Profesa Lipumba ashangazwa na Rais Samia kumuachia mtu aliyekula njama katika wizi wa shilingi zaidi ya bilion 300 za Escrow kwa kutoa bilion 26 tu

Mimi nashangaa watu humu wanamuona Lipumba ni mnafki na kigeugeu lakini sioni sifa hizo kupewa Lissu au Mbowe kwa kigeugeu cha kumpa fomu ya kugombea urais kwenye chama mtu ambaye miaka yote wamekuwa wakimtambua kama fisadi, na walishatoaga kauli kuhusu huyo mtu ambazo zinapingana na walichokuja kukifanya 2015.

Pamoja na yote hayo ila hukuti hao watu kuitwa wanafki,binafsi nashindwa kuelewa.
 
Mimi nashangaa watu humu wanamuona Lipumba ni mnafki na kigeugeu lakini sioni sifa hizo kupewa Lissu au Mbowe kwa kigeugeu cha kumpa fomu ya kugombea urais kwenye chama mtu ambaye miaka yote wamekuwa wakimtambua kama fisadi, na walishatoaga kauli kuhusu huyo mtu ambazo zinapingana na walichokuja kukifanya 2015.

Pamoja na yote hayo ila hukuti hao watu kuitwa wanafki,binafsi nashindwa kuelewa.
Lipumba alikataa uhuni wa Seif
 
Wanaomlaumu Lipumba kupambana na Maalimu Seif ndani ya CUF hawamjui vizuri Maalim. Maalim ndiye alitemsaliti Jumbe, na Maalim ndiye aliyeuza ramani kwa kukubali kuingia ndani ya Serikali ya Hussein Mwinyi licha ya Mauaji na wizi wa kutisha wa kura ambao CCM waliufanya mwaka jana.

Lipumba aliamua kugangamala bdani ya CUF baada ya kukasirishwa na kitendo cha Maalimu kuamua kumuunga mkono Lowasa akishirikiana na Juma Duni hulu akimbypass yeye kama mwenyekiti wa chama. Hiyo ni dharau na Lipumba aliamua kukunjua makucha ili apewe heshima yake!.
Unajua maana ya kitu kinaitwa maridhiano....
au ww ni mtu wa visasi tu....
 
Prof Lipumba anatakiwa awashauri waanasheria wa serikali kupeleka ushahidi unaothibitisha kuwa Habinger Seth Ni mwizi wa pesa za escrow unless ni uonevu na dhuluma ya haki za kibinadamu kumuweka mtu Mahabusu miaka zaidi ya mitatu eti mnatafuta ushahidi.
Tunakwama wapi?

Mama Samia alisema kesi zisizokuwa na ushahidi Ni kufutilia mbali Kwasababu ndizo zinazoleta chuki katika jamii
 
3. Samia kuendelea kukumbatia baraza la mawaziri la Magufuli na baadhi ya wateule wa Magufuli akidhani kuwa atawamudu kwa kuwa yeye ni rais, bila shaka ni ishara ya kuendeleza status quo, na kwa kuwa hawa ndiyo washauri wake wakubwa basi tutegemee mambo ya Kimagufulimagufuli yakirudi polepole maana hiyo ndiyo njia pekee wanayoijua ya kulinda vyeo vyao, hawawezi kumshauri awe fair kwa wapinzani wake hawa maana fairness inahitaji kujiamini na kujenga hoja za ushawishi mbele ya wananchi badala ya ujanjaujanja tuliouona katika miaka 5 iliyopita
Kweli kabisa, Angalia yule anamshauri rais eti viwanda vya nyungu vifichwe jeshini!, mwingine anamshauri Mama eti madeni ya mifuko ya jamii yageuzwe kuwa hati fungani na eti hiyo inakwenda kumaliza shida ya wastaafu kutolipwa kwa kuwa serikali imekopa fedha zao.
Na hao wengine eti katiba mpya isubiri uchumi ukue, vijana wapate ajira - sijui lini. Hawajui kuwa kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya democrasia na kukua kwa uchumi. Wengine eti katiba mpya si ilani ya CCM na haina bajeti - wanasahau kuwa hata uwanja wa ndege msalato hauna bajeti
 
Tangu alipowavuruga kwa kujiudhuru akaja kwa mabavu ya msajili wa vyama,hata aongee point vipi.Huwa namuunga mkono msukuma ambaye husema wasomi wanatuchanganya
 
Akiongea na waandishi wa habari leo profesa Lipumba ameonyesha kushangazwa na hatua ya Rais Samia kumuachia huru mtu aliyekula njama za kukwapua zaidi ya shilingi bilion 350 za Escrow kwa kulipa shilingi bilion 26 tu, Profesa anahoji hizo pesa nyingine sasa zinakwenda wapi, na tutazipataje?

Akiongea kwa utulivu na kwa data, profesa Lipumba pamoja na kutambua baadhi ya mambo mazuri ambayo rais Samia ameyafanya ndani ya siku 100 za uongozi wake, Profesa Lipumba ameendelea kusisitiza kuwa Demokrasia ndiyio msingi wa uchumi shirikishi, kwamba huwezi kujenga uchumi shirikishi wenye kunufaisha wananchi bila demokrasia.

Profesa anasema kuwa licha ya rais Magufuli kufungia shughuli za kisiasa kwa madai hayohayo ya kukuza uchumi kwanza lakini takwimu zinaonyesha kuwa thamani yote ya pesa za uwekezaji nchini ilipungua kutoa zaidi ya dola bilion 2 mwaka 2015 hadi dola milion 800 tu mwaka 2019 tena kabla ya gonjwa la korona halijaikumba dunia, Profesa anahoji kuwa kama kuzuia shughuli halali za kisiasa ndiyo kukuza uwekezaji mbona basi uwekezaji ulishuka kipindi cha Magufuli?

Profesa akaendelea kusema kuwa uwekezaji ulishuka nchini kwa sababu Magufuli alikuwa haheshimu sheria, kitu ambacho Rais Samia amekionyesha kuwa naye atakuwa siyo mheshimu sheria baada ya kutoa tangazo la kuzuia shughuli halali za kisiasa kama zinavyoruhusiwa na sheria za nchi. Kutoheshimu sheria kunaua confidence ya wawekezaji na wenye mitaji yao!

Profesa Lipumba anasema kuna uwezekanao Wahafidhina ndani ya Chama cha Mapinduzi wanamshauri vibaya rais Samia ili asikutane na wapinzani na kumshawishi kuchukua hatua za kuvunja sheria kama hizi tunazoanza kuona akichukua.

Profesa anasema kuwa rais Samia anayo nafasi adhimu ya kukumbukwa kwa kuacha urathi (legacy) ya maana iwapo atawaachia wananchi katiba mpya, Profesa anasema kwamba kwamba hoja ya rais Samia kwamba tusubiri ajenge uchumi kwanza ndo tuzungumze habari za katiba ni ya kushangaza, ni ya kushangaza kwa sababu wao wanasema sisi tayari tuko katika uchumi wa kati, Profesa anahoji anasema au Samia anataka hadi tuwe uchumi wa juu ndo afikirie habari za katiba mpya?

Profesa Lipumba pia ametoa maoni yake pia kuhusu bajeti ya nchi, Amesema kwamba bajeti ya shilingi trilion 36 iliyosomwa bungeni haitekelezeki, anasema haoni means ambazo seriakli itaweza kupata fedha za kutosheleza bajeti hiyo

MY TAKE:
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Profesa ameongea mambo mazito sana leo na ni fact tupu!

1.Tunataka tujue ni nini hatma ya pesa za wananchi za Escrow, Habinder Seth ameachiwa , kwa nini kalipa bilion 26 tu, zilizobaki zitalipwa na nani? (By the way Profesa kasema Habinder Seth kalipa shilingi milioni 200 tu kwa hiyo hata hiyo bilioni 26 nayo ina question mark)

2. Bila Political reforms na economic reforms vikienda kwa pamoja rais Samia atashindwa kukidhi mahitaji ya wananchi, ajiandae ama kuwa dikteta kuzidi Magufuli ili kunyamazisha watu, au aonyeshe leadership kwa kuachana na wahafidhina ndani ya CCM wanaomshauri afuate njia zilizofeli za kutoheshimu sheria na kuminya haki za makundi mbali mbali ya kijamii

3. Samia kuendelea kukumbatia baraza la mawaziri la Magufuli na baadhi ya wateule wa Magufuli akidhani kuwa atawamudu kwa kuwa yeye ni rais, bila shaka ni ishara ya kuendeleza status quo, na kwa kuwa hawa ndiyo washauri wake wakubwa basi tutegemee mambo ya Kimagufulimagufuli yakirudi polepole maana hiyo ndiyo njia pekee wanayoijua ya kulinda vyeo vyao, hawawezi kumshauri awe fair kwa wapinzani wake hawa maana fairness inahitaji kujiamini na kujenga hoja za ushawishi mbele ya wananchi badala ya ujanjaujanja tuliouona katika miaka 5 iliyopita

4. Hii ya kumuachia mtu anayetuhumiwa kula njama za kuiba mabilioni ya fedha za wananchi, na ile tuliyoishuhudia kutoka kwa mtangulizi wa rais Samia ya kufunga watu kiuonevu ni Uthibitisho usioyumba kuwa wananchi tunahitaji katiba mpya ili tuweze kuondoa abuse hii ya mamlaka, kinyume cha hapo, kwa katiba hii hata ukiujenga uchumi ukawa kama Singapore bado inatoa mwanya mchwa kuutafuna kifisadi huku wakilindwa na katiba!
profesa njaa tuu huyo hana lolote, zile bilioni tatu alizopewa na jakaya akasema anaacha siasa, zilipo karibia kukata na kuona upande wa znzbar cuf inakaribia kushinda akakimbilia zanzibar kuunga cuf mkono na akarudi tena kwenye siasa.

Huyu profesa ccm walimtumia sana, kibaraka wa ccm, huyu wa kupuuzwa tuu anatafuta ugali kwa mama. Yake hayaoni anaona yawenzake tuu.
 
Prof Lipumba anatakiwa awashauri waanasheria wa serikali kupeleka ushahidi unaothibitisha kuwa Habinger Seth Ni mwizi wa pesa za escrow unless ni uonevu na dhuluma ya haki za kibinadamu kumuweka mtu Mahabusu miaka zaidi ya mitatu eti mnatafuta ushahidi.
Tunakwama wapi?

Mama Samia alisema kesi zisizokuwa na ushahidi Ni kufutilia mbali Kwasababu ndizo zinazoleta chuki katika jamii
Uko sawa, ila kama alilipa 26bn zilikuwa za nini?
 
Kwanza kabisa fedha za escrow sio za wananchi pesa ya wananchi ni kodi tu...kwa hiyo sio kweli kuwa bill 300 zote ni za wananchi
 
Pamoja na maneno matamu ya Profesa Lipumba, naomba kumuuliza Prof. mbona hatukumuona akiyasema haya kumshauri Bwana Magufuli? PILI, naomba kujua wakati Prof. anakipokea chama chake kwa kuwapora wananchi na kujimilikisha, kilikuwa na hali gani?

Wabunge wangapi? na sasa chama hicho kipo wapi? Naomba Prof. anijuze kabla ya kutoka nje kuhangaika na kibanzi kilicho kakika macho ya wenzake, anatoaje maboriti yaliyo katika macho yake?
Umetoka nje ya maada
 
Ajabu eti Chadema wanafurahia na kushangilia akiachiwa Singa singa wa escrow.2
Walichoshauri ni suala la upelelez umalizike hukumu itoke na sio kuwekwa mahabusu tu, je vp waliobeba jala kweny sandarusi? Ni bora kuliko wanaoshangilia singa kua uraiani?
 
Back
Top Bottom