Propaganda za wapinzani zimepungua JF

Masaka

JF-Expert Member
Oct 1, 2007
437
1
Naona sasa watoa propaganda wa chadema na wapinzani wengine wametulia na kupunguza propaganda zao hapa jf. Inaonekana members wenye kazi ya propaganda na uzushi wameishiwa. kazi inayofanywa na ccm wakiongozwa na kamanda wao Kikwete imeonekana kushika kasi hasa baada ya bajeti mpya kutoka na sasa watu hawana cha kusema.

Wabunge wa ccm wameanza kushughulikia matatizo kidogokidogo ndani ya chama na sasa mambo yamekuwa safi na yanategemewa kuwa safi zaidi kwenye hili bunge.

Watoa propaganda nao wameanza kujichimbia na wengine hata hawatokezi tena hapa. Balance hii ambayo wengine tumekuwa tunaiomba hapa naona sasa imepatikana na kadri Kikwete anavyoendelea kufanya kazi nzuri ya kuleta maendeleo ya nchi basi mengi mazuri yatakuja.

kidumu chama cha mapinduzi.
 
Kazi gani ya Kikwete? Wizi na procastination?

Bajeti gani? Huko kufanyia mchezo wa kuigiza msaada unakuita bajeti?
 
ni ujinga kutegemea watu waharibu ili utoe umbeya unatakiwa uombe mabaya yasifanyike.

Tumaini
 
Naona sasa watoa propaganda wa chadema na wapinzani wengine wametulia na kupunguza propaganda zao hapa jf. Inaonekana members wenye kazi ya propaganda na uzushi wameishiwa. kazi inayofanywa na ccm wakiongozwa na kamanda wao Kikwete imeonekana kushika kasi hasa baada ya bajeti mpya kutoka na sasa watu hawana cha kusema.

Wabunge wa ccm wameanza kushughulikia matatizo kidogokidogo ndani ya chama na sasa mambo yamekuwa safi na yanategemewa kuwa safi zaidi kwenye hili bunge.

Watoa propaganda nao wameanza kujichimbia na wengine hata hawatokezi tena hapa. Balance hii ambayo wengine tumekuwa tunaiomba hapa naona sasa imepatikana na kadri Kikwete anavyoendelea kufanya kazi nzuri ya kuleta maendeleo ya nchi basi mengi mazuri yatakuja.

kidumu chama cha mapinduzi.

Achana na dhana potofu! Wanachama wa CHADEMA hapa ni wachache mno! Wengi tuna mapenzi na nchi yetu na kuhuzunishwa na mwelekeo wake ambao kila kukicha maisha yanazidi kuwa magumu kwa Watanzania walio wengi wakati mafisadi wachache wanakuwa matajiri wa kupindukia kwa kuiba rasilimali za Watanzania na makusanyo yao ya kodi na kisha kujijengea majumba ya kifahari ndani na nje ya nchi na kununua magari ya kifahari.

Hivi ni wanachama wangapi unaowafahamu hapa JF ambao pia wana uanachama wa CHADEMA? Acha kubwabwaja kaka!! kama huna la kusema bora ukae kimya kuliko kuja na dhana potofu. Watanzania tuna haki ya kukilaumu chama kilicho madarakani na hata vyama vya upinzani na hapa JF yote hayo yanafanyika, siyo lazima tuwe wanachama wa chadema ili kukiromea chama cha mafisadi.

Usiwe unabwabwaja kama Kasuku kwa kupewa mistari ya kuandika hapa JF na wewe kuiandika kama ulivyopewa bila kuhoji chochote. Jifunze tabia ya kuchanganua mambo na kujiuliza maswali kabla ya kuimba kama kasuku.
 
Naona sasa watoa propaganda wa chadema na wapinzani wengine wametulia na kupunguza propaganda zao hapa jf. Inaonekana members wenye kazi ya propaganda na uzushi wameishiwa. kazi inayofanywa na ccm wakiongozwa na kamanda wao Kikwete imeonekana kushika kasi hasa baada ya bajeti mpya kutoka na sasa watu hawana cha kusema.

Wabunge wa ccm wameanza kushughulikia matatizo kidogokidogo ndani ya chama na sasa mambo yamekuwa safi na yanategemewa kuwa safi zaidi kwenye hili bunge.

Watoa propaganda nao wameanza kujichimbia na wengine hata hawatokezi tena hapa. Balance hii ambayo wengine tumekuwa tunaiomba hapa naona sasa imepatikana na kadri Kikwete anavyoendelea kufanya kazi nzuri ya kuleta maendeleo ya nchi basi mengi mazuri yatakuja.

kidumu chama cha mapinduzi.

Ulichokisema hapo hakina mantiki!

Kama unasema vilio vya vya upinzani vimepungua kwa sababu CCM na Kikwete wameanza kufanya kazi, ina maana waliyokuwa wanayasema hayakuwa propaganda. Na hapo hapo ina maana unakubali CCM na Kikwete walikuwa wachovu. Unaona usivyo make sense? Watu wengine vipi jamani?
 
duh ! mod kaamua kuifanyia MBOWEISM hii thread !! ukiona kitu ambacho ni kizuri kwa serikali na watu wakaanza kukiponda na thread ikahamishwa ili wapinzani wasione jema lolote, hiyo huitwa MBOWEISM !!
 
Achana na dhana potofu! Wanachama wa CHADEMA hapa ni wachache mno! Wengi tuna mapenzi na nchi yetu na kuhuzunishwa na mwelekeo wake ambao kila kukicha maisha yanazidi kuwa magumu kwa Watanzania walio wengi wakati mafisadi wachache wanakuwa matajiri wa kupindukia kwa kuiba rasilimali za Watanzania na makusanyo yao ya kodi na kisha kujijengea majumba ya kifahari ndani na nje ya nchi na kununua magari ya kifahari.

Hivi ni wanachama wangapi unaowafahamu hapa JF ambao pia wana uanachama wa CHADEMA? Acha kubwabwaja kaka!! kama huna la kusema bora ukae kimya kuliko kuja na dhana potofu. Watanzania tuna haki ya kukilaumu chama kilicho madarakani na hata vyama vya upinzani na hapa JF yote hayo yanafanyika, siyo lazima tuwe wanachama wa chadema ili kukiromea chama cha mafisadi.

Usiwe unabwabwaja kama Kasuku kwa kupewa mistari ya kuandika hapa JF na wewe kuiandika kama ulivyopewa bila kuhoji chochote. Jifunze tabia ya kuchanganua mambo na kujiuliza maswali kabla ya kuimba kama kasuku.

Mhh, kwa kweli sijui kama ni wanachama wa chadema ni wachache hapa JF na kama hili ni kweli basi nafurahi sana kujua kuwa wana chadema hapa JF ni wachache sana. Ni vizuri pia lakini kujua kuwa wana ccm tumeongezeka hapa na balance imepatikana.

Tujenge nchi sasa na tuache majungu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom