Purukushani Mkutano Wa CCM Iringa

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Mkutano wa viongozi wa CCM kutangaza uzuri wa bajeti ulienda vizuri kwenye viwanja vya Mwembetogwa kuanzia saa kumi jioni hadi ilipotimu saa kumi na mbili jioni pale kada wa zamani wa Chadema aliyehamia CCM Bwana Shaibu Akwilombe alipotoa tuhuma kuwa Chadema inaondeshwa kindugu huku akitaja orodha ya majina katika kupeana vyeo kindugu. Ndipo hapo kada wa Chadema aliyesimama mbali mkutanoni alipotamka kwa sauti; " Mbona humtaji mtoto wa Mwinyi, Husein Mwinyi! Mbona humtaji mtoto wa Karume Zanzibar!". Ndipo hapo purukushani zikaanza mara ile makada wa CCM walipomwendea kada wa Chadema kutaka kumshughulikia kwa kuvuruga mkutano wao. Angalia picha za tukio hilo katika; http://mjengwa.blogspot.com
 
kumbe hawa watu wanatumia mabavu kuvuta washabiki? ngoja kwenye kura kama watatumia mabavu
 
Akwilpmbe ana njaa sana na kasi ya kuwa na wanawake 2 inambana sasa anaanza kutokwa ushuzi mdomoni. Alipokuwa huko mbona hakusema na aliptoka huko mbona hakuyasema haya ? Hivi hii ndiyo bajeti wanayo ielezea huko ? Wala si Mwinyi pekee kuna Makongoro Nyerere, JK mwenyewe mke na watoto na ndugu zake .Jamani Akwilombe kweli anachanganyikiwa.
 
akwilombe hana lolote alinunuliwa na ccm [makamba] kwa bei ya tsh 7,000,000 /= mwenzake hizza tambwe alinunuliwa kwa tsh 30,000,000/=..na lipumba naye kashanunuliwa kwa kuwa recomended ajira newyork....maalim kama mnavyojua kashapatiwa mafao yake na pesa kedekede kilele zimekwisha.............

kimsingi inabidi tuwaunge mkono mkono CHADEMA Kwa mkakati wao wa kuwajenga vijana ili kujenga safu mpya wa wapinzani vijana walioandaliwa....
 
kweli Philemon ila kasi yao isije ikawa nguvu ya soda maana tumeshaona wengi wakikaribia kufanikiwa wanafarakana hasa Mrema sina imani naye kabisa
 
habari za uhakika ni kuwa mrema ameshakubali kugombea ubunge ..ila kinachotatiza wapinzani ni kuchelewa kupitishwa kwa sheria ya coalition of parties[yaani uwezekano wa vyama kuungana kwenye chama kimoja as coorprate member na bado vikabaki na identity zao]..inaelekea serikali bado haitaki kupitisha hiyo sheria...ni tatizo sana kuwaambia viongozi wavunje vyama vyao..
 
kimsingi inabidi tuwaunge mkono mkono CHADEMA Kwa mkakati wao wa kuwajenga vijana ili kujenga safu mpya wa wapinzani vijana walioandaliwa....

Mkuu ni kweli, lakini it is about time sasa tukaaanza kuwasikia na wengine huko Chadema, badala ya Freeman, Zitto, na Dr. Slaaa, na wengine wapewe nafasi nao tuwasikie, tatizo la kutegemea viongozi wachache ni kwamba wakinunuliwa kama Seif, basi chama kizima kinakufa kama CUF ilivyo sasa hakuna muelekeo!

Na ikiwezekana kufanyike mpango wa kuviunganisha vyama vyote vya upinzani kuwa chama kimoja!
 
safari ndio anayeingia CUF..lakini hataweza ..kuna hisia kuwa CUF hawana shida na bara..na huwa wanaweka mwenyekiti toka bara kama fomalities za kufulfill requirements za vyama..analieni walivyowatumia kama wapagazi james mapalala[tabora],masubi mageni [tabora],ibrahim lipumba[tabora]...CUF nguvu kubwa wanawekeza visiwani..hata budget zao za uchaguzi asilimia 80% huelekezwa visiwani....wanafanya kosa sana kimkakati kwa kuwa ili wao wafanikiwe visiwani wanahitaji kuungwa mkono na watu wengi wa bara...

kimya cha CUF hata katika hili suala la bot na buzwagi hawaoneshi sana kuguswa ..amabaye kidogo anaonekana mstari wa mbele kwenye umoja wa vyama ni wailfred rwakatare..amabye definately anaguswa na pia ana malengo ya kisiasa ya kurudisha kiti chake cha ubunge bukoba mjini amabapo kagasheki alimshinda kwa mbinu...
 
hivi lipumba kanunuliwa na ccm? acheni speculation hizo

mzee wa pwani ...sio speculations..ndio hivyo tena CUF watafute mwenyekiti na katibu...aliyesema LIPUMBA NDIO MCHUMI GENIOUS kuliko wote nani??? ile post hangeweza kupewa bila KUPENDEKEZWA huko UN[?]..NA serikali ya jamhuri ya muungano pia impendekeze ,[vetted]..sasa unafikiri waliompeleka huko wanampenda sana au?? na kama angekuwa hajachoka na mambo ya CUF alikuwa na haja gani ya kukubali kuhamia huko..acha kukubali kazi maana hata kabla alikuwa anafanya consultancy za hadi miezi mitatu mfulululizo bila kuadhiri chama ..sasa hii ni permanent...serikali inao watu wengi tu ambao ingewweza kuwapendekeza kwa hiyo kazi....

pili nilishawahi kupost hapa kuwa hii kitu inaitwa muafaka ilikuwa na danganya toto..na rushwa ya waziwazi kwa viongozi wa cuf..kuwa keep busy kila siku hadi miaka mitano inaiosha wanaenda uchaguzi wanashindwa life goes on ..wana uhakika baada ya uchaguzi vikao vya muafaka vinaendelea ..ipo siku niliwakuta wajumbe wa baraza kuu walio kwenye vikao kila mmoja akijisifu namna alivyonunua gari mpya dubai kwa posho za vikao visivyoisha....

pia jiulizeni kwa nini lipumba apewwe kazi hasa baada ya wanachama ku revolt na kumtaka awape majibu ya vikao visivyoisha vya muafaka ..tangu hapo kaingia mitini na KAZI JUU..

i hope maalim will also go ..and there comes juma duni haji and hamad rashid....
 
mzee wa pwani ...sio speculations..ndio hivyo tena CUF watafute mwenyekiti na katibu...aliyesema LIPUMBA NDIO MCHUMI GENIOUS kuliko wote nani??? ile post hangeweza kupewa bila KUPENDEKEZWA huko UN[?]..NA serikali ya jamhuri ya muungano pia impendekeze ,[vetted]..sasa unafikiri waliompeleka huko wanampenda sana au?? na kama angekuwa hajachoka na mambo ya CUF alikuwa na haja gani ya kukubali kuhamia huko..acha kukubali kazi maana hata kabla alikuwa anafanya consultancy za hadi miezi mitatu mfulululizo bila kuadhiri chama ..sasa hii ni permanent...serikali inao watu wengi tu ambao ingewweza kuwapendekeza kwa hiyo kazi....

pili nilishawahi kupost hapa kuwa hii kitu inaitwa muafaka ilikuwa na danganya toto..na rushwa ya waziwazi kwa viongozi wa cuf..kuwa keep busy kila siku hadi miaka mitano inaiosha wanaenda uchaguzi wanashindwa life goes on ..wana uhakika baada ya uchaguzi vikao vya muafaka vinaendelea ..ipo siku niliwakuta wajumbe wa baraza kuu walio kwenye vikao kila mmoja akijisifu namna alivyonunua gari mpya dubai kwa posho za vikao visivyoisha....

pia jiulizeni kwa nini lipumba apewwe kazi hasa baada ya wanachama ku revolt na kumtaka awape majibu ya vikao visivyoisha vya muafaka ..tangu hapo kaingia mitini na KAZI JUU..

i hope maalim will also go ..and there comes juma duni haji and hamad rashid....


Mkuu heshima mbele, siyajui vizuri ya huko ndani upande wa pili lakini this is strong and powerful, nilijua kuwa Seif amewauza pale tu alipokubali kupewa nyumba ya serikali huko kwao, Dar, na Dodoma, kama waziri kiongozi mstaafu, na walinzi wawili kutoka serikalini, na kusafiri ndege moja na Mangula kwenda UN, kuelezea muafaka ambao ulikuwa haujaisha mpaka leo, sikujua na Lipumba naye amechukua chake mapema, damn!

Yaani siku hizi wote wanamuiga Mkapa, kuchukua chako mapema kabla wananchi hawajashituka!
 
Haya ya Iringa yanachefua. maana hii inaonyesha ccm wamekosa hoja. kutumia hoja ile ele iliyozomewa Mbeya kunaonyesha kwamba ubongo wao hauna maarifa ya kubadili sura mchezo. Inawezekana huo ndiyo upeo wao wa kufikiri. wako limited.

Mzee Makamba alidhani kuwapata Akwilombe na Hizza kalamba Dume, kumbe galasa. badala ya kujenga chama sasa wanabomoa kwa mikono yao wenyewe.
 
akwilombe hana lolote alinunuliwa na ccm [makamba] kwa bei ya tsh 7,000,000 /= mwenzake hizza tambwe alinunuliwa kwa tsh 30,000,000/=..na lipumba naye kashanunuliwa kwa kuwa recomended ajira newyork....maalim kama mnavyojua kashapatiwa mafao yake na pesa kedekede kilele zimekwisha.............

kimsingi inabidi tuwaunge mkono mkono CHADEMA Kwa mkakati wao wa kuwajenga vijana ili kujenga safu mpya wa wapinzani vijana walioandaliwa....

Kwa sasa nikuwaunga mkono wapinzani haswa CHADEMA wakitupeleka pori basi, kwa safu mpya ya vijana waliyo nayo wasiyo nunulika hii ni njia nzuri, hawa wenye tamaa utaona mwisho wao, huko CCM.
 
kwa safu mpya ya vijana waliyo nayo wasiyo nunulika hii ni njia nzuri,

are u sure mkuu?
kwenye dhiki, wewe penyeza rupia.... kila kitu kinakuwa sawa.

just remember
'there is no truth wherever money matters'
 
cha kujiuliza hivi mnadhani leo hii wapinzani wakiingia IKULU/SERIKALINI kutakuwa hamna rushwa ?mie naangalia tu !
 
cha kujiuliza hivi mnadhani leo hii wapinzani wakiingia IKULU/SERIKALINI kutakuwa hamna rushwa ?mie naangalia tu !

Nadhani hoja hapa sio kuingia ikulu, Kada, hata wakiingia wapinzani rushwa itakuwepo na rushwa ipo sehemu yeyote duniani eg Marekani, world bank, Japan etc. Hapa issue ni kuwa kusiwe na monopoly kwenye politics na hii iitasaidia kupunguza rushwa na kuwajibika. Unajua hii monopoly ya CCM imefanya watumishi na viongozi wake wawe na kiburi na kula bila woga? sasa kidogo kama kukiwa na uwiano kwenye siasi hii itapunguzwa na si kumalizwa.

Tumeona Kenya walishinda lakini bado mabadiliko si makubwa sana, Zambia nako wapinzani walishinda lakini bado mambo ni yale yale. Ila wakati kunakuwepo na ushindani nadhani inasaidia kwa kiasi fulani.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom