Psychoanalysis ya Waomba Msamaha Kwa Rais, Makamba Snr is the Next, Membe Will Never for Pride, Kiburi na Jeuri, Kinana Will Never for Integrity

Quote ''......Kwa vile mimi ni miongoni mwa waandishi wa habari, mara moja moja nipatapo nafasi nitakuwa nawaletea news analysis ya baadhi ya matukio muhimu kwa taifa letu. ...''

Furusa Tz bado nyingi sana.... Mnaonaje mkianzisha chombo / gazeti, kitakacho ratibu shughuli za uchunguzi na kufuatilia matukio yote makubwa ya Kitaifa...
Kwa nini limetokea, nani wahusika, mapendekezo ya nini kifanyike lisitokee tena, nani atatekeleza na kufuatilia utekelezaji wa mapendekezo ya kutojirudia tena?

Chombo hicho kiwe na watalaam kama Wanasheria, waandishi wa habari, wachumi, wahandisi, wapelelezi (utoka vyombo vya dola wastaafu), nk.
 
Mimi nazitazama siasa za bongo km Ni za kusalitiana lkn pia za kuviziana mambo yanavyokuwa magumu . Mr mayalla ulichokisema msamaha ambao una strategic reasons inaweza kuwa sahihi lkn ndan yake pakawa na harufu ya usaliti. Mimi naweza sema makamba Jr na Nape kwa upande wa Rais au Mwenyekiti wa chama inaweza ikawa chambo ya kuwavuta akina Makamba senior, kinana na Membe nao waone it is time for them kwenda kuomba msamaha lkn kwa upqnde wa Ant- Mwenyekiti wa chama ( Kinana, Membe na Makamba senior) inaweza ikawa akina Nape Ni agents wa kwenda kusoma nini kilichopo kwa Mwenyekiti yaan wakatumika Kama spiers ili kupeleka taarifa kwa wazee wale.

Kwa mantiki hiyo Basi Mimi siitazama season hiyo km ndo inaenda kuisha Bali bado Ni mbichi sn. Aliyeombwa msamaha hawez ingia miguu yote kuwakubali akina bwana mdogo wale lkn nao akina beana mdogo hawawez kuamini km wamesamehewa. But all in all ni suala la wakati.
 
Wanabodi

Kati ya udhaifu mkubwa sana wa media zetu Tanzania, sii redio, TV na Magazeti, hatuna competent people wa kufanya news analysis, kazi kubwa media zetu ni kufanya reportage tuu ya matukio, lakini hatuna uchambuzi wa matukio na hatuna wachambuzi.

Kwa vile mimi ni miongoni mwa waandishi wa habari, mara moja moja nipatapo nafasi nitakuwa nawaletea news analysis ya baadhi ya matukio muhimu kwa taifa letu.

Uchambuzi wa leo, nitawachambulia kuhusu mfululizo wa matukio ya rais Magufuli kuombwa msamaha na baadhi ya wanasiasa baada ya voice notes zao ku leak kwenye media.

Waomba ambao tayari wameomba msamaha ni January Makamba, huyu ameomba msamaha for strategic reasons, sio kwa sababu amekosa. Ngeleja kaomba msamaha kwa kujikomba tuu, Nape kaomba msamaha kwa uoga wa kitakacho mkuta. Bado kuna watu watatu wengine ambao voice notes zao zili leak na hawajaomba msamaha, hawa ni Makamba Senior, Benard Membe na Abraham Kinana. Kuna swali watu wanajiuliza who is next kwenda kwa rais Magufuli kuomba msamaha. The next Makamba Snr, huyu ataomba msamaha kwa sababu rais Magufuli kasema ametukanwa, Membe will never kneel down kwa Magufuli kuomba msamaha for Pride, Kiburi na Jeuri, na Kinana pia, will never beg for mercy for Integrity reasons, aombe msamaha kwa kosa gani?.

Nauweka uchambuzi in points format ili iwe rahisi kuulizia any specific point.

Kwa utangulizi, kwa vile humu mitandaoni, kila siku kuna watu ni wageni, naomba nianze na utambulisho wa psychoanalysis ni nini.
Karibu uandamane nami.

1. Psychoanalysis ni Nini, na ya Kazi Gani?
Kuna msemo usemao, information is power, yaani ukiwa na taarifa sahihi, unakuwa na nguvu, hivyo hii psychoanalysis ni somo la kujifunza kwa nini watu wana behave kwa namna fulani kwenye situations fulani. Hivyo ukijua tabia za watu, kwa nini they behave the way they behave, wewe unakuwa na power ya kuwafahamu na sometimes bila wenyewe kujifamu, hivyo kwa kuandika humu kuhusu human behaviors, hii inaweza kuwasaidia kubadilika, and changing for the better kwa kupunguza maneno na kuongeza vitendo. Waalimu wakuu wa hili somo la psychoanalysis, ni wawili, Carl Jung na Sigmund Freud
Kujua zaidi Psychoanalysis tembeleeni

Paskali.
Paskal:-
1. Watu hawawezi kufanya uchambuzi zaidi ya kinachoonekana kwa sababu wataishia kuwa kama hao watu wanaowachambua;
2. Mimi ninaona kama ni mchezo wa kuigiza vile
 
Makamba Jr ilikua hakuna jinsi kwake kuomba msamaha kwa sababu;

1) Yeye alijikuta kwenye lile sakata baada ya watu fulani kupitia njia ya mkato kwa "BABA YAKE MZAZI" kumvuta katika pande yao.

NB madhaifu hua hayakosekani kwa mtu/kiongozi hasa mzazi wake anapokua ROLE MODEL wake, na anapokua chanzo kikuu cha yeye kufika hapo alipo na kuelekea kwenye ndoto zake. Waswahili wanasema "Mtoto kwa baba hakui".

Hata sisi pia, tukiangalia maisha yetu kwa umakini toka utotoni mpaka hapa tulipo, watu kadhaa mara ngapi walishawahi kuwatumia wazazi wetu kutushawishi kufanya jambo fulani katika nyakati tofauti tofauti na tukafanya?

2) Ni kijana mdogo ambae bado ana safari ndefu kisiasa.

Tofauti na mtu kama Abdulrahman Kinana au Makamba Sr, ambao umri umeshawapa mkono, wameshafanya yao mengi sana katika ulingo wa siasa. Sasa hivi hawahitaji kufanya siasa kama ajira. Ni muda wao kupumzika na kulea wajukuu.

Ila kwa Makamba Jr bado umri anao mwingi, tofauti na hao tajwa hapo juu. Ndoto zake ni siasa na bado hajakomaa kisiasa ipasavyo, na kama angefuata PRIDE yake impeleke kunako basi angepotea katika ulingo wa siasa kabisa (Unless angekua BRAVE & BRIGHT enough kucheza karata zake kwa network/support aliokua nayo CIA na upinzani).

3) Hana kinga CCM.

Mzee wake ndio tayari mstaafu, Kinana nae pia mstaafu, Kikwete pia yupo kando (Wangekua active polititions angekua na back up).

CCM ya sasa kuna watu wanajiita "CCM MPYA" ambayo ina watu wake waliokua installed na wenye nguvu na ushawishi mkubwa sana, tena ni vijana wadogo. Na kwa ushawishi waliokua nao hawa vijana wa lumumba wa kisasa basi wangemtoa katika dira ya siasa kwa kufumba macho na kufumbua tu.

4) CV zake kisiasa/serikalini.

CV yake ya kisiasa/serikalini tanzania kwa ufupi si kubwa na ya kutisha kana kwamba REPLACEMENT yake ingekua tabu, au kumpoteza serikalini/CCM ili akaweweseke upinzani au mtaani sio issue kabisa (Contrary to Bernad Membe au Abdurahman Kinana = Ni hatari sana).

Bernad Kamilius Membe, hawezi kuomba msamaha sio kwasababu ana PRIDE na kadhalika, bali hawezi kuomba msamaha kwasababu;

1) Hatambui kama amekosea sehemu yoyote, anaamini na kusimamia anacho kiamini yeye binafsi yakua hajamkosea yoyote. Zengwe lilianzishwa na Cyprian Musiba na kushikiliwa kasi na Raia wanao muunga mkono (Hazikua kiki au chanzo chochote kutoka kwake direct).

2) Ana influence kubwa kwa jamii, wanasiasa, serikalini (Na yeye binafsi analitambua hili). 80% ya watu wanaofatilia siasa kwa sasa macho yapo kwake, maamuzi anayochukua, matamko anayotoa, mambo anayopost n.k.. CV yake toka chuo inajieleza vizuri, wala haina haja ya kumchambua zaidi ya kwanini hakurupuki kuichafua taaswira yake kwa umma.

3) Ana nia ya kuchukua form ya kugombea urais. Kuomba kwake msamaha atakua amejishusha chini (In indirect way, he will prove to the public and himself to be lower than CCM chairperson).

4) He is brave enough kucheza karata zake kisiasa. Akipata na akikosa kwake itakua sawa na haitamu affect kuendelea na maisha yake ya mbele.

5) Atapotea kisiasa kama ataomba msamaha. Public yote itapata sababu ya kumdhihaki, kumkejeli na kumchambua maamuzi yake (Wengi watamtolea maneno ya shombo).


#Uchambuzi wangu kutokana na uelewa wangu. Nothing Personal.

#Maybe nta UPDATE zaidi.
 
Makamba atakwenda kuomba msamaha kwakua ni kigeu geu na hana self esteem!!

I know Makamba Snr tangu akiwa katibu wa CCM huko Tanga!! Ni mtu wa kujipendekeza na asiye na msimamo kabisa!!

Makamba bila Lowassa na JK asingefika hapo alipo hivyo si mtu wa juhudi.

Makamba ana very low emotional intelligence kumlinganisha na Kinana au Membe!! Japo ili kulinda maslahi yake machafu namuona Kinana akienda kupiga goti.

I doubt kama kweli Nape ni mmwera kama niwajuavyo wamwera vizuri linapokuja suala la kulinda utu au heshima yao.

Mwisho kabisa haya matukio yanatufundisha jinsi tulivyo na mifumo ya kikoloni kuliko wakoloni weupe!

Karne hii mtu anaamini hawezi ishi bila kudra za mwanadamu mwenzie ni huruma sana!!
 
Huo msamaha wa hadharani ni wa hovyo maana lengo lake kuu ni lile la kujilimbikizia tu utukufu na ufalme kwa mtu mmoja bila sababu yoyote ile ya msingi.

Yaani hutaki ukosolewe, hutaki ushauri, hutaki mtu awe na mawazo tofauti na ya kwako! How come? Hata ningekua mimi, nisingepiga magoti wallah! Labda kama anasingiziwa kuhusu hayo maneno aliyoambiwa.
 
Ukinijibu maswali haya nitakuja ku discuss topic yako ,and am sure utapata ninaamini pia haya maswali ndio mzizi wa hoja zako na resolution ya claims zako ,kama ifuatavyo

1.Nani Alivujisha audio calls na kwa lengo lipi?kuna mtuhumiwa amekamatwa hadi Leo hii?ni nani mara amewahi kuropoka kwenye public kuwa anasikiliza simu za watu which is against the constitution?

2.Makamba Jr, nitajie neno la kejeli au matusi lililosababisha kuomba samahani

3.Membe ,Kinana,Makamba Sr kwenye ile audio clip wamemuongelea neno gani baya au tusi ambao ,namba moja anapaswa kuomba msamaha?

Namaliza hivi:ilikua ni strategy ya mtu fulani...aombwe msamaha
Hivi inakuaje mtu una cheo kikubwa kama kile bado you are begging for other people's fame?
 
Ahsante mkuu, ila hili la kwamba ulimchomea Erick Kabendera lina kuweka kwenye kingdom hadi species moja na mashetani wasiojulikana!

That means nawe ni usiyejulikana unayejulikana na unaanza unafiki wako........ Kabendera is deadly sick kwa sasa, how do you benefit?
Mwenyezi Mungu amsaidie apone.
Hivi Kabendera ndo nani?
 
Kuna mabadiliko makubwa nayaona yanatokea nchini sasa, ambayo ni lazma yawe na sacrifices...

Kuna matukio chanya ambayo hatujayazoea...Uki-analyze recent history vs current events, unaweza ku-generate insights flani flani...is this not similar to what watu wa masoko wanaita "rebranding"?

Kiukweli kabisa ni jambo jema hata kama ni la muda mfupi kwa ajili ya tukio flani siku zijazo au ni some pressure mounting, au ni kutambua mema na mabaya....Whatever the case.
 
IMG-20190913-WA0004.jpg
 
Back
Top Bottom