baadhi walikuja kutuuliza kama huyu rafiki yangu anafanya kazi na sisi au tumemleta tu kama afiki.

Kiukweli hadi saa nyingine unaweza kuogopa kutembea nae, maana mnaweza kuwa kwenye shughuli ya heshima kidogo unawaza tu hivi dj akipiga ngoma anazopenda jamaa itakuwaje sasa.

Je, hii ni kawaida?

Ni tiba ya Kisaikolojia Kwake kutokana na yanayomsibu Kichwani ( Ubongoni ) Kwake.

Tena Shukuru akiwa anasikia Nyimbo azipendazo anafurahia na Kuzicheza kwani hizo nyingi angeweza hata Kufanya Jambo baya na msingsamini.

Tatizo la Kisaikolojia ni Kubwa Tanzania.
 
Ulevi ni ulevi. Tumbaku haramu,pombe,ulafi,uzinifu,kupiga chabo,mwizi,nk. Huo nao ni ulevi kupenda kuliko vuka kiwango.
 
Mimi nilitikisa kichwa ukweni,nilipoisikia nyimbo ya Diamond jeje,kumbe mamkwe ananichora tu

Kukutanisha macho,akatabasamu na kuinuka lile eneo,nikajawa na aibu kutwa nzima

Ilaaniwe K vant na ukoo wake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mtu nipo nae karibu hapa ninemsikia anataka kuanzisha bendi anatafuta wacheza shoo nataka nimuoneshe uzi wako ila nasitasita
 
Huyo ananifaa kabisa kuwa rafiki yangu. Huyo ni yeye kabisa na anajikubali, anajiamini na ni mtu mwenye amani sana na asiye na vinyongo wala hasira hasira hata ukimuudhi hana hasira za kutisha huyo. Hakika unarafiki mzuri mno.

Huyo Yuko vizuri na ninamoongeza, mwambie namsalimia na asije acha kupenda mziki na kuucheza. Mziki ni Maisha
 
Back
Top Bottom