PSSSF yatangaza neema mpya kwa wastaafu

diana chumbikino

JF-Expert Member
May 29, 2018
428
368
NI neema tupu: Hivi ndivyo unavyoweza kueleza baada ya Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), kuanza kulipa wastaafu tofauti ya fedha iliyokuwa haijalipwa kutokana na matumizi ya kikokotoo kipya.

Kanuni hizo zilianza kufanya kazi Agosti mwaka jana, baada ya marekebisho ya Sheria ya Hifadhi ya Jamii iliyounganisha mifuko wa PSPF, PPF, LEPF na GEPF na kuunda mfuko wa PSSSF. Watumishi waliostaafu kuanzia Agosti mosi, mwaka jana walilipwa mafao yao kwa kikokotoo kipya cha asilimia 25 na baada ya uamuzi wa Rais John Magufuli wa kurudisha kikokotoo cha zamani cha asimilia 50, wastaafu wa PSSSF wataanza kuongezewa walichopunjwa. Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Eliud Sanga, alisema wastaafu hao wanastahili kulipwa Sh. bilioni 119.

Alisema tangu kutolewa kwa agizo la rais Desemba 28, mwaka jana, walianza kuwatambua na kuwalipa wale waliopunjwa malipo ya mkupuo na wanaendelea kuwalipa. “Tulishaanza kuwalipa ile tofauti ya fedha ya asilimia 25 ili kutimiza asilimia 50 kwa mujibu wa kikokotoo cha zamani cha PSPF, tunaendelea kuwalipa kwa kadiri hadi tutakapomaliza,” alisema na kuongeza: “Agizo la rais ni la kutekeleza moja kwa moja halina kusubiri, nasi tulishaanza kuwalipa wastaafu.

wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii, ni kuwa mfuko wa NSSF ambao ni kwa ajili ya sekta binafsi na PSSF zingelipa mafao kwa kikokotoo kimoja. Kikokotoo kilichokuwa kimependekezwa ni asilimia 25 ya malipo ya mkupuo, ambayo fomula yake ni moja ya 580 mara jumla ya mishahara mara mishahara minono ya miaka mitatu katika miaka kumi ya kukaribia kustaafu mara 12.5 mara asilimia 25. Pensheni ya kila mwezi ni moja ya 580 mara jumla ya mishahara mara mishahara minono ya miezi mitatu kwa miaka 10 ya mwisho ya mstaafu mara asilimia 75 mara 1/12.

Desemba 28, mwaka jana, Rais alikutana na viongozi wa vyama vya wafanyakazi, wakuu wa mifuko ya PSSSF na NSSF, Mdhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana na Ajira, na baada ya majadiliano ya muda mrefu alitangaza kufuta kikokotoo kipya na kutaka kila mfuko kurejea kwenye kikokotoo walichokuwa wanatumia kabla. Kwa mabadiliko hayo, NSSF itaendelea kutumia kikokotoo cha asilimia 25 kwa kuwa ndicho kilichokuwa kwenye kanuni za mwaka 2014 ambazo zilitumika kwenye mifuko yote. Kwa mabadiliko hayo kwa sasa kutakuwa na vikokotoo viwili ambavyo vinatofautiana miaka ya makadirio ya kuishi ikiwa ni NSSF miaka 12.5 na PSSSF ni miaka 15.5.
 
Neema hapo iko wapi wakati ni stahili zao
Kww mujibu wa sheria? Haki yako utaitaje ni neema???
 
  • Thanks
Reactions: rr3
Hivi huyu Sanga anazungumzia waliopunjwa kutokana na vikokotoo vipi madai mengine ya wastaafu kabla ya hapo. Mbona viongozi wa sasa wanashindwa kujituma hadi raisi awawekee maneno mdomoni. Kuna madai mengi kwa mfano ya PPF kwa wastaafu hata pale mahakama ilipo elekeza kulipa lakini bado. Mfano ni suala la madai ya wastaafu wa ATCL ambalo bado lina pigwa dana dana kati ya Wizara Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, na Hazina. Wastaafu wamefanyiwa uhakiki kule ATCL mara kadhaa lakini hawalipwi. Raisi unaombwa ulitafutie ufumbuzi suala hili kwani ipo barua ya wastaafu ilitumwa IKULU kuomba ufumbuzi wazee wamesubiri sana japo wenye bahati wamerejea kwenye ajira ya mkataba kama maengineer. RAISI WA WANYONGE WASAIDIE WAZEE WASTAAFU ATCL.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
To me naona ni hali tu ya ubinafsi ambayo binadamu wengi imetutawala.Tunapenda kujifikiria maslahi yetu zaidi kuliko ya wenzetu ndio maana hatujali hata kama wenzetu watakufa njaa.Sitakwenda kwenye details nikimachisha na hali ya Mifuko kwa sasa.Nimebaki kusikitika tu
 
NI neema tupu: Hivi ndivyo unavyoweza kueleza baada ya Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), kuanza kulipa wastaafu tofauti ya fedha iliyokuwa haijalipwa kutokana na matumizi ya kikokotoo kipya.

Kanuni hizo zilianza kufanya kazi Agosti mwaka jana, baada ya marekebisho ya Sheria ya Hifadhi ya Jamii iliyounganisha mifuko wa PSPF, PPF, LEPF na GEPF na kuunda mfuko wa PSSSF. Watumishi waliostaafu kuanzia Agosti mosi, mwaka jana walilipwa mafao yao kwa kikokotoo kipya cha asilimia 25 na baada ya uamuzi wa Rais John Magufuli wa kurudisha kikokotoo cha zamani cha asimilia 50, wastaafu wa PSSSF wataanza kuongezewa walichopunjwa. Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Eliud Sanga, alisema wastaafu hao wanastahili kulipwa Sh. bilioni 119.

Alisema tangu kutolewa kwa agizo la rais Desemba 28, mwaka jana, walianza kuwatambua na kuwalipa wale waliopunjwa malipo ya mkupuo na wanaendelea kuwalipa. “Tulishaanza kuwalipa ile tofauti ya fedha ya asilimia 25 ili kutimiza asilimia 50 kwa mujibu wa kikokotoo cha zamani cha PSPF, tunaendelea kuwalipa kwa kadiri hadi tutakapomaliza,” alisema na kuongeza: “Agizo la rais ni la kutekeleza moja kwa moja halina kusubiri, nasi tulishaanza kuwalipa wastaafu.

wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii, ni kuwa mfuko wa NSSF ambao ni kwa ajili ya sekta binafsi na PSSF zingelipa mafao kwa kikokotoo kimoja. Kikokotoo kilichokuwa kimependekezwa ni asilimia 25 ya malipo ya mkupuo, ambayo fomula yake ni moja ya 580 mara jumla ya mishahara mara mishahara minono ya miaka mitatu katika miaka kumi ya kukaribia kustaafu mara 12.5 mara asilimia 25. Pensheni ya kila mwezi ni moja ya 580 mara jumla ya mishahara mara mishahara minono ya miezi mitatu kwa miaka 10 ya mwisho ya mstaafu mara asilimia 75 mara 1/12.

Desemba 28, mwaka jana, Rais alikutana na viongozi wa vyama vya wafanyakazi, wakuu wa mifuko ya PSSSF na NSSF, Mdhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana na Ajira, na baada ya majadiliano ya muda mrefu alitangaza kufuta kikokotoo kipya na kutaka kila mfuko kurejea kwenye kikokotoo walichokuwa wanatumia kabla. Kwa mabadiliko hayo, NSSF itaendelea kutumia kikokotoo cha asilimia 25 kwa kuwa ndicho kilichokuwa kwenye kanuni za mwaka 2014 ambazo zilitumika kwenye mifuko yote. Kwa mabadiliko hayo kwa sasa kutakuwa na vikokotoo viwili ambavyo vinatofautiana miaka ya makadirio ya kuishi ikiwa ni NSSF miaka 12.5 na PSSSF ni miaka 15.5.
Ni vema mtumishi akalipwa kiasi chote . Kwa Nini iwezekane kwa wanasiasa ishindikane kwa Hawa wanyonge????? Kama sivyo mtumishi alambe 75% ibaki hiyo 25% .

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom