Profesa msolla - karibu tena sua

Ustaadh

JF-Expert Member
Oct 25, 2009
413
19
Naye aliyekuwa Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Peter Msolla, alisema ameridhishwa na uamuzi wa rais kumuacha nje ya baraza hilo.


“Nimeridhika kabisa na maamuzi aliyochukua Rais Kikwete, naamini maamuzi yake yamezingatia vigezo katika uteuzi… sina cha kuongeza zaidi ya kuwatakia kila la heri katika utendaji wao wa kazi za kila siku,” alisema Profesa Msolla.


Alisema moja ya rai anayowapa mawaziri wapya ni kuwataka watimize maratajio ya wananchi ambao wanaonekana kuwa na shauku ya maendeleo.


“Nimefanya kazi yangu kwa ubunifu mkubwa, nategemea hata kama wakihitaji maoni yangu niko tayari kushirikiana nao,” alisema Profesa Msolla.
 
Too late to act!!!!! Ebu tuwe wakweli jamani hivi prof. Msola anaweza kuwa na ushauri gani wa maana na unaohusu nini!!! Arudi tu akashike chaki aendelee kufundisha. Labda kama anataka aeleze namna Bodi ya Mikopo ilivyomshinda kuendesha. Ushauri siyo lazima ufocus kwenye mambo uliyofanikiwa tu hata kwa mambo uliyovurunda.
 
Back
Top Bottom