HAKIKA....Hakuna atakayekupenda kama wewe, hakuna atakayekuheshimu kama wewe, hakuna atakaye kutunzia siri zako kama wewe, hakuna atakayekuthamini kama wewe, hakuna atakayefurahia mafanikio yako kama wewe, hakuna atakayekuhurumia Kama wewe
Nawe pia MkuuNiwatakie siku njema
Kweli kabisaOngeza volum kidogo...irudiwe irudiweee
Ukiweza kujipenda, kujijali na kujiheshim wewe mwenyewe, ni rahisi kuwapenda wengine pia.
Hauwezi kutoa kitu usichokua nacho
AminHaka ka"thread" kanafaa kuombea mkopo! Tufanye mpango kawe laminated
Ujumbe mzuri sanaHakuna atakayekupenda kama wewe, hakuna atakayekuheshimu kama wewe, hakuna atakaye kutunzia siri zako kama wewe, hakuna atakayekuthamini kama wewe, hakuna atakayefurahia mafanikio yako kama wewe, hakuna atakayekuhurumia Kama wewe.
Jifunze kujifurahia, kujipenda, kujisahihisha unapokosea, jifunze ku-enjoy company yako mwenyewe, Jifunze kumtafuta Mungu mwenyewe kwa bidii bila kulazimishwa maana yeye ni uzima na afya mifupani mwako. Jifunze kujiwekea mipaka itakayokufanya uheshimike, usiongee kila kitu( kuwa na mipaka kwenye kinywa chako)
Shibisha akili yako na vitabu vinavyojenga, kula chakula chenye afya, jitengenezee mazingira rafiki hasa kwenye nafsi yako, jisemee mambo mazuri, jishughulishe ili usiwe tegemezi.
Mara moja moja ukipata nafasi jipe likizo. Ukianguka amka, jikung'ute mavumbi, na songa mbele.
Ukihisi kuumizwa na kusalitiwa kwa namna yoyote ile; lia kidogo, futa machozi kisha songa mbele.
Usipoteze muda wako kukaa katika maumivu kwani siku zako za kuishi zimehesabiwa.
Usikubali maneno mabaya ya walimwengu yajenge kiota kwenye kichwa chako
Usikubali mtu akuumize bila ruhusa yako.Jifunze kuondokana mazingira au makundi unapoona yanakuondolea amani na kudhoofisha afya ya nafsi yako.
Jifunze kuridhika na ulichonacho huku ukipambana kuwa bora kuliko jana.
Usipende kujilinganisha na wengine hasa kwenye mafanikio labda ukiwa na lengo la kujifunza tu ili na wewe uongeze bidii na juhudi za kufanikiwa.
Mwisho kabla ya kujenga urafiki na wanadamu, jenga urafiki wa karibu na Mungu wako anayejua mwanzo na mwisho wa maisha yako.
Otherwise FURAHIA UHAI ULIOPEWA NA MUNGU NA UTENDEE HAKI UZIMA WAKO
Neema ya Mungu ikuatamie leo!
Niwatakie siku njema.
Sent using Jamii Forums mobile app
AmenMarafiki ni wanafiki kuliko shetani.I have learnt it in hard way.
Niko kwenye uwepo wa bwana@wa stendi nini wewe umeandikika mkuu???
Chukua tuu kuwa amaniNaomba ridhaa yako mkuu, ikikupendeza nichapishe huu ujumbe kisha nibandike chumbani kwa watoto wangu…. natanguliza shukrani.
hata hapo uwanjani pako jenga tu MerciNawe pia Mkuu
Tukujengee Mnara stendi ipi?
Itapendesa pale makao makuuNawe pia Mkuu
Tukujengee Mnara stendi ipi?