PSSSF ijitathimini kwa kutokulipa mafao kwa wakati

Haya ndio ya kujadiliwa ili kuwasaidia watu kupata stahiki zao lakini cha ajabu nyuzi kama hizi hata michango inakuwa michache

Panapotokea mambo kama yakina lijualikali,sijui chadema kinajifia michango inakuwa kama yote..ikumbukwe ya kwamba hivyo vyama vina watu ambao ni wafanyakazi ambao ni wastaafu watarajiwa,kila siku tunaimba humu siasa ndio inayoamua hatma ya mfumo wetu wa kimaisha pamoja na waki-nchi.

PSSSF nanyi ni majipu,wengine mpaka leo tuna suffer kukamilisha taaratibu za kupata mafao yetu kwa tulioachishwa kazi,Mara lete barua ya mwanasheria yenye kuthibitisha kama hujapata kazi,sijui copy kitambulisho ipigwe muhuri wa mwanasheria,sijui andika barua kwanini mchango wako ulichelewa kuingizwa baada ya wewe kuanza kazi, basi tafrani tupu.

Kwa hili la wastaafu tafadhali wafanyie wepesi kupata stahiki zao,si mlikuwa mnasema kuwa tumeondoa fao LA kujitoa Pamoja na kutengeneza kikokoto kipya eti kisa mnatuonea huruma tukifika kuwa wazee tutateseka, Sasa wazee ndio hao wameshastaafu muwaone huruma kwa kuwalipa mafao yao.

Yaani hii nchi inataratibu za kishenzi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Urasimu kwenye hii nchi ni janga
 
Hahaha Watalipaje pesa wakati huu wa vita dhidi ya covid-19?! Tuko vitani hamuelewi nini?! Tuko vitani wewe unaomba pesa?!
 
Nina mwaka wa miwili nafuatilia fao langu PSSSF bila mafanikio nkifika pale huwa natamani hata nivae bomu niilipue ile ofisi nzima ili iwe legacy kwa wastaafu wanaodai hela zao.

Wanakera saana.
 
Uliza walipokua huko ppf, walikuwa wakijilipa gratuity mamilion kila baaada ya miaka miwili
Bora umetaja jina. Yupo mstaafu mmoja wanamzungusha sana tena kwasababu ambazo hazimuhusu. Nakusanya evidence alafu nitatumia hadi PA ili wajue wanachofanya ni uhuni.

Wao wakistaafu wanaweza kuishi miaka miwili bila hata senti moja kulipwa? Wastaafu wananyanyasika sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ebu tuone kwa wabunge Kama watacheleweshewa mafao ndipo tujijue sisi wastaafu hatuthaminiwi na mtu
 
Nchi imeoza hii.. Mambo ya msingi Kama haya hakuna anayefuatilia.....

Watendaji wa Serikali wao Ni matamko tu Kila siku.....

Wabunge nao ndio hovyo kabisa, yeye analipwa mafao yake Hapo hapo.... Huo muda wa kufuatilia ya mpiga kura wake Hana.....

Ukitaka kujua nchi hii imeoza..... Nini kinamshinda mtumishi wa umma kufuata Agizo la Rais???????
 
We with draw competition
So stick to the point if there is no competition there is actually no efficiency
Kwanini tulivunja mifuko mingine hapo tunakosa ushindani kama tunakosa ushindani basi hakuna uwajibikaji bora
Crdb ni bora tu pale akishindwanisha na nmb,postal bank nbc nk
 
Bora umetaja jina. Yupo mstaafu mmoja wanamzungusha sana tena kwasababu ambazo hazimuhusu. Nakusanya evidence alafu nitatumia hadi PA ili wajue wanachofanya ni uhuni.

Wao wakistaafu wanaweza kuishi miaka miwili bila hata senti moja kulipwa? Wastaafu wananyanyasika sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Inasikitisha sana kusema kweli, kumbuka wao (wanasiasa) wakistaafu wanalipwa mamilioni yao yote kwa mkupuo ila wazee masikini wanasoteshwa miaka na miaka kupata haki yao, huu ni unyanyasaji na uonevu mkubwa.
 
Hili dude pssf limerudisha urasimu na ukiritimba wa zamani.Watu wengi watakufa na pressure kabla hawajapata mafao.Na warithi sioni wanazipataje kama sio kudhulumiwa tu
 
Pumbavu sana hao hela wanakukata kwa lazima ukifika muda wa kupewa chako zengwe linaanza.Mstaafu anakaa miaka bila kulipwa ? Kila siku faili lipo kwa cashier na huduma kwa wateja mavi mavi tu.Yakionekana kwenye TV na tshirt zao za polo utasema majitu ya maana kumbe mavi mavi tu.Hawa ndio wanamuangusha mawe.
 
Mzee wangu amestafu kitambo tuu ila hela yake anazungushwa tuu, kuna jamaa mmoja pale kwenye mfuko anamwomba million 4 ili amsaidie kupata hela yake halali..... Pale kuna wala ruswa sana ndo wanacheleweshewa ili watengeneze mazingira ya rushwa.

Kuna rushwa sana pale. Serikali iangazie pale
 
Mara ya mwisho nilipewa form nikaenda nikajaza kila kitu kikawa tayari, siku narejesha nikakutana na tangazo limebandikwa ...... Form zote za madai ziletwe na waajiri, nikajifanya sijaona tangazo nikaenda dirishan kukabidhi, akarudia yaleyale kwamba sipokei form toka kwa aliyekua muajiriwa, form zote ziletwe na aliyekua muajiri wako........nimerudisha zile form na sijui nn kinaendelea mpka sasa, nadhan ndicho walichokua wanalenga.
 
Acha hao wazee wapate msoto , hii nchi bila kila mtu kuguswa kea namna moja au nyingine hatutakukuja kuwa na collective measures za kudai haki zetu..


Hao wazee wabanwe kisawasawa.
 
Mzee wangu amestafu kitambo tuu ila hela yake anazungushwa tuu, kuna jamaa mmoja pale kwenye mfuko anamwomba million 4 ili amsaidie kupata hela yake halali..... Pale kuna wala ruswa sana ndo wanacheleweshewa ili watengeneze mazingira ya rushwa.

Kuna rushwa sana pale. Serikali iangazie pale

Wastaafu kupigwa danadana hapo PSSSF ni kawaida kabisaaa.
 
Back
Top Bottom