Mohamed Ismail
JF-Expert Member
- Mar 16, 2014
- 214
- 229
Huwa sijajua hadi leo kati ya tabia na mazoea ni kipi kilimtangulia mwenzake. Kwenye makuzi yangu nilikua katika mazingira ya usomaji kwa kuwa baba yangu ni mpenzi msomaji wa vitabu pamoja na maandiko mbalimbali. Alikuwa ni msomaji wa gazeti la Rai Mwema ambalo lilikuwa likitoka kila alhamisi lakini kutokana na miundombinu ya kipindi kile kufika hadi nyumbani iliweza kufika Ijumaa au Jumamosi.
Ilikuwa likifika Bukoba mjini baba analiagiza watu wa daladala za kuja nyumbani na mimi mara nyingi ndio nilienda kulipokea.
Nikiwa tu shule ya msingi niliweza kusoma mawazo ya waandishi kama wakina Maggid, Jenerali Ulimwengu pamoja na Padri Privatus Karugendo.
Leo hii asubuhi nimesikitika sana kuona mwandishi gwiji Privatus Karugendo katutoka na hayupo nasi tena. Nilimsoma nikiwa bado kinda hata ukubwani nimemsoma kwenye magazeti ya Raia mwema, Tanzania daima na Mwanahalisi.
Kwetu wapenzi wasomaji huu ni msiba mkubwa na tumepoteza maestro katika taaluma ya uandishi.Alikuwa na uwezo wa kutengeneza sanamu na katika maandishi yake akakuaminisha ni binadamu na mwishowe ukakubaliana naye.
Binafsi mlimwengu mimi nakuombea mapumziko mema ya milele na kwangu utabaki kuwa mwandishi gwiji wa kusimamia kile ulichokiamini kwa kutumia bongo yako na kalamu yako.
Rest in peace Padri P. Karugendo
#mlimwengumimi
Ilikuwa likifika Bukoba mjini baba analiagiza watu wa daladala za kuja nyumbani na mimi mara nyingi ndio nilienda kulipokea.
Nikiwa tu shule ya msingi niliweza kusoma mawazo ya waandishi kama wakina Maggid, Jenerali Ulimwengu pamoja na Padri Privatus Karugendo.
Leo hii asubuhi nimesikitika sana kuona mwandishi gwiji Privatus Karugendo katutoka na hayupo nasi tena. Nilimsoma nikiwa bado kinda hata ukubwani nimemsoma kwenye magazeti ya Raia mwema, Tanzania daima na Mwanahalisi.
Kwetu wapenzi wasomaji huu ni msiba mkubwa na tumepoteza maestro katika taaluma ya uandishi.Alikuwa na uwezo wa kutengeneza sanamu na katika maandishi yake akakuaminisha ni binadamu na mwishowe ukakubaliana naye.
Binafsi mlimwengu mimi nakuombea mapumziko mema ya milele na kwangu utabaki kuwa mwandishi gwiji wa kusimamia kile ulichokiamini kwa kutumia bongo yako na kalamu yako.
Rest in peace Padri P. Karugendo
#mlimwengumimi