Profesa Kabudi: Nilitumwa kazi Canada nikasumbuliwa sana. Niliandika barua ya kujiuzulu lakini kabla sijaipeleka kwa Rais nikanyan'ganywa

Kwahiyo kule canada kumbe tulipigwa? Siyo kama tulivyoaminishwa kuhusu makinikia

Sent using Jamii Forums mobile app
Wakati mwingine muwe mnafatilia hotuba ili angalau wewe mwenyewe ujue nini kilisemwa kuepusha kuwasikiliza watu ambao wanaleta taarifa kwa namna yao wanayo jua wenyewe, watawapoteza hawa.
 
Hiyo barua alikua anaandika kwa kumia peni na karatasi au aliiandika kupitia kwenye komputa ? Hebu tuanzie napo. Kama kwenye computer copy itakuwepo
 
When Kabudi addresses an audience you’d be forgiven to assume he was giving a church sermon to a Christian audience rather than speaking as a national minister.

Who recommends these bozzos to senior posts.

Hakuna mtu mwenye akili zake timamu atamtuma Kabudi kufanya contract negotiation ni serikari ya Tanzania tu.
 
Kweli sikio la kufa halisikii dawa, yaani ni jana tu Lugola kaaibishwa mbele ya kadamnasi lkn bado huyo Kabundi hajifunzi tu?
Katika hafla inayoendelea sasa hivi Ikulu ya Utiaji saini kati ya Tanzania na Barrick Gold, Profesa kutoka Jalalani akiwa anatoa hotuba yake bila tashwishwi amedai kwamba alitumwa kazi na Rais Magufuli lakini kazi ile hakufanikiwa na ikawa fedhaha kubwa kwake kwa kutumwa kazi na Rais na kushindwa kuitekeleza, hivyo alichukua maamuzi ya kumwandikia Rais barua ya kujiuzulu lakini kabla hajaifikisha sehemu husika akawa amepokonywa.

Nanukuu

Katika kujadili mikataba 9 itakayosainiwa leo, hicho kipindi kilikuwa kigumu. Hawakuwa hawa, walikuwa wenzao hawapo hapa. Sipendi kuwataja majina ila hawakutaka mikataba hii isainiwe na tufanikiwe. Kila tulipokutana na kukubaliana kesho yake walibadilika


Ilifika mahali Rais nilitaka kuingiwa na dhambi ya kukata tamaa na vitimbi hivyo vilishia kwa wao wenyewe kufukuzana kazi. Leo nataka kumshukuru Luteni Kanali Mstaafu Richard William

Tulipofika kukata tamaa, Rais nilikuwa nimendika barua ya kujiuzulu kuja kwako. Kwamba kazi uliyonipa imenishinda. Aibu hii na fedheha hii nitaibeba. Barua hiyo sikuileta maana Casmir Simba Kyuke alininyang'anya na kuichana

Nilisema sijawahi kutumwa kazi na Mkuu wangu wa nchi nikashindwa, ila sasa hawa watu hawataki. Rais unaniuliza mnakwendaje, mbona nasikia hamuendelei! Namjibu tunaendelea huku najua hatuendelei.Ndipo nilipowapigia Maaskofu wangu wa Anglikana.
FB_IMG_1579773272376.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swali fikirishi je aliandika barua wakiwa wote hadi kunyang'anywa hiyo barua ila kuongea nyuma ya mikamera kuna raha yake hata ukijitoa ufahamu kamera zina ona tu
Alimpa kama external supervisor ili aipitie kabla ya ku-publish ikulu.. alifikiri ni "pepa"
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom