Pwani: Askari Polisi agoma kusema CCM oyee. Afukuzwa kwenye mkutano na kiongozi wa CCM, aambiwa atakiona

Sirro hapo kanyamaza kimyaa kama vile hajaona.Ingekuwa ni mchadema kafanya hivyo kelele kila pande angepaza kukemea
 
Huyo askari anatakiwa apandishwe cheo.
Majeshi ndiyo nguzo muhimu ya taifa na askari wote wanatakiwa wafanye kazi kwa weledi na uzalendo.
Walinde katiba na pale hali ya uvunjifu wa amani, uonevu kwa raia unapozidi kutokana na sababu za kisiasa, washike madaraka kwa muda.
Hawatakiwi kabisa kuungana na makundi ya kisiasa hadharani, hasa wakati wa amani.
Kwani alikuwa yupo kazini?
 
Habari ambayo ina-trend sana kwenye mitandao ya kijamii kwa hivi sasa zinahusu mkutano wa CCM uliofanyika mkoani Pwani siku chache zillizopita, ambapo mjumbe mmoja wa Halmashauri Kuu ya Taifa, alimtaka askari mmoja, atoe salaam za chama chao za CCM oyee

Kitendo cha askari huyo kukataa kutoa salaam hizo kimeungwa mkono na mamilioni ya watanzania, kwa kuwa inaeleweka wazi kuwa nchi yetu ipo kwenye mfumo wa vyama vingi na hivyo majeshi yote nchini yanatakiwa yawe "impartial" bila kushabikia chama chochote cha kisiasa

Kwa hiyo ni wazi kuwa Kitendo cha mjumbe huyo wa NEC ni cha uvunjaji wa wazi kabisa wa Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 3(1) ambayo inatamka wazi kuwa nchi yetu ni ya kidemokrasia inayofuata mfumo wa vyama Vingi, ambapo majeshi yote nchini hayapaswi kushabikia chama chochote cha siasa

Kwa kuwa Kitendo kilichofanywa na mjumbe huyo wa NEC ni cha uvunjaji wa wazi wa Katiba yetu ya chama, kwa hiyo tunamsubiri Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Bashiru Ally atoe kauli ya kulaani Kitendo hicho cha mjumbe wake wa NEC kutoa kauli hiyo hadharani ambayo siyo tu inaweza kuleta machafuko nchini, bali pia ni kinyume kabisa cha Katiba yetu ya nchi

Kitendo cha kukaa kimya kwa Dkt Bashiru Ally, watanzania tutajua kuwa kumbe kauli hiyo ya mjumbe wa NEC ndiyo msimamo wa chama chao cha CCM!
 
Hivyo ndiyo serikali yetuinavyoendeshwa. Tulishasema mara nyingi tu kuwa serikali inalazimisha askari kuwaunga mkono kwa lazima.
Nampongeza sana huyu askari kwa msimamo wake, hata kama utamgharimu kazi yake na maisha pia.

Matatizo ya watu waliowekwa madarakani kwa kunyooshewa vidole badala ya taaluma ndiyo hayo.

Na ili ujue katumwa, hutasikia kiongozi yeyote wa serikali au chama akilaanihicho kitendo alichofanyiwa huyo askari.

Natamani siku moja askari wagome tuone kitakacho tokea
 
Nawaza kama ingekuwa kwenye halmashauri inayoongozwa na CDM halafu CDM wamfanyie huyo askari hivyo,nadhani sasa hivi wangekuwa central!
Absolutely true

Hatutaki hizo "double standard" zinazoendelea nchini, kwa kuwa zikiaachwa ziendelee, zinaweza leta machafuko makubwa nchini
 
Ccm ina watu wa ovyo saana katika nchii hii ni katika ile takwimu ya kwenye watu wa 4 mmoja n kichaa basi lumumba pale kwenye 4 basi 3 ni gongowazi.
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
Askari anakuwa kazini 24/7 hata kama yuko baa anakula kilaji lakini pale alikuwa ameenda kikazi na ndiyo maana akatakiwa kuongea kama askari na si kama raia tu wa kuchangia mada, goodness kaonyesha msimamo stahiki wa kiaskari.
Huwa nachukia polisi wa kibongo kwa kupenda kubambikia watu kesi ili wawageuze dili na kuwakamua pesa lakini kwenye hili huyu koplo kongole nyingi kwake.
Kwani alikuwa yupo kazini?
 
Aiseee ukisikia top down effect ndiyo hii.

Kinachofanyika juu kinashuka na kuigwa chini, WE ARE DOOMED, it is just a matter of time TUNAENDA KUSAMBARATIKA KABISA,

Angalia hii video kwa makini ujionee na usikie mwenyewe,sitashangaa kusikia huyo askari katoweshwa au kachukuliwa hatua kali kwa maelekezo fulani.


View attachment 1181707

Tunaongozwa na washamba
 
Kuulizwa swali la kwa Nini kituo hakifunguliwi masaa 24 nalo Ni swali la Askari yule kujikanyaga? Hadi kusema sihojiwi na chama? Yule Askari alitoka nje ya ulingo wa kazi Yake.Angejibu tu na Wala haikuwa kesi .Askari yule ana uelewa mdogo wa kazi Yake.Alipanic alipoona watu wamevaa nguo za CCM .Swali lile lilikuwa la kawaida kabisa la kikwzi Wala SI la kisiasa kwake.
Kakatishwa baada kukataa kusema CCM oyeeee...., hakuulizwa swali lolote pale so don't prove to us the jerk that you are.
Yaani hata clip iliyo crystal clear unaandika utumbo kujaribu kudanganya kifala namna hiyo?
You're a certified stupid ass.
 
Kwani alikuwa yupo kazini?
Mkuu kwa akili zako ili askari awepo kazini lazima awe amevaa sare...or awe yupo kituoni????...askari yupo kazini muda wote na kikawaida hata wewe hapo mtaani kwenu mnaweza mkawa na mkutano wa mtaa na mnaruhusiwa kumuomba askari yoyote aje kwenye mkutano wenu kama kuna jambo mnahitaji lipate ufafanuzi kutoka kwenye vyombo vya usalama
 
32 Reactions
Reply
Back
Top Bottom