Profesa Lipumba ashangazwa na Rais Samia kumuachia mtu aliyekula njama katika wizi wa shilingi zaidi ya bilion 300 za Escrow kwa kutoa bilion 26 tu

Tuliwaambia JPM alikuwa mzalendo halisi na mtamkumbuka. Haya sasa mbona!??? Bi Mkubwa ajiuzulu tuu asingoje ilee 2025.

Ndugu punguza chuki zako kwa mama.. kumfananisha jpm na Mama samia ni kumkosea sana mama wa watu.. ndio kwanzaa ana siku 100 na kidogo sasa mnataka maendeleo gani ya haraka ivyo.. ipo siku mtamkubali huyu mama.


Na achaneni na RIP zenu hizo kila day, mara ohh tutamkumbuka baba, mara sijui nini!!! Hata mimi nirikua namkubali japo kuna mabaya na mazuri amefanya..


Mwishoe munakufuru kwa uyu mbaba aise.

Mwisho kabisa Mama samia ndio mzalendo, ana imani na huruma.
 
Akiongea na waandishi wa habari leo profesa Lipumba ameonyesha kushangazwa na hatua ya Rais Samia kumuachia huru mtu aliyekula njama za kukwapua zaidi ya shilingi bilion 350 za Escrow kwa kulipa shilingi bilion 26 tu, Profesa anahoji hizo pesa nyingine sasa zinakwenda wapi, na tutazipataje?

Akiongea kwa utulivu na kwa data, profesa Lipumba pamoja na kutambua baadhi ya mambo mazuri ambayo rais Samia ameyafanya ndani ya siku 100 za uongozi wake, Profesa Lipumba ameendelea kusisitiza kuwa Demokrasia ndiyio msingi wa uchumi shirikishi, kwamba huwezi kujenga uchumi shirikishi wenye kunufaisha wananchi bila demokrasia.

Profesa anasema kuwa licha ya rais Magufuli kufungia shughuli za kisiasa kwa madai hayohayo ya kukuza uchumi kwanza lakini takwimu zinaonyesha kuwa thamani yote ya pesa za uwekezaji nchini ilipungua kutoa zaidi ya dola bilion 2 mwaka 2015 hadi dola milion 800 tu mwaka 2019 tena kabla ya gonjwa la korona halijaikumba dunia, Profesa anahoji kuwa kama kuzuia shughuli halali za kisiasa ndiyo kukuza uwekezaji mbona basi uwekezaji ulishuka kipindi cha Magufuli?

Profesa akaendelea kusema kuwa uwekezaji ulishuka nchini kwa sababu Magufuli alikuwa haheshimu sheria, kitu ambacho Rais Samia amekionyesha kuwa naye atakuwa siyo mheshimu sheria baada ya kutoa tangazo la kuzuia shughuli halali za kisiasa kama zinavyoruhusiwa na sheria za nchi. Kutoheshimu sheria kunaua confidence ya wawekezaji na wenye mitaji yao!

Profesa Lipumba anasema kuna uwezekanao Wahafidhina ndani ya Chama cha Mapinduzi wanamshauri vibaya rais Samia ili asikutane na wapinzani na kumshawishi kuchukua hatua za kuvunja sheria kama hizi tunazoanza kuona akichukua.

Profesa anasema kuwa rais Samia anayo nafasi adhimu ya kukumbukwa kwa kuacha urathi (legacy) ya maana iwapo atawaachia wananchi katiba mpya, Profesa anasema kwamba kwamba hoja ya rais Samia kwamba tusubiri ajenge uchumi kwanza ndo tuzungumze habari za katiba ni ya kushangaza, ni ya kushangaza kwa sababu wao wanasema sisi tayari tuko katika uchumi wa kati, Profesa anahoji anasema au Samia anataka hadi tuwe uchumi wa juu ndo afikirie habari za katiba mpya?

Profesa Lipumba pia ametoa maoni yake pia kuhusu bajeti ya nchi, Amesema kwamba bajeti ya shilingi trilion 36 iliyosomwa bungeni haitekelezeki, anasema haoni means ambazo seriakli itaweza kupata fedha za kutosheleza bajeti hiyo

MY TAKE:
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Profesa ameongea mambo mazito sana leo na ni fact tupu!

1.Tunataka tujue ni nini hatma ya pesa za wananchi za Escrow, Habinder Seth ameachiwa , kwa nini kalipa bilion 26 tu, zilizobaki zitalipwa na nani? (By the way Profesa kasema Habinder Seth kalipa shilingi milioni 200 tu kwa hiyo hata hiyo bilioni 26 nayo ina question mark)

2. Bila Political reforms na economic reforms vikienda kwa pamoja rais Samia atashindwa kukidhi mahitaji ya wananchi, ajiandae ama kuwa dikteta kuzidi Magufuli ili kunyamazisha watu, au aonyeshe leadership kwa kuachana na wahafidhina ndani ya CCM wanaomshauri afuate njia zilizofeli za kutoheshimu sheria na kuminya haki za makundi mbali mbali ya kijamii

3. Samia kuendelea kukumbatia baraza la mawaziri la Magufuli na baadhi ya wateule wa Magufuli akidhani kuwa atawamudu kwa kuwa yeye ni rais, bila shaka ni ishara ya kuendeleza status quo, na kwa kuwa hawa ndiyo washauri wake wakubwa basi tutegemee mambo ya Kimagufulimagufuli yakirudi polepole maana hiyo ndiyo njia pekee wanayoijua ya kulinda vyeo vyao, hawawezi kumshauri awe fair kwa wapinzani wake hawa maana fairness inahitaji kujiamini na kujenga hoja za ushawishi mbele ya wananchi badala ya ujanjaujanja tuliouona katika miaka 5 iliyopita

4. Hii ya kumuachia mtu anayetuhumiwa kula njama za kuiba mabilioni ya fedha za wananchi, na ile tuliyoishuhudia kutoka kwa mtangulizi wa rais Samia ya kufunga watu kiuonevu ni Uthibitisho usioyumba kuwa wananchi tunahitaji katiba mpya ili tuweze kuondoa abuse hii ya mamlaka, kinyume cha hapo, kwa katiba hii hata ukiujenga uchumi ukawa kama Singapore bado inatoa mwanya mchwa kuutafuna kifisadi huku wakilindwa na katiba!
Hili la kigogo wa Escrow hata mimi najiuliza, analipa bilioni 26 kati ya bilioni 350 zilizobaki atalipa nani?
 
Shida ya Lipumba ni unafiki.Leo kaongea km Profesa halisi wa wa uchumi.Lakini wakimuwekea bahasha mezani tu anajitoa ufahamu wote mpaka mtu unajiuliza,Hivi huyu ndo Prof Lipumba au msukule wake?!!! Aache kubadilika badilika km kinyonga.
Umesahau na mbowe pia alilegaza paja mbele ya pesa zaowass mbona hukuwahi kushangaa
 
Hoja ya Lipumba ni ya kisiasa halafu haina mantiki.

Escrow uikiingalia kwa jicho la kiutu uzima, utajua sakata zima ni SIASA tu zinachezwa na hao kina Sethi ni mbuzi tu wa kafara.

Jiulize,

- Lipumba anaposema Sethi alikula 350b siyo kweli kwasababu hiyo ndiyo iliyokuwa pesa yote ya Escrow waliyogawana wahusika wote sasa Lipumba anasemaje pesa yote alikula Sethi?

- Maana yake kwenye hiyo 350B kuna mgawo wa kina Rugemarila na wale wa Stanbic Bank ( ambao mpaka sasa hawajulikani ni kina nani ).

Kuwakomalia kina Rugemarila na Sethi kwasababu pesa zao waligawana kwa uwazi kupitia Mkombozi bank na kutojihusisha na chochote kuhusu wale wa Stanbic inaonesha dhahiri sakata lote ni siasa tu.
Hapana sio akina Seth, alichosema huyo atalipa b.26 zilizobaki atalipa nani? Kwa maana nyingine wasakwe waliogawiwa na wote warudishe mgao, je itawezekana?
 
Akiongea na waandishi wa habari leo profesa Lipumba ameonyesha kushangazwa na hatua ya Rais Samia kumuachia huru mtu aliyekula njama za kukwapua zaidi ya shilingi bilion 350 za Escrow kwa kulipa shilingi bilion 26 tu, Profesa anahoji hizo pesa nyingine sasa zinakwenda wapi, na tutazipataje?

Akiongea kwa utulivu na kwa data, profesa Lipumba pamoja na kutambua baadhi ya mambo mazuri ambayo rais Samia ameyafanya ndani ya siku 100 za uongozi wake, Profesa Lipumba ameendelea kusisitiza kuwa Demokrasia ndiyio msingi wa uchumi shirikishi, kwamba huwezi kujenga uchumi shirikishi wenye kunufaisha wananchi bila demokrasia.

Profesa anasema kuwa licha ya rais Magufuli kufungia shughuli za kisiasa kwa madai hayohayo ya kukuza uchumi kwanza lakini takwimu zinaonyesha kuwa thamani yote ya pesa za uwekezaji nchini ilipungua kutoa zaidi ya dola bilion 2 mwaka 2015 hadi dola milion 800 tu mwaka 2019 tena kabla ya gonjwa la korona halijaikumba dunia, Profesa anahoji kuwa kama kuzuia shughuli halali za kisiasa ndiyo kukuza uwekezaji mbona basi uwekezaji ulishuka kipindi cha Magufuli?

Profesa akaendelea kusema kuwa uwekezaji ulishuka nchini kwa sababu Magufuli alikuwa haheshimu sheria, kitu ambacho Rais Samia amekionyesha kuwa naye atakuwa siyo mheshimu sheria baada ya kutoa tangazo la kuzuia shughuli halali za kisiasa kama zinavyoruhusiwa na sheria za nchi. Kutoheshimu sheria kunaua confidence ya wawekezaji na wenye mitaji yao!

Profesa Lipumba anasema kuna uwezekanao Wahafidhina ndani ya Chama cha Mapinduzi wanamshauri vibaya rais Samia ili asikutane na wapinzani na kumshawishi kuchukua hatua za kuvunja sheria kama hizi tunazoanza kuona akichukua.

Profesa anasema kuwa rais Samia anayo nafasi adhimu ya kukumbukwa kwa kuacha urathi (legacy) ya maana iwapo atawaachia wananchi katiba mpya, Profesa anasema kwamba kwamba hoja ya rais Samia kwamba tusubiri ajenge uchumi kwanza ndo tuzungumze habari za katiba ni ya kushangaza, ni ya kushangaza kwa sababu wao wanasema sisi tayari tuko katika uchumi wa kati, Profesa anahoji anasema au Samia anataka hadi tuwe uchumi wa juu ndo afikirie habari za katiba mpya?

Profesa Lipumba pia ametoa maoni yake pia kuhusu bajeti ya nchi, Amesema kwamba bajeti ya shilingi trilion 36 iliyosomwa bungeni haitekelezeki, anasema haoni means ambazo seriakli itaweza kupata fedha za kutosheleza bajeti hiyo

MY TAKE:
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Profesa ameongea mambo mazito sana leo na ni fact tupu!

1.Tunataka tujue ni nini hatma ya pesa za wananchi za Escrow, Habinder Seth ameachiwa , kwa nini kalipa bilion 26 tu, zilizobaki zitalipwa na nani? (By the way Profesa kasema Habinder Seth kalipa shilingi milioni 200 tu kwa hiyo hata hiyo bilioni 26 nayo ina question mark)

2. Bila Political reforms na economic reforms vikienda kwa pamoja rais Samia atashindwa kukidhi mahitaji ya wananchi, ajiandae ama kuwa dikteta kuzidi Magufuli ili kunyamazisha watu, au aonyeshe leadership kwa kuachana na wahafidhina ndani ya CCM wanaomshauri afuate njia zilizofeli za kutoheshimu sheria na kuminya haki za makundi mbali mbali ya kijamii

3. Samia kuendelea kukumbatia baraza la mawaziri la Magufuli na baadhi ya wateule wa Magufuli akidhani kuwa atawamudu kwa kuwa yeye ni rais, bila shaka ni ishara ya kuendeleza status quo, na kwa kuwa hawa ndiyo washauri wake wakubwa basi tutegemee mambo ya Kimagufulimagufuli yakirudi polepole maana hiyo ndiyo njia pekee wanayoijua ya kulinda vyeo vyao, hawawezi kumshauri awe fair kwa wapinzani wake hawa maana fairness inahitaji kujiamini na kujenga hoja za ushawishi mbele ya wananchi badala ya ujanjaujanja tuliouona katika miaka 5 iliyopita

4. Hii ya kumuachia mtu anayetuhumiwa kula njama za kuiba mabilioni ya fedha za wananchi, na ile tuliyoishuhudia kutoka kwa mtangulizi wa rais Samia ya kufunga watu kiuonevu ni Uthibitisho usioyumba kuwa wananchi tunahitaji katiba mpya ili tuweze kuondoa abuse hii ya mamlaka, kinyume cha hapo, kwa katiba hii hata ukiujenga uchumi ukawa kama Singapore bado inatoa mwanya mchwa kuutafuna kifisadi huku wakilindwa na katiba!
Uongozi ni kuonyesha njia iliyonyooka ambayo wengine wanaweza wasiipenda kabisa. Ukishakuwa na kiongozi anayetaka kumfurahisha kila mtu, basi elewa kuwa hajui ni njia ipi anataka kuwaongoza watu wake.
 
Bora hizo 26B kuliko kumfunga tukakosa hata hicho kidogo, ESCROW kuna akina JK huko ndani ndiyo maana hakuna kesi zaidi ya utapeli tu.
 
Lipumba alikataa uhuni wa Seif

Sitaki kumtetea Lipumba hivyo wanavyomuona kuwa ni mnafki ila nashangaa kwamba kwanini na wengine pia waliyofanyaga unafki ila hawakuwahi kuitwa wanafki mpaka leo na bado wanaendelea kuaminiwa ila kwa Lipumba ni tofauti? 2015 kulifanyika unafki mkubwa sana watu walishuhudia kitu ambacho hawakuwahi kufikiri kama ingewezekana kufanyika ila watu walijilazimisha kuwaelewa Chadema kwa walichokifanya hawakuwaita wanafki ila Lipumba ndio kabaki kuitwa mnafki.
 
hoja ya Lipumba dhaifu mno

ukituhumiwa kwa kosa la kula njama za kuiba kuku wa Rashidi ina maana mlijipanga lakini kuku hakuibiwa. Kuku angeibiwa ungetuhumiwa kuiba kuku.

huwezi kuambiwa sasa rudisha kuku wa Rashidi wakati tangia hapo kuku anae mwenyewe Rashidi.
Sasa mkuu kama hakukuwa na "financial loss" inakuwaje wamdai kiasi kikubwa hivyo.
 
Hivi jamani kwanza tusahihishe kiswahili chetu na maana ya maneno tunayotumia. Huyu mtu anatuhumiwa kuiba au kula njama za kuiba? Kula njama haimaanishi kuwa alifanikiwa kuiba.
 
Kwenye suala la ESCROW ukitaka kusimamia haki kwa asilimia zote vigogo wa CCM na baadhi ya viongozi wa dini hakuna hata mmoja atakayesalimika, Magufuli mwenyewe pamoja na umwamba wake kwenye suala la ESCROW aliufyata mwenyewe zaidi ya kuishia kusema kuwa tuwaache wapumnzike wametufanyia mengi, yaani mengi ni pamoja na kutupiga kwenye ESCROW.
 
Sitaki kumtetea Lipumba hivyo wanavyomuona kuwa ni mnafki ila nashangaa kwamba kwanini na wengine pia waliyofanyaga unafki ila hawakuwahi kuitwa wanafki mpaka leo na bado wanaendelea kuaminiwa ila kwa Lipumba ni tofauti? 2015 kulifanyika unafki mkubwa sana watu walishuhudia kitu ambacho hawakuwahi kufikiri kama ingewezekana kufanyika ila watu walijilazimisha kuwaelewa Chadema kwa walichokifanya hawakuwaita wanafki ila Lipumba ndio kabaki kuitwa mnafki.
Achana na mambo ya chadema maana hayo maufisadi yote yalifanya ccm ikiwa madarakani,polisi wenu,takukuru ya kwenu,mahakama zenu na Dpp wenu.aya tunaomba matokeo ya kesi za ufisadi mlizofungua na hukumu zake.
 
Achana na mambo ya chadema maana hayo maufisadi yote yalifanya ccm ikiwa madarakani,polisi wenu,takukuru ya kwenu,mahakama zenu na Dpp wenu.aya tunaomba matokeo ya kesi za ufisadi mlizofungua na hukumu zake.
Kwanini niachane na mambo ya chadema Ni kwamba hutaki kujadili makosa ya chadema au vp?
 
Akiongea na waandishi wa habari leo profesa Lipumba ameonyesha kushangazwa na hatua ya Rais Samia kumuachia huru mtu aliyekula njama za kukwapua zaidi ya shilingi bilion 350 za Escrow kwa kulipa shilingi bilion 26 tu, Profesa anahoji hizo pesa nyingine sasa zinakwenda wapi, na tutazipataje?

Akiongea kwa utulivu na kwa data, profesa Lipumba pamoja na kutambua baadhi ya mambo mazuri ambayo rais Samia ameyafanya ndani ya siku 100 za uongozi wake, Profesa Lipumba ameendelea kusisitiza kuwa Demokrasia ndiyio msingi wa uchumi shirikishi, kwamba huwezi kujenga uchumi shirikishi wenye kunufaisha wananchi bila demokrasia.

Profesa anasema kuwa licha ya rais Magufuli kufungia shughuli za kisiasa kwa madai hayohayo ya kukuza uchumi kwanza lakini takwimu zinaonyesha kuwa thamani yote ya pesa za uwekezaji nchini ilipungua kutoa zaidi ya dola bilion 2 mwaka 2015 hadi dola milion 800 tu mwaka 2019 tena kabla ya gonjwa la korona halijaikumba dunia, Profesa anahoji kuwa kama kuzuia shughuli halali za kisiasa ndiyo kukuza uwekezaji mbona basi uwekezaji ulishuka kipindi cha Magufuli?

Profesa akaendelea kusema kuwa uwekezaji ulishuka nchini kwa sababu Magufuli alikuwa haheshimu sheria, kitu ambacho Rais Samia amekionyesha kuwa naye atakuwa siyo mheshimu sheria baada ya kutoa tangazo la kuzuia shughuli halali za kisiasa kama zinavyoruhusiwa na sheria za nchi. Kutoheshimu sheria kunaua confidence ya wawekezaji na wenye mitaji yao!

Profesa Lipumba anasema kuna uwezekanao Wahafidhina ndani ya Chama cha Mapinduzi wanamshauri vibaya rais Samia ili asikutane na wapinzani na kumshawishi kuchukua hatua za kuvunja sheria kama hizi tunazoanza kuona akichukua.

Profesa anasema kuwa rais Samia anayo nafasi adhimu ya kukumbukwa kwa kuacha urathi (legacy) ya maana iwapo atawaachia wananchi katiba mpya, Profesa anasema kwamba kwamba hoja ya rais Samia kwamba tusubiri ajenge uchumi kwanza ndo tuzungumze habari za katiba ni ya kushangaza, ni ya kushangaza kwa sababu wao wanasema sisi tayari tuko katika uchumi wa kati, Profesa anahoji anasema au Samia anataka hadi tuwe uchumi wa juu ndo afikirie habari za katiba mpya?

Profesa Lipumba pia ametoa maoni yake pia kuhusu bajeti ya nchi, Amesema kwamba bajeti ya shilingi trilion 36 iliyosomwa bungeni haitekelezeki, anasema haoni means ambazo seriakli itaweza kupata fedha za kutosheleza bajeti hiyo

MY TAKE:
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Profesa ameongea mambo mazito sana leo na ni fact tupu!

1.Tunataka tujue ni nini hatma ya pesa za wananchi za Escrow, Habinder Seth ameachiwa , kwa nini kalipa bilion 26 tu, zilizobaki zitalipwa na nani? (By the way Profesa kasema Habinder Seth kalipa shilingi milioni 200 tu kwa hiyo hata hiyo bilioni 26 nayo ina question mark)

2. Bila Political reforms na economic reforms vikienda kwa pamoja rais Samia atashindwa kukidhi mahitaji ya wananchi, ajiandae ama kuwa dikteta kuzidi Magufuli ili kunyamazisha watu, au aonyeshe leadership kwa kuachana na wahafidhina ndani ya CCM wanaomshauri afuate njia zilizofeli za kutoheshimu sheria na kuminya haki za makundi mbali mbali ya kijamii

3. Samia kuendelea kukumbatia baraza la mawaziri la Magufuli na baadhi ya wateule wa Magufuli akidhani kuwa atawamudu kwa kuwa yeye ni rais, bila shaka ni ishara ya kuendeleza status quo, na kwa kuwa hawa ndiyo washauri wake wakubwa basi tutegemee mambo ya Kimagufulimagufuli yakirudi polepole maana hiyo ndiyo njia pekee wanayoijua ya kulinda vyeo vyao, hawawezi kumshauri awe fair kwa wapinzani wake hawa maana fairness inahitaji kujiamini na kujenga hoja za ushawishi mbele ya wananchi badala ya ujanjaujanja tuliouona katika miaka 5 iliyopita

4. Hii ya kumuachia mtu anayetuhumiwa kula njama za kuiba mabilioni ya fedha za wananchi, na ile tuliyoishuhudia kutoka kwa mtangulizi wa rais Samia ya kufunga watu kiuonevu ni Uthibitisho usioyumba kuwa wananchi tunahitaji katiba mpya ili tuweze kuondoa abuse hii ya mamlaka, kinyume cha hapo, kwa katiba hii hata ukiujenga uchumi ukawa kama Singapore bado inatoa mwanya mchwa kuutafuna kifisadi huku wakilindwa na katiba!
Anashangaa nini sasa hajui ikulu iko Msoga?
Tudai tu Katiba mpya hakuna namna tena...enough is enough!
 
Hapana sio akina Seth, alichosema huyo atalipa b.26 zilizobaki atalipa nani? Kwa maana nyingine wasakwe waliogawiwa na wote warudishe mgao, je itawezekana?
Ninavyojua Singasinga dhamana yake ni mitambo mpaka akimaliza deni.

Fact ni kwamba siyo 350B yote ilikuwa ya TANESCO.
 
Rais SSS shikilia hapohapo! Kenge ametoka shimoni mchana kweupee baada ya njaa kutamalaki. Enzi za mwendazake hili jamaa lilikuwa jeuri alipokuwa anakula meza moja na JPM.
 
Rais SSH shikilia hapohapo. Kenge moja ametoka shimoni mchana kweupee baada njaa kuwa kali. Hili lipropesa lilikuwa likisifu mambo yote ya hayati kwa sababu alikuwa akila naye meza moja.
 
Sasa mkuu kama hakukuwa na "financial loss" inakuwaje wamdai kiasi kikubwa hivyo.
Fines

adhabu ya kosa la kula njama

hakuna hela iliyoliwa mazima

bali hela ililiwa njama

angeiba angeshtakiwa kuiba, sio kula njama
 
Prof baregu (hayati)

Alimfata lipumba nyumbani kwake akamuuliza profesa kulikoni ,nimerudi cuf naona kunawatu(maalim seif) ,anataka kuuvunja muungano..



Lipumba prof
 
Back
Top Bottom