Hivi R, L na H, ni Ugonjwa wa Taifa?

Yako makosa mengi sana, matumizi ya maneno " yeyote na yoyote " bado nichangamoto. Wekeni kanuni ya matumizi R na L hapa twende pamoja. Au nikukariri tu hakuna kanuni?
Sidhani kama kuna kanuni.Ngoja waje wajuvi tuskie.
 
Hao watu wasiojua kutofautisha kati ya "R' na " L' mpaka kwenye kuandika , vipi kwa maneno ya kiingereza sasa maana kuna maneno ukichanganya unaharibu maana
Road= load
Play= play
au huwa kiingereza hawajui
 
Tatizo lingine kubwa ni hili kama lako. Wengi hawajui wapi h au a inatumika. Mfano wewe ulitakiwa kuandika waandishi. Au mwingine hajui tofauti ya HANA na ANA.
Hawa wa H ndo wanakera zaidi bora hata R na L unaeza sema mbwembwe
 
Turudi kweye mada, nadhani tunaongea uandishi wa hivi:

Screenshot_20190909-110301_Adobe Acrobat.jpg
 
Makabila pia yanachangia,mfano wanyamwezi wanatumia sana L kwenye R, utasikia mtu anasema Gali badala ya Gari au Habali badala ya Habari.
 
Huu ni ugonjwa wa taifa, ni 'haibu' sana miandiko mibovu kweli mpaka watu maarufu wenye nyadhifa kubwa tu serikalini ama mashirika binafsi hawajui kutofautisha r na l, a na ha, inafikia hatua msomaji unaona hata aibu kwa niaba ya mwandishi
aibu umesema haibu
 
Lazima tufike sehemu sasa tukubaliane na hali, kanda ya ziwa, mbeya kote, kanda ya kati na sehemu mbalimbali hizi herufi zimeshaashindikana. Tukubali tu kama vile mjerumani hawezi kusema roho anasema hoho au mtu wa india kusema wewe hawezi hata umshikie bunduki atasema veve. Au kama kiingereza cha kimarekani kilivyo tofauti kimatamshi na kiingereza cha uingereza. Kuna sehemu mpaka bbadhi ya majina yameathirika KAROLI...KALOLI,nk
Makabila yote ya kanda ya nyanda za juu kusini hayana herufi 'R' kwenye misamiati yao. Kwa mfano wanyakyusa hawana herufi 'V' na 'R' badala yake sehemu yenye v kuna 'f' na r kuna 'l'. Kwa sasa V wanaweza kuitamka vizuri ila R imeshindikana kabisa.

Jambo linalonishangaza siku zote ni ilikuaje Mwanza kukawa na eneo linaloitwa Usagara wakati watu wa huko hawana herufi 'R'?
 
Wakurya wakisema tumefiwa utacheka au uji mtamu sana
Wazenji huwa wanasema 'tumefiriwa'. Sasa sijui upande upi upo sahihi kati ya sisi wabara tunaosema TUMEFIWA na wazenji wanaosema TUMEFIRIWA. Wanakiswahili nisaidieni hapo
 
Naamini wana JF wote mpo sawa. JF imepata bahati kuwa na waandishi au wadadavuaji wazuri sana.

Lkn wapo ambao wanasumbuliwa na Maneno 'R' na 'L'. Baadhi hawajui R watumie wapi na L waweke wapi. Kuna mwana JF kaandika lais JPM badala ya rais JPM.

Mwingine kaandika jambo lahisi...badala ya jambo rahisi.Mwingine kaandika mahali 'namshukulu Mungu,' badala ya 'namshukuru Mungu'.

Wapo pia wanaotatizwa na neno 'hawezi kufika' wakiandika 'awezi kufika'.

Nia yangu ya kuandika uzi huu ni kwamba, tusome vizuri uzi za wadadavuaji wa JF ambao tunawajua wako vizuri kwenye kiswahili maana Elimu haina mwisho.
Huu uzi unamhusu Faiza Foxy mwenyewe.

Hapa nimejaribu kufuatilia wengi waliopata elimu zao za msingi miaka ya 90 kuendelea, wengi wanao huo 'ugonjwa', lakini sielewi kisababishi.

Mtu kama aliungishwa elimu ya msingi, hujivuta hivyohivyo hadi chuo kikuu na akikuandikia mada unabakia kubishi juu ya elimu yake!

Nimesemea elimu ya msingi zaidi ndiyo inawatia ulemavu wa maisha wasipofundwa kuanzia hapo, kwa sababu wengi sana wanarekebishwa humu juu ya matumizi sahihi ya silabi, lakini hawaelimiki ama hawajifunzi chochote.

Ndiyo maana Faiza Foxy huwatandika kwa neno lake maarufu ... 'hivi shuleni ulienda kusomea ujinga?'...
 
Zinawasumbua sana sana wanachama wa CCM na mada zao!

Na pia wengi wasiopenda wenzao waongee Kiingereza!

Sisi Watanzania hadi Kiswahili ni shida,sijui tutaweza nini dunia hii!

Shame on us!
Tunaweza kupinga na kubeza kila kitu, na kutukana mitandaoni kutwa kuchwa bila kusahau vigodoro
 
Back
Top Bottom