Profesa René Dumont aliyethubutu kumpinga wazi Nyerere kwenye suala la vijiji vya ujamaa kwa hoja nzito ambayo tayari imetimia

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,909
51,904
Nyerere miaka ya 1970 aliwahi kumualika Profesa Mfaransa Rene Dumont mtu aliyebobea kwenye uchumi wa kilimo aliyesifiwa mno kwa uwezo kwenye eneo hilo la uchumi wa kilimo duniani.

Alipofika alitembezwa sehemu mbalimbali vijijini. Wakati huo operation ya vijiji vya ujamaa ndio ilikuwa imepamba moto watu waliondolewa maeneo yao ya asili wakaenda kurundikwa sehemu moja ambayo Nyerere alisema ni kwa ajili ya kuwasaidia watu wapate huduma kirahisi za maji, afya, elimu n.k sehemu moja.

Profesa akampinga kasema alichofanya sio operation vijiji ni operation anzisha miji. Sababu miji yote duniani ilianzishwa kama centre za huduma kama hizo. Akasema maana ya kijiji ni kila nyumba kuzungukwa na mashamba wakati mji ni kila nyumba kuzungukwa na nyumba zingine.

Na ni kweli alichosema vijiji vingi vya operation vijiji sasa hivi ni miji midogo na waliokuwa watoto wa wana vijiji wamegeuka watoto wa mjini kulima hawataki wanafanya kazi tu za mijini za umachinga n.k

Nguvu kazi imepotea ambayo ingeachwa kule kule kijijini tungeendelea kuwa na wana vijiji kibao.
 
Mimi nimetokea katika vijiji hivyo, familia yangu inakaa maeneo ya kijiji lakini ina shamba lake lile ambalo babu yangu alilihama kipindi hicho na huwa nikienda huko naenda shamban kuendelee na kazi ya shamba.
Nyerere hakukosea kitu unaona jinsi umeme wa LEA unavyowafikia watu kwa urahisi na miradi ya maji,
Fikiria mfano shamba letu ni kubwa hekari zipatazo 100 na mwingine huenda hivyo hivyo huoni ingekuwa kazi kupata huduma,
Na tofauti na hivyo kuna wengine walisharudi kwenye maeneo yao ya mwanzo na wengine huendeleza shughuli za kilimo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyerere hakukosea kitu unaona jinsi umeme wa LEA unavyowafikia watu kwa urahisi na miradi ya maji,
Fikiria mfano shamba letu ni kubwa hekari zipatazo 100 na mwingine huenda hivyo hivyo huoni ingekuwa kazi kupata huduma,
Kwani walisema wanahitaji umeme? hitaji lao lilikuwa umeme miaka hiyo?
 
Nguvu kazi imepotea ambayo ingeachwa kule kule kijijini tungeendelea kuwa na wana vijiji kibao.
Hao "wanavijiji kibao" wangesaidia kitu gani?
Profesa akampinga kasema alichofanya sio operation vijiji ni operation anzisha miji. Sababu miji yote duniani ilianzishwa kama centre za huduma kama hizo. Akasema maana ya kijiji ni kila nyumba kuzungukwa na mashamba wakati mji ni kila nyumba kuzungukwa na nyumba zingine.
Ni wapi ulaya palipo na vijiji badala ya miji?

Kwa maana ya huduma, huoni kwamba lengo la kuwa na hivyo vijiji linaendelea kutekelezwa kadri uwezo unapopatikana? Maji, umeme, shule, hospitali, n.k.
 
Hao "wanavijiji kibao" wangesaidia kitu gani?

Ni wapi ulaya palipo na vijiji badala ya miji?

Kwa maana ya huduma, huoni kwamba lengo la kuwa na hivyo vijiji linaendelea kutekelezwa kadri uwezo unapopatikana? Maji, umeme, shule, hospitali, n.k.
Hilo lijitu halitaki kizazi kipya kinachoendelea kumea katika maeneo mengi ya nchi hii ikiwa jamii werevu baada ya exposure ya mjini. Anajua vijiji vikiisha nchini chama chake kitakosa mtaji wa wapiga kura ambao mara nyingi ni wale bumbumbu wa vijijini wanaodanganyika hata kwa kanga na kilo moja ya unga wa mahindi.
 
Kabla ya kumlaumu Nyerere hebu angalieni nchi za Asia ambazo ziliamini mambo ya kuboresha miji lakini sasa hivi zimekosa ardhi ya kilimo na sisi tunaingia ujinga huo huo kwa kubadili matumizi ya ardhi ya kilimo na kuwa ardhi ya makazi.
Nyerere hakuwa sahihi kwa kila jambo ila mazuri yake msiyapotoshe operation ya vijiji vya ujamaa ilikuwa na nia nzuri ila utekelezaji wake ulikuwa na mapumgufu ambayo ndiyo tungeyajadili.
 
Nyerere miaka ya 1970 aliwahi kumualika Profesa Mfaransa Rene Dumont mtu aliyebobea kwenye uchumi wa kilimo aliyesifiwa mno kwa uwezo kwenye eneo hilo la uchumi wa kilimo duniani.

Alipofika alitembezwa sehemu mbalimbali vijijini. Wakati huo operation ya vijiji vya ujamaa ndio ilikuwa imepamba moto watu waliondolewa maeneo yao ya asili wakaenda kurundikwa sehemu moja ambayo Nyerere alisema ni kwa ajili ya kuwasaidia watu wapate huduma kirahisi za maji, afya, elimu n.k sehemu moja.

Profesa akampinga kasema alichofanya sio operation vijiji ni operation anzisha miji. Sababu miji yote duniani ilianzishwa kama centre za huduma kama hizo. Akasema maana ya kijiji ni kila nyumba kuzungukwa na mashamba wakati mji ni kila nyumba kuzungukwa na nyumba zingine.

Na ni kweli alichosema vijiji vingi vya operation vijiji sasa hivi ni miji midogo na waliokuwa watoto wa wana vijiji wamegeuka watoto wa mjini kulima hawataki wanafanya kazi tu za mijini za umachinga n.k

Nguvu kazi imepotea ambayo ingeachwa kule kule kijijini tungeendelea kuwa na wana vijiji kibao.

Nimeipenda hii "Maana ya kijiji ni kila nyumba kuzungukwa na mashamba wakati mji ni kila nyumba kuzungukwa na nyumba zingine".
 
Nyerere miaka ya 1970 aliwahi kumualika Profesa Mfaransa Rene Dumont mtu aliyebobea kwenye uchumi wa kilimo aliyesifiwa mno kwa uwezo kwenye eneo hilo la uchumi wa kilimo duniani.

Alipofika alitembezwa sehemu mbalimbali vijijini. Wakati huo operation ya vijiji vya ujamaa ndio ilikuwa imepamba moto watu waliondolewa maeneo yao ya asili wakaenda kurundikwa sehemu moja ambayo Nyerere alisema ni kwa ajili ya kuwasaidia watu wapate huduma kirahisi za maji, afya, elimu n.k sehemu moja.

Profesa akampinga kasema alichofanya sio operation vijiji ni operation anzisha miji. Sababu miji yote duniani ilianzishwa kama centre za huduma kama hizo. Akasema maana ya kijiji ni kila nyumba kuzungukwa na mashamba wakati mji ni kila nyumba kuzungukwa na nyumba zingine.

Na ni kweli alichosema vijiji vingi vya operation vijiji sasa hivi ni miji midogo na waliokuwa watoto wa wana vijiji wamegeuka watoto wa mjini kulima hawataki wanafanya kazi tu za mijini za umachinga n.k

Nguvu kazi imepotea ambayo ingeachwa kule kule kijijini tungeendelea kuwa na wana vijiji kibao.
Sijakusoma unataka kutuambia nini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vikitajwa vijiji vya ujamaa sijui kwa nini fikra zangu hua zinarudi kwa RC wa Iringa Dr. Kleruu rafiki yake Said Mwamwindi.

Sent from my DUB-LX1 using Tapatalk
 
Back
Top Bottom