Nchi na mataifa mbalimbali sasa wanaendeleza hamasa ya kuungana na chama chenye malengo ya kuongoza nchi kwa misingi ya amani, umoja, na upendo, na maendeleo pia na kuimarisha diplomasia. Hii ni kutokana na itikadi na misingi mizuri ya kuanzishwa kwake.
Prof Wajackoya, nguli wa sheria na mwanasiasa maarufu nchini Kenya, akitoa salamu zake kwenye mkutano mkubwa uliokusanyika kumpokea Kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Godbless Lema, aliyewasili nchini mchana wa leo kupitia Uwanja wa Ndege wa KIA. Wajackoya anasema ametumwa na Mh Raila Odinga kuomba radhi kwa kuwa hapo nyuma alikuwa mshirika wa Chadema lakini akalega kidogo. Lakini sasa amerudisha uhusiano na chama hicho makini.
Itakumbukwa kuwa kwenye siasa za Tanzania miaka michache iliyopita, Raila Odinga alikuwa rafiki wa karibu sana wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kufikia kiwango cha kutembeleana mpaka nyumbani. Pia iliwahi kusemwa kwamba mmoja wa watoto wa Dr John Pombe Magufuli (R.I.P) alikuwa anasomea Kenya akiishi kwenye familia ya Raila.
Prof Wajackoya, nguli wa sheria na mwanasiasa maarufu nchini Kenya, akitoa salamu zake kwenye mkutano mkubwa uliokusanyika kumpokea Kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Godbless Lema, aliyewasili nchini mchana wa leo kupitia Uwanja wa Ndege wa KIA. Wajackoya anasema ametumwa na Mh Raila Odinga kuomba radhi kwa kuwa hapo nyuma alikuwa mshirika wa Chadema lakini akalega kidogo. Lakini sasa amerudisha uhusiano na chama hicho makini.
Itakumbukwa kuwa kwenye siasa za Tanzania miaka michache iliyopita, Raila Odinga alikuwa rafiki wa karibu sana wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kufikia kiwango cha kutembeleana mpaka nyumbani. Pia iliwahi kusemwa kwamba mmoja wa watoto wa Dr John Pombe Magufuli (R.I.P) alikuwa anasomea Kenya akiishi kwenye familia ya Raila.