Rada ya JNIA yadaiwa kuzeeka, TCAA kununua nyingine

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,261
ebec85bd60d42c30ef533e380dffa4ba.jpg

Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya usafiri wa anga Tanzania (TCAA) Hamza Johari amesema rada iliyofungwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Junius Nyerere imezeeka.

Rada hiyo ilinunuliwa kwa mabilioni ya shilingi kutoka kampuni ya vifaa ulinzi ya BAE Systems ya uingereza na kuzua mtafaruku kwa madai ilikuwa kuukuu.

Akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es salaam jana Johari alisema rada hiyo ilinunuliwa mwaka 2002 na uhai wake ulikuwa kati ya miaka 10 hadi 12 hivyo haina uwezo tena wa kufanya kazi.

Kutokana na hali hiyo mamlaka itanunua rada nne ambazo zitafungwa katika mikoa ya Dar es salaam, kilimanjaro, Mwanza na Mbeya.

Kwenye mawasiliano hatuna tatizo kubwa ila rada iliyopo imezeeka na imepitwa na muda, imechokachoka hivyo tukifunga rada hizo anga yetu itaonekana vizuri tofauti na ilivyo sasa.

Chanzo.. Gazeti Jambo Leo.
 
Matatizo Mengi katika nchi yalitokana na awamu ya tatu ya BWM.
1. Ubinafsishaji wa mashirika ya umma.
hili lilikuwa kosa namba moja ambalo ndio
lilianzisha ufisadi mkubwa unaolitia taifa
hasara.
2. Kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari,
kutoruhusu uwazi kwenye utendaji
na utemi kwenye mambo ya msingi.
3. Ushemeji kwenye mali za umma.

Leo ukiangalia kila skendo iliyoibuka awamu ya nne ya JK utaona mwanzo wake ni awamu ya tatu na mzizi uliwekwa awamu ya tatu, makosa makubwa yaliyofanywa kwenye utawala wa awamu ya tatu ya BWM yameligharimu taifa kuanzia awamu ya nne, tano mpaka awamu ya sita yatatugharimu tusipo kuwa serious.

Siku unafiki utakapoachwa na ukweli ukasemwa kwenye taifa hili kwa maslahi ya tanzania na watanzania wote basi ni hapo taifa la tanzania litakapokuwa taifa lililoendelea..
 
Huyu mkurugenzi vipi rada izeeke halafu mawasiliano kusiwe na tatizo .. inawezekana vp
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom