Pwani: Askari Polisi agoma kusema CCM oyee. Afukuzwa kwenye mkutano na kiongozi wa CCM, aambiwa atakiona

Akili zingne za kijinga sana Kwahiyo Ccm kupewa ridhaa ya kuunda serikali ndio wanajiona wao ndio wanalipa mishahara watu?

Yaan wao kuwa wakusanyaji wa kodi kwa niaba ya wananchi ndio wanajiona wanatoa hela mfukoni mwao!

Ni sawa na msimamizi wa ujenzi wa nyumba anauetumwa akawalipe mafundi basi anajiona yeye ndio boss na mwenue nyumba
 
Kama anajua salama siyo kitu chochote ni kitu cha kawaida sana kwa nini anamind sasa mpaka kumtimua askari...

Kuna binadamu wana mambo ya ajabu sana... anaelekezwa ukweli ubishi umemjaa tuu..



Cc: mahondaw
 
Hakuna popote kwenye clip panakoonekana au kusikika akikataa kujibu swali. Wamemkatisha kwa kumlazimisha asalimie kwanza kichama, na akawajibu kiungwana kuwa haruhusiwi. Walipomtajia reference za IGP na RPC wa Arusha akawajibu kuwa hao ni viongozi wanaruhusiwa, yeye ni askari mdogo haruhusiwi.
hapo kwenye viongozi pia alijikanyaga.

askari yeyote unayemjua kwa mujibu wa katiba,ni marufuku kujihusisha na itikadi zozote za chama chochote nchini.rejea koplo wa jeshi(jwtz)aliyeonekana akiwa amenyanyua vidole viwili juu na mh lema arusha 2010,nini kilitokea.
 
Chuki inayo jengwa hapo, aki matokeo yake yataonekana siku moja.

Time will tell.
Magufuri siku moja tutakuchoka hata sisi tunaokupenda ukiendelea kufimbia macho haya mambo.

Naumia nafsi,akili, moyo na Mwili.
 
Huyo askari anatakiwa apandishwe cheo.
Majeshi ndiyo nguzo muhimu ya taifa na askari wote wanatakiwa wafanye kazi kwa weledi na uzalendo.
Walinde katiba na pale hali ya uvunjifu wa amani, uonevu kwa raia unapozidi kutokana na sababu za kisiasa, washike madaraka kwa muda.
Hawatakiwi kabisa kuungana na makundi ya kisiasa hadharani, hasa wakati wa amani.
 
Aiseee ukisikia top down effect ndiyo hii.

Kinachofanyika juu kinashuka na kuigwa chini, WE ARE DOOMED, it is just a matter of time TUNAENDA KUSAMBARATIKA KABISA,

Angalia hii video kwa makini ujionee na usikie mwenyewe,sitashangaa kusikia huyo askari katoweshwa au kachukuliwa hatua kali kwa maelekezo fulani.


View attachment 1181707

CCM sasa wanavuka mipaka Kitengo hicho cha kumshurutisha Asikari Polisi atoe salam ya chama cha CCM ni udhalilishaji wa Idara ya Polisi kwani kikatiba na Sheria za Nchi Polisi hapaswi kuegemea upande wowote haruhusiwi kuwa mwanachama wa chama chochote.
 
Akili zingne za kijinga sana Kwahiyo Ccm kupewa ridhaa ya kuunda serikali ndio wanajiona wao ndio wanalipa mishahara watu?

Yaan wao kuwa wakusanyaji wa kodi kwa niaba ya wananchi ndio wanajiona wanatoa hela mfukoni mwao!

Ni sawa na msimamizi wa ujenzi wa nyumba anauetumwa akawalipe mafundi basi anajiona yeye ndio boss na mwenue nyumba
Meya wa jiji la Dsm ni chadema walipa kodi ni wananchi wote pasipo itikadi yeyote iweje CCM wajione pesa za watanzania wote ni pesa zao binafsi?
 
Makada wa CCM kwa siku za karibuni wamezidisha udhalilishaji mkubwa kwa watumishi wa umma inashangaza hata katibu mkuu wa CCM kashindwa kulikemea hilo.
 
Huyo askari anatakiwa apandishwe cheo.
Majeshi ndiyo nguzo muhimu ya taifa na askari wote wanatakiwa wafanye kazi kwa weledi na uzalendo.
Walinde katiba na pale hali ya uvunjifu wa amani, uonevu kwa raia unapozidi kutokana na sababu za kisiasa, washike madaraka kwa muda.
Hawatakiwi kabisa kuungana na makundi ya kisiasa hadharani, hasa wakati wa amani.
Naungana na hoja yako kwa 100%
 
Hapa America na Ulaya pia ni marufuku kwa Polisi kujihusisha na Siasa ikibainika Polisi anafanya vitendo vya kukipendelea chama fulani anashitakiwa kwa mujibu wa Sheria hawapendi kwenda kinyume na katiba kama Tanzania ya sasa.
 
Aiseee ukisikia top down effect ndiyo hii.

Kinachofanyika juu kinashuka na kuigwa chini, WE ARE DOOMED, it is just a matter of time TUNAENDA KUSAMBARATIKA KABISA,

Angalia hii video kwa makini ujionee na usikie mwenyewe,sitashangaa kusikia huyo askari katoweshwa au kachukuliwa hatua kali kwa maelekezo fulani.


View attachment 1181707
Poor, kwNza huyu kiongoz ni wa kuchukuliwa hatua. Askari unamwambia atoe salama ya chams ?? Umetudhalilisha sana, fuatilia viongoz wote waliowahi pita Kama huu upuuzi wake upo, tumsamehe bure tuendelee na ujenz wa Taifa la uchum wa kat Na viwanda
 
IGP mwenyewe anashangalia CCM kindakindaki Acha IGP kuna CDF pale wote wale wale tu mamaee... Siku hizi wanatinga kwenge mikutano na Magwanda kabisa...!! Aibu kubwa sana hii Jeshi kuingia kwenye Siasa ndo maana Mwamnyange alikuwa hataki mazoea ya kipuuzi kama haya...
 
CCM:Kituo cha polisi hakifunguliwi masaa 24,............,leta maneno!

Askari:Kwakweli hilo suala....(anakatishwa)

CCM:Salimia kichama bhana

Askari:(Anajieleza kwanini hawezi kusalimia kichama:

CCM:Kama IGP mwenyewe anasalimia,RPC anasalimia kichama,wewe nani bhana?

Askari:Mimi ni mtu mdogo sana kwa cheo,sipaswi....

CCM:Mshahara unalipwa na nani?

Askari:Serikali

CCM:................ondoka hapa,naombeni jina lake na cheo chake(Sijui anataka ampigie Magu ili aongezwe cheo ili kwa siku za baadae aseme CCM oyee)


Unajua Mr Saidi hakupewa nafasi ya kujibu swali lolote, pia akasema yeye ni mtu mdogo sana, inabidi afuate sheria, maadili, ya kazi yake.

Labda ana familia, labda watoto, baba na mama, babu na bibi kama mimi na wewe. Wote wataona hii clips.

Muhimu kuwaheshimu watu wa chini yako, juu yako. Huyu ni binadamu kama wewe. Polisi ni walinzi wako. Walinzi wetu sisi wote. Heshima kwao ni muhimu, pamoja na mapungufu yao.
 
Back
Top Bottom