CUF Habari
JF-Expert Member
- Dec 12, 2019
- 239
- 234
USHETU, SHINYANGA.
Nchi yetu imejaa ufisadi, ubinafsi, migawanyiko, kuumizana, ubaguzi,
kutokuaminiana, chuki, kukata tamaa na huzuni. Haya ni majerahay anayohitaji kutibiwa na kuwarejeshea wananchi matumaini.
Tumefikia hapat ulipo kutokana na Tanzania kukosa taasisi imara za kusimamia uendeshajiw ake. Taasisi zilizoko uimara wake ni wa kinadharia kuliko wa uhalisia.
Katika mazimgira haya mustakabali wa nchi umekuwa ukitegemea zaidi haiiba na matakwa ya rais aliyeko madarakani kuliko taratibu za kitaasisi.
CUF inataka nchi iwe na taasisi imara zinazounda mfumo madhubuti ambaou tahakikisha kuwa nchi iko salama bila kujali ni chama gani kiko kwenyen adaraka.
Kuunda mfumo huu kunahitaji nguvu ya pamoja na ushirikishwaji wa kila Mtanzania. Kwa sababu hii CUF inapendekeza serikali ya umoja wa kitaifa.
Serikali hii jumuishi itakuwa na jukumu la kujenga mfumo unaohitajika.
Serikali ya Umoja wa Kitaifa chini ya CUF itaweka misingi ya kuhakikisha kuwa taifa linakuwa na Demokrasia ya kweli.
Serikali ya umoja wa kitaifa itakamilisha mchakato wa kupata katiba mpya yenye misingi imara ya demokrasia na utawala bora.
Katiba ambayo pamoja na mambo mengine itatenganisha kikamilifu mamlaka na nguvu za mihimili mbalimbali,italinda misingi ya ushindani wa kisiasa, itapanua na kukuza haki za kiraia, na itahakikisha uwepo wa uhuru wa kutosha wa vyombo vya habari na fursa yak ujieleza.
Tunahitaji kuwa na katiba nzuri inayompa kila Mtanzania uhuru wa kweli wak uchagua na au kuchaguliwa. Tunahitaji kuwa na Muungano wa Watanganyika na Wazanzibari usio na mashaka ndani yake kwa pande zote mbili.
Tunahitaji Umoja wa Kitaifa wa kweli ambapo ubaguzi wa aina yoyote iwe ni wa jinsia, rangi, dini au ulemavu utakuwa ni jinai inayoadhibiwa kwamujibu wa sheria.
Aidha tunahitaji kuwa na katiba inayojilinda isivunjwe na wanasiasa walioko madarakani kwa ajili ya maslahi yao binafsi na maslahi yam akundi wanayoyashabikia.
Katiba ya sasa haikidhi vigezo vinavyohitajika ili kuchochea maendeleo ya demokrasia nchini mwetu.
Chini ya Sera za HAKI SAWA NA FURAHA KWA WOTE, serikali ya umoja wa kitaifa chini ya CUF itaandaa utaratibu unaofaa wa kupata Katiba Mpya ya wananchi.