Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,488
- 13,608
Amesikika Profesa maarufu wa Chuo Kikuu cha Dar Issa Shivji akiongelea namna wafanyabiashara wakishakuwa wametajirika wanavyovyamia masuala ya kisiasa na kitaalam. Labda ni baada ya kusoma majina ya wale wajumbe wa bodi ya TANESCO ndio akajenga hoja alizozijenga. Kwamba wafanyabiashara wenye akili za kibiashara ni ngumu kuwa na ufanisi wenye kujikita katika kutatua matatizo ya walio wengi pasipo kutanguliza nia zake za kisiasa.
Anaweza kuwa na hoja lakini naziona zimejikita katika kutaka kumpaisha yeye Shivji kama yeye lakini sizioni zikiwa zikitazama mbali. Ni hoja nyepesi kama tukiamua kuiangalia historia ya wabunge ambao ni wafanyabiashara na hata kuingia kwao bungeni hakukuondoa ule ukweli kwamba wao ni watu wa sekta binafsi.
Ipo mifano mingi ya wafanyabiashara na namna walivyokuwa ni sehemu ya utungaji wa sera na sehemu ya utatuzi wa matatizo sugu ya wananchi. Mifano ni mingi, miaka ile ya 1990 alikuwepo hayati Abbas Gulamali, aliyeanzia Yanga kama mdhamini halafu akaingia bungeni akiwa mbunge wa jimbo moja la Morogoro.
Hayati Gulamali aliweza kuchanganya siasa na maslahi yake mapana ya biashara pasipo kuharibu upande wowote kati ya hizo mbili. RIP Gulamali alikuwa ni mmoja wa matajiri wa kwanza kabisa kusimama na kutetea wakazi wa Morogoro akiwa Bungeni, wala usingeweza kuutambua ule ufanyabiashara wake wa kiwango cha juu aliokuwa nao kipindi kile.
Mzee Mzindakaya ni mfano mwingine ya namna ujasiriamali unavyoweza kuchanganywa na masuala ya kisiasa, huyu amekuwa mbunge kwa miongo kama minne na zaidi kidogo. Ni mkulima mkubwa na wakati huo huo ni mtunga seramahiri, mwenye kuchanganya vyema masuala hayo mawili.
Mohamed Dewji ni mfano mwingin wa tajiri anavyoweza kuwa mwanasiasa hapa Tanzania. Alianzia michezoni akaenda siasani na baadae amerudi michezoni. Na akiwa siasani aliweza kuchagiza maendeleo makubwa ya jimbo lake la Singida. Mohamed ni mmoja wa wajasiriamali wenye uchungu na maisha ya kawaida ya mtanzania. Misaada yote aliyoitoa jimboni kwake haina nia za kulikuza jina lake mwenyewe zaidi ya kuukuza ubinadamu wa wapiga kura wake.
Mwingine ni Shabiby wa Morogoro. Tajiri huyu akisimama bungeni anachokiongelea kina uhusiano na utetezi wa moja kwa moja wa shida za wakazi wa Morogoro. Ni mpaka uambiwe kuwa huyu mzungumzaji wa sasa ni mmiliki wa mabasi mengi na ni mjasiriamali mkubwa wa mkoa wa Morogoro.
Kuamini kwamba mfanyabiashara ni mtu wa kumhisi vibaya haswa pale anapokuwa na maslahi kwenye taasisi za kisiasa ni imani potofu.Ni mtazamo wa Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere kwamba ubepari ni unyama. Profes Shivji akiwa ni mfuasi kindakindaki wa Mwalimu Nyerere anaweza kueleweka akiwa na mitazamo ya kutowaamini wafanyabiashara.
Lakini dunia ya sasa ambayo kuna wale wasemaji wenye kuwapa moyo wananchi (Motivational Speakers) huwezi kuukwepa ushawishi wa tajiri kwenye siasa. Dunia hii ya mtu kuanza maisha kama muuzaji wa bidhaa za kutembeza karibu na taa za magari mijini na mpaka kufika hatua ya kusimama kama mjasiriamali mkubwa, huwezi kuukwepa ushawishi wake wala simulizi nzito zenye kutia moyo.
Tujaribu kutazama kile chanya kinachoweza kuwa ni mchango wa tajiri anapopewa nafasi ndani ya taasisi nyeti za kiserikali kuliko kutanguliza kwanza ile hofu ya yeye kuweza kuitumia vibaya taasisi hiyo kwa masuala ya kibinafsi. Tajiri siku zote tunamuona kama ni mwizi kwanza kabla ya kuwa tajiri, tunamuona ni mtu siye wa kumuamini kwanza kwa ubinadamu wake na uzoefu wake wa kibiashara. Hizi dhana za kijamaa zinatunyima mengi na zinaendelea kutokosesha ule uhuru wa kiushindani wenye kuanzia kichwani kwanza kabla ya kushuka kwenye matendo yetu.
Marekani ni utajiri wao wote walishindwa kuukwepa ushawishi wa Ross Perot miaka ile ya 1980, akiwa ni mfanyabiashara mkubwa aliyeutafuta na kuupata utajiri kwa nguvu zake mwenyewe. Na ni huko Marekani nchi ya dunia ya kwanza ambapo hatuwezi kuwa na Tanzania pasipo uwepo wa mahusiano hai ya kisiasa na kiuchumi.
Kwa kweli Profesa Shivji amekosea kutokuwa na imani na sekta binafsi mpaka akaiwekea wasiwasi kichwani mwake. Waendeshaji wa bandari kubwa kubwa kama zile za Afrika ya kusini ni wafanyabiashara wa zamani waliofanikiwa, ndio wenye kuwekeza uzoefu wao wenye kuleta tija. Mfano wa karibu ni Erick Hamisi, Bosi wa TPA wa sasa ambaye msingi wake ni sekta ya benki namna anavyofanya mapinduzi pale bandarini tofauti na Kaka Kakoko aliyekosa uzoefu wa kibiashara na kiuchumi.
Profesa Shivji naamini kujifunza ni daima kwani elimu haina mwisho. Jaribu kusoma kwa kina ushawishi walionao wafanyabiashara kwenye sekta za umma na utajifunza mengi yenye umuhimu.
Anaweza kuwa na hoja lakini naziona zimejikita katika kutaka kumpaisha yeye Shivji kama yeye lakini sizioni zikiwa zikitazama mbali. Ni hoja nyepesi kama tukiamua kuiangalia historia ya wabunge ambao ni wafanyabiashara na hata kuingia kwao bungeni hakukuondoa ule ukweli kwamba wao ni watu wa sekta binafsi.
Ipo mifano mingi ya wafanyabiashara na namna walivyokuwa ni sehemu ya utungaji wa sera na sehemu ya utatuzi wa matatizo sugu ya wananchi. Mifano ni mingi, miaka ile ya 1990 alikuwepo hayati Abbas Gulamali, aliyeanzia Yanga kama mdhamini halafu akaingia bungeni akiwa mbunge wa jimbo moja la Morogoro.
Hayati Gulamali aliweza kuchanganya siasa na maslahi yake mapana ya biashara pasipo kuharibu upande wowote kati ya hizo mbili. RIP Gulamali alikuwa ni mmoja wa matajiri wa kwanza kabisa kusimama na kutetea wakazi wa Morogoro akiwa Bungeni, wala usingeweza kuutambua ule ufanyabiashara wake wa kiwango cha juu aliokuwa nao kipindi kile.
Mzee Mzindakaya ni mfano mwingine ya namna ujasiriamali unavyoweza kuchanganywa na masuala ya kisiasa, huyu amekuwa mbunge kwa miongo kama minne na zaidi kidogo. Ni mkulima mkubwa na wakati huo huo ni mtunga seramahiri, mwenye kuchanganya vyema masuala hayo mawili.
Mohamed Dewji ni mfano mwingin wa tajiri anavyoweza kuwa mwanasiasa hapa Tanzania. Alianzia michezoni akaenda siasani na baadae amerudi michezoni. Na akiwa siasani aliweza kuchagiza maendeleo makubwa ya jimbo lake la Singida. Mohamed ni mmoja wa wajasiriamali wenye uchungu na maisha ya kawaida ya mtanzania. Misaada yote aliyoitoa jimboni kwake haina nia za kulikuza jina lake mwenyewe zaidi ya kuukuza ubinadamu wa wapiga kura wake.
Mwingine ni Shabiby wa Morogoro. Tajiri huyu akisimama bungeni anachokiongelea kina uhusiano na utetezi wa moja kwa moja wa shida za wakazi wa Morogoro. Ni mpaka uambiwe kuwa huyu mzungumzaji wa sasa ni mmiliki wa mabasi mengi na ni mjasiriamali mkubwa wa mkoa wa Morogoro.
Kuamini kwamba mfanyabiashara ni mtu wa kumhisi vibaya haswa pale anapokuwa na maslahi kwenye taasisi za kisiasa ni imani potofu.Ni mtazamo wa Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere kwamba ubepari ni unyama. Profes Shivji akiwa ni mfuasi kindakindaki wa Mwalimu Nyerere anaweza kueleweka akiwa na mitazamo ya kutowaamini wafanyabiashara.
Lakini dunia ya sasa ambayo kuna wale wasemaji wenye kuwapa moyo wananchi (Motivational Speakers) huwezi kuukwepa ushawishi wa tajiri kwenye siasa. Dunia hii ya mtu kuanza maisha kama muuzaji wa bidhaa za kutembeza karibu na taa za magari mijini na mpaka kufika hatua ya kusimama kama mjasiriamali mkubwa, huwezi kuukwepa ushawishi wake wala simulizi nzito zenye kutia moyo.
Tujaribu kutazama kile chanya kinachoweza kuwa ni mchango wa tajiri anapopewa nafasi ndani ya taasisi nyeti za kiserikali kuliko kutanguliza kwanza ile hofu ya yeye kuweza kuitumia vibaya taasisi hiyo kwa masuala ya kibinafsi. Tajiri siku zote tunamuona kama ni mwizi kwanza kabla ya kuwa tajiri, tunamuona ni mtu siye wa kumuamini kwanza kwa ubinadamu wake na uzoefu wake wa kibiashara. Hizi dhana za kijamaa zinatunyima mengi na zinaendelea kutokosesha ule uhuru wa kiushindani wenye kuanzia kichwani kwanza kabla ya kushuka kwenye matendo yetu.
Marekani ni utajiri wao wote walishindwa kuukwepa ushawishi wa Ross Perot miaka ile ya 1980, akiwa ni mfanyabiashara mkubwa aliyeutafuta na kuupata utajiri kwa nguvu zake mwenyewe. Na ni huko Marekani nchi ya dunia ya kwanza ambapo hatuwezi kuwa na Tanzania pasipo uwepo wa mahusiano hai ya kisiasa na kiuchumi.
Kwa kweli Profesa Shivji amekosea kutokuwa na imani na sekta binafsi mpaka akaiwekea wasiwasi kichwani mwake. Waendeshaji wa bandari kubwa kubwa kama zile za Afrika ya kusini ni wafanyabiashara wa zamani waliofanikiwa, ndio wenye kuwekeza uzoefu wao wenye kuleta tija. Mfano wa karibu ni Erick Hamisi, Bosi wa TPA wa sasa ambaye msingi wake ni sekta ya benki namna anavyofanya mapinduzi pale bandarini tofauti na Kaka Kakoko aliyekosa uzoefu wa kibiashara na kiuchumi.
Profesa Shivji naamini kujifunza ni daima kwani elimu haina mwisho. Jaribu kusoma kwa kina ushawishi walionao wafanyabiashara kwenye sekta za umma na utajifunza mengi yenye umuhimu.