Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,010
- 9,875
JESHI la Polisi mkoani Pwani linamshikilia Chacha Machangu (27) mkazi wa Kibindu kata ya Kibindu Tarafa ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, kwa tuhuma ya kumuua mke wake kwa kumkatakata kwa panga kisha kumfukia kwenye shimo.
Aidha linawashikilia ndugu zake wawili kwa kushiriki tukio hilo la kumuua mke ambapo baada ya mauaji hayo walichimba shimo na kuufukia mwili wake.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha jana, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Wankyo Nyigesa alisema lilitokea Machi 10 saa 8 mchana Kibindu.
Nyigesa alisema baada ya mtuhumiwa kumfumania mkewe alimshambulia kwa kumkata sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia majeraha yaliyosababisha kifo usiku wa tukio hilo.
“Baada ya kumuua mtuhumiwa akishirikiana na ndugu zake, Emmanuel Machangu (19) na Hamis Machangu (22) wote wakazi wa Kibindu, walichimba shimo kwenye shamba la mahindi na kumfukia marehemu,” alisema Nyigesa.
Alisema walipata taarifa na kufuatilia na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wote watatu Machi 19 na kwa ridhaa yao wenyewe walionesha shimo lilipo.
“Ilibidi Polisi wafukue na kuukuta mwili wa ambapo ulifanyiwa uchunguzi na daktari na kufanyiwa maziko na ndugu zake kwa heshima zote tofauti na walivyofanya watuhumiwa kuuzika bila ya taratibu,” alisema Nyigesa.
Chanzo: HabariLeo
Aidha linawashikilia ndugu zake wawili kwa kushiriki tukio hilo la kumuua mke ambapo baada ya mauaji hayo walichimba shimo na kuufukia mwili wake.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha jana, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Wankyo Nyigesa alisema lilitokea Machi 10 saa 8 mchana Kibindu.
Nyigesa alisema baada ya mtuhumiwa kumfumania mkewe alimshambulia kwa kumkata sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia majeraha yaliyosababisha kifo usiku wa tukio hilo.
“Baada ya kumuua mtuhumiwa akishirikiana na ndugu zake, Emmanuel Machangu (19) na Hamis Machangu (22) wote wakazi wa Kibindu, walichimba shimo kwenye shamba la mahindi na kumfukia marehemu,” alisema Nyigesa.
Alisema walipata taarifa na kufuatilia na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wote watatu Machi 19 na kwa ridhaa yao wenyewe walionesha shimo lilipo.
“Ilibidi Polisi wafukue na kuukuta mwili wa ambapo ulifanyiwa uchunguzi na daktari na kufanyiwa maziko na ndugu zake kwa heshima zote tofauti na walivyofanya watuhumiwa kuuzika bila ya taratibu,” alisema Nyigesa.
Chanzo: HabariLeo