muonamambo
JF-Expert Member
- Sep 3, 2010
- 875
- 545
Lile Sakata la Kaimu DED Rufiji aliyewekwa ndani kwa kudaiwa kuwa amemdanganya mkuu wa nchi leo limechukua sura mpya baada ya TEMESA kukiri kuwa Gari lilikuwa bovu na kuwa wameshalitengeneza. Nisiwachoshe karibu msikie wenyewe.
MAAGIZO YA MH RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI YAANZA KUTEKELEZWA PWANI
==========
Mtakumbuka kwamba tarehe 30/07/2020 tulikuwa na ziara ya Mh. Rais alipita katika mkoa wa Pwani na alipita katika wilaya zetu tatu kwa maana ya Mkuranga, Rufiji na Kibiti. Katika wilaya hizo aliongea na wananchi na kutoa maelekezo mbalimbali.
Alipokuwa wilaya ya Rufiji alitengua uteuzi wa DC. Njuayo na Kumteua Ruteni Kanali Patrick Sawala ambae sisi kama mkoa tulimuapisha tarehe 31/ 07/ 2020.
GARI LA KUBEBA WAGONJWA
Na akiwa pale Rufiji kulikuwa na changamoto ya gari la wagonjwa "Ambulance" taarifa ambazo zilitolewa na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Rufiji ni kuwa gari lile la wagonjwa lilikuwa bovu, na Rais akatoa maelekezo kuwa ndani ya siku tano gari hilo litarabatiwe na liwe limetengenezwa.
Na leo nafurahi kuwaonesha kwamba maelekezo ya Rais yametekelezwa gari hilo limetengenezwa na TEMESA na nitalikabidhi kwa mganga mkuu wa mkoa na dereva wake yupo hivyo litakwenda Rufiji kuanza kazi.
UJENZI WA CHOO
Na alipokuwa Kibiti alitoa maelekezo kwa almashauri ya wilaya ya Kibiti ukamilishe mara moja ujenzi wa vyoo vya soko la pale Kibiti.
Nafurahi kuwataarifu kuwa kwa taarifa ambazo nimepewa asubuhi hii na wataalam wetu wa regional secretairiete baada ya kuwa wametembelea eneo lenyewe na pia nimeongea na mkuu wa wilaya na mkurugenzi wamesema kuwa matundu tisa na ifikapoJumamosi inayokuja yaani kwamba mabafu mawili na vyoo saba vitakuwa tayari vimekamilika.
MGOGORO WA ARDHI
Alipokuwa pale Mkuranga pamoja na mambo mengine mengi limeibuka sUala la mgogoro wa ardhi yenye takribani ukubwa wa hekari 1750 na akatoa maagizo kwamba Mkuu wa wilaya, mbunge na mkurugenzi wafanyie kazi utatuzi wa mgogoro huo na kwa taarifa nilizozipata leo asubuhi ni kwamba tayari wizara ya imeshawaita wahusika wote wa ardhi ile tayari juzi wameshafanya mazungumzo na katibu mkuu na kamishna wa pale wizara ya ardhi na leo tumepokea taarifa kuwa kesho tarehe nne na tano Waziri wa ardhi atakuwa na ziara wilaya ya Mkuranga pamoja na mabo mengine atakwenda kushughulikia suala la mgogoro wa ardhi hekari 1750 kulingana na maelekezo ya Rais.
Sasa niwaombe sana wananchi wa wilaya ya Mkuranga hasa eneo lile lenye mgogoro wa ardhi maana kwa taarifa ambazo nimepewa na vyombo vyetu vinasema baada ya Rais wananchi walikwenda kuvamia shamba lile na kugawana wakidhani rais amewapa shamba lile, hapana rais hakuwaagiza muende kuvamia shamba lile haikuwa hivyo maelekezo yalikuwa kwa wizara na serikali ya wilaya ya Mkuranga walitolee utatuzi suala hilo, kwa hiyo wananchi walivamia shamba lile maelekezo hayakuwa hivyo.
Kwa hiyo niwaombe sana waganga wakuu wa hospitali magari haya ya wagonjwa kuwa ni muhimu sana tusisubiri wananchi wamlalamikie kiongozi mkuu wa kitaifa wakati sisi tupo, Tuhakikishe magari haya yanakuwa salama na kama gari lina natatizo ni jukumu lenu kulitengeneza. Basi tuyashughulikie sio mpaka Rais aje na hata matatizo mengine ya wananchi sio hadi rais aje atukumbushe kutatua mambo ambayo yapo ndani ya uwezo wetu ni aibu kabisa.
UPDATE
Mh JPM amemsamehe kaimu DED kwa kosa la kusema uongo kuwa gari la wagonjwa “ Ambulance “ kuwa ni mbovu , Ilhali Gari ni zima .
MAAGIZO YA MH RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI YAANZA KUTEKELEZWA PWANI
==========
Mtakumbuka kwamba tarehe 30/07/2020 tulikuwa na ziara ya Mh. Rais alipita katika mkoa wa Pwani na alipita katika wilaya zetu tatu kwa maana ya Mkuranga, Rufiji na Kibiti. Katika wilaya hizo aliongea na wananchi na kutoa maelekezo mbalimbali.
Alipokuwa wilaya ya Rufiji alitengua uteuzi wa DC. Njuayo na Kumteua Ruteni Kanali Patrick Sawala ambae sisi kama mkoa tulimuapisha tarehe 31/ 07/ 2020.
GARI LA KUBEBA WAGONJWA
Na akiwa pale Rufiji kulikuwa na changamoto ya gari la wagonjwa "Ambulance" taarifa ambazo zilitolewa na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Rufiji ni kuwa gari lile la wagonjwa lilikuwa bovu, na Rais akatoa maelekezo kuwa ndani ya siku tano gari hilo litarabatiwe na liwe limetengenezwa.
Na leo nafurahi kuwaonesha kwamba maelekezo ya Rais yametekelezwa gari hilo limetengenezwa na TEMESA na nitalikabidhi kwa mganga mkuu wa mkoa na dereva wake yupo hivyo litakwenda Rufiji kuanza kazi.
UJENZI WA CHOO
Na alipokuwa Kibiti alitoa maelekezo kwa almashauri ya wilaya ya Kibiti ukamilishe mara moja ujenzi wa vyoo vya soko la pale Kibiti.
Nafurahi kuwataarifu kuwa kwa taarifa ambazo nimepewa asubuhi hii na wataalam wetu wa regional secretairiete baada ya kuwa wametembelea eneo lenyewe na pia nimeongea na mkuu wa wilaya na mkurugenzi wamesema kuwa matundu tisa na ifikapoJumamosi inayokuja yaani kwamba mabafu mawili na vyoo saba vitakuwa tayari vimekamilika.
MGOGORO WA ARDHI
Alipokuwa pale Mkuranga pamoja na mambo mengine mengi limeibuka sUala la mgogoro wa ardhi yenye takribani ukubwa wa hekari 1750 na akatoa maagizo kwamba Mkuu wa wilaya, mbunge na mkurugenzi wafanyie kazi utatuzi wa mgogoro huo na kwa taarifa nilizozipata leo asubuhi ni kwamba tayari wizara ya imeshawaita wahusika wote wa ardhi ile tayari juzi wameshafanya mazungumzo na katibu mkuu na kamishna wa pale wizara ya ardhi na leo tumepokea taarifa kuwa kesho tarehe nne na tano Waziri wa ardhi atakuwa na ziara wilaya ya Mkuranga pamoja na mabo mengine atakwenda kushughulikia suala la mgogoro wa ardhi hekari 1750 kulingana na maelekezo ya Rais.
Sasa niwaombe sana wananchi wa wilaya ya Mkuranga hasa eneo lile lenye mgogoro wa ardhi maana kwa taarifa ambazo nimepewa na vyombo vyetu vinasema baada ya Rais wananchi walikwenda kuvamia shamba lile na kugawana wakidhani rais amewapa shamba lile, hapana rais hakuwaagiza muende kuvamia shamba lile haikuwa hivyo maelekezo yalikuwa kwa wizara na serikali ya wilaya ya Mkuranga walitolee utatuzi suala hilo, kwa hiyo wananchi walivamia shamba lile maelekezo hayakuwa hivyo.
Kwa hiyo niwaombe sana waganga wakuu wa hospitali magari haya ya wagonjwa kuwa ni muhimu sana tusisubiri wananchi wamlalamikie kiongozi mkuu wa kitaifa wakati sisi tupo, Tuhakikishe magari haya yanakuwa salama na kama gari lina natatizo ni jukumu lenu kulitengeneza. Basi tuyashughulikie sio mpaka Rais aje na hata matatizo mengine ya wananchi sio hadi rais aje atukumbushe kutatua mambo ambayo yapo ndani ya uwezo wetu ni aibu kabisa.
UPDATE
Mh JPM amemsamehe kaimu DED kwa kosa la kusema uongo kuwa gari la wagonjwa “ Ambulance “ kuwa ni mbovu , Ilhali Gari ni zima .