Kiranja Mkuu
JF-Expert Member
- Feb 18, 2010
- 4,059
- 4,053
Jana nimeibiwa laptop, power window, head rest, redio na mkoba uliokuwa na makabrasha na nyaraka mbalimbali nilipokuwa Mlimani City mida ya usiku. Walinzi wa Mlimani City wanasema kuwa wao hawahusiki na ulinzi wa magari. Basi kwenye kudadisi kwangu mlinzi mmoja akaniambia wanaovunja vioo na kuiba vitu kwenye magari hapo Mlimani City ni kundi la Q Chief.
Nikaenda kutoa taarifa kituo cha Polisi Mwenge ambako nilipewa Rb. Polisi nao wakaniambia kuwa hilo kundi ni la Q Chief.
Polisi wakanielekeza niende mitaa ya gerezani huko ntaweza kupata vifaa vya gari yangu.
Sasa natokea gerezani, nimepata vitu vyangu na kuhusu laptop wameniambia niende Azam kuna bwana anaitwa Salehe nimuone.
Cha kushangaza ni hiki, Polisi wanajua kuwa Q Chief ni mwizi na anamtandao wake, kwa nini hawamkamati na kumfungulia mashtaka?
Kweli jeshi letu la Polisi linanuka rushwa.
Nikaenda kutoa taarifa kituo cha Polisi Mwenge ambako nilipewa Rb. Polisi nao wakaniambia kuwa hilo kundi ni la Q Chief.
Polisi wakanielekeza niende mitaa ya gerezani huko ntaweza kupata vifaa vya gari yangu.
Sasa natokea gerezani, nimepata vitu vyangu na kuhusu laptop wameniambia niende Azam kuna bwana anaitwa Salehe nimuone.
Cha kushangaza ni hiki, Polisi wanajua kuwa Q Chief ni mwizi na anamtandao wake, kwa nini hawamkamati na kumfungulia mashtaka?
Kweli jeshi letu la Polisi linanuka rushwa.