Profesa Kabudi: Katiba tuliyonayo ni madhubuti ndio maana imetuvusha tulipopata matatizo!

Mlishasema hamuutambui uchaguzi mkuu uliopita. Kwa hiyo hamulitambui wala kulikubali bunge lililopo. Maana yake hata rais aliyepo madarakani kutokana na uchaguzi huo hamumutambui wala hamumukubali.

Sasa mbona munahangaika kumuomba rais kumuomba katiba mpya? Atawapaje hiyo katiba mpya wakati yeye siyo rais (kwa akili yenu) maana hamumutambui kama yeye ni rais, amiri jeshi mkuu na mkuu wa nchi? Si muendelee tu kutunga hiyo katiba yenu mpya peke yenu na tuone mtakachokipata. Kelele za nini?

Mungalikuwa na akili sasa hivi mungekuwa mmekazana kuweka mikakati ya kushika dola ifikapo 2025 (kwa katiba hii hii - Lowassa alibakiza kidogo tu kuwavusha uchaguzi wa 2015). Baada ya kuchukua dola ndipo sasa mungalileta hiyo katiba yenu mpya munayoitamani. It is that simple but not now when you are nobody.
Usinilishe maneno mdomoni. Nani kasema hamtambui Rais? Nimesema wabunge walioko hawana sifa za kuitwa wawakilishi wa wananchi.

Mtu anashinda kura ya maoni anaachwa anachukuliwa mwingine kwenda kuomba kura! Na mbaya zaidi, mmoja wa wagombea wa Urais ndiye anateua Mkuu wa Tume ya Uchaguzi na watendaji wake! Yaani timu moja ichague refa na linesmen wanaowapenda wao, na wawambie wasithubutu kuruhusu timu nyingine kufunga goli, kisha useme wamepata ushindi halali?

Wewe ulimsikia Rais aliyepita akiwaambia Wakurugenzi kwamba hawezi kuwateua yeye kisha wamtangaze mtu asiye wa chama chake kushinda. Sasa mbunge anayechaguliwa kihivyo ni mwakilishi wa wananchi? You make me laugh.

Na hao wabunge 19 walioingizwa kwa hila na Spika ni wawakilishi wa wananchi wepi!

You can cheat some of the people some of the time but you cannot cheat all the people all the time. CCM iache sasa mbinu za kudanganya kwani tunaelewa ukweli na haki vikoje.

I have not given up on Mama Samia. Nadhani anasukumwa tu na watu wanaotaka kuhodhi madaraka, ila yeye si thulumati. Tim will tell.
 
Mtu mnafiki kama Kabudi, ni useless kwa Taifa. Watu wanafiki na wachumia tumbo wa namna hii, hawastahili kupewa heshima katika jamii, zaidi ya ule utu wamwanadamu asiye na msimamo wowote.
 
Usinilishe maneno mdomoni. Nani kasema hamtambui Rais? Nimesema wabunge walioko hawana sifa za kuitwa wawakilishi wa wananchi.

Mtu anashinda kura ya maoni anaachwa anachukuliwa mwingine kwenda kuomba kura! Na mbaya zaidi, mmoja wa wagombea wa Urais ndiye anateua Mkuu wa Tume ya Uchaguzi na watendaji wake! Yaani timu moja ichague refa na linesmen wanaowapenda wao, na wawambie wasithubutu kuruhusu timu nyingine kufunga goli, kisha useme wamepata ushindi halali?

Wewe ulimsikia Rais aliyepita akiwaambia Wakurugenzi kwamba hawezi kuwateua yeye kisha wamtangaze mtu asiye wa chama chake kushinda. Sasa mbunge anayechaguliwa kihivyo ni mwakilishi wa wananchi? You make me laugh.

Na hao wabunge 19 walioingizwa kwa hila na Spika ni wawakilishi wa wananchi wepi!

You can cheat some of the people some of the time but you cannot cheat all the people all the time. CCM iache sasa mbinu za kudanganya kwani tunaelewa ukweli na haki vikoje.

I have not given up on Mama Samia. Nadhani anasukumwa tu na watu wanaotaka kuhodhi madaraka, ila yeye si thulumati. Tim will tell.
Sikulishi maneno mdomoni. Ninaongea logic ya msimamo wenu. Kwamba huo uchaguzi mkuu wa 2020 mnauita ulikuwa uchafuzi mkuu na kwa hiyo yote yaliyotokana na uchafuzi huo mkuu hamuyatambui. Na yaliyotokana na huo mnaouita uchafuzi mkuu ni pamoja na hao wabunge uliowataja wakiwamo hao 19 na pia rais wa Tanzania. That is the logic of your position.

Kuyapinga matokeo ya uchaguzi huo mahakamani kwa mjibu wa sheria zetu, nayo mlikataa kwa kutokuwa na imani na mahakama zetu kwa kuwa majaji wanateuliwa na rais. Baraza kuu la chama chenu kuitishwa kusikiliza na kuamua rufaa ya hao 19 kwa mjibu wa katiba yenu, nayo mmekataa kwa kisingizio cha kuwa 'it is a waste of time'.

Hivyo logically misimamo yenu inashindwa kueleweka kwa watu makini.
 
Sikulishi maneno mdomoni. Ninaongea logic ya msimamo wenu. Kwamba huo uchaguzi mkuu wa 2020 mnauita ulikuwa uchafuzi mkuu na kwa hiyo yote yaliyotokana na uchafuzi huo mkuu hamuyatambui. Na yaliyotokana na huo mnaouita uchafuzi mkuu ni pamoja na hao wabunge uliowataja wakiwamo hao 19 na pia rais wa Tanzania. That is the logic of your position.

Kuyapinga matokeo ya uchaguzi huo mahakamani kwa mjibu wa sheria zetu, nayo mlikataa kwa kutokuwa na imani na mahakama zetu kwa kuwa majaji wanateuliwa na rais. Baraza kuu la chama chenu kuitishwa kusikiliza na kuamua rufaa ya hao 19 kwa mjibu wa katiba yenu, nayo mmekataa kwa kisingizio cha kuwa 'it is a waste of time'.

Hivyo logically misimamo yenu inashindwa kueleweka kwa watu makini.
Unataja msimamo "WENU". Wa mimi na nani? Si mwanachama wa chama chochote mimi.

Mtu ukisema uchaguzi umekuwa wa kuiba kura haina maana kwamba humtambui aliyetangazwa kuwa Rais. Likatiba lenyewe linasema akishatangazwa basi hakuna ruhusa ya kudai mahakamani kwamba hakuchaguliwa kihalali. Sasa hivi sidhani kama kuna mtu au chama ambacho hakimtambui Mama kwamba ni Rais wa Tanzania. Dr Mwinyi pia ni Rais wa Zanzibar. Sikubali kwamba walichaguliwa na wananchi kushika nafasi hizo lakini natambua walitangazwa kuzishika.

Stop making wild assumptions. I am not a member of Chadema.
 
Kama katiba iliyopo ya sasa ni imara, je, ilikuwaje Kabudi na tume ya jaji Warioba walizunguka nchi nzima kukusanya maoni kwa wananchi?

Waandishi wa habari wanatakiwa, wawe wanatusaidia kuwauliza wanasiasa maswali chokonozi!
 
Tatizo siyo kifo kweli! Lakini kumbuka aliyefariki ni Rais,tena ndiyo yuko Madarakani,Kama kungetokea wale wavamizi wa Mirathi ya Mama unazani saa hizi hali ingekuwaje!?

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
uwe na katiba au usiwe nayo. iwe nzuri au mbaya......wanaoweza kufanya hivyo ni jeshi. ukiwa na jeshi linaloheshimu mfumo hilo haliwezi kutokea hata kama rais na makamu wake wafe. bado litasoma katiba na liifuate. Hizi porojo za kabudi ni za kutetea tumbo tu
 
Mtu mweusi ni Kima aliechangamka.Imagine CCM wanatumia zile ndege za serikali katika shughuli zao za kila siku kana kwamba ni mali ya chama!
MMvO0.jpg
Dor0.jpg
 
Aliyekuwa mjumbe wa Tume ya katiba iliyoongozwa na Jaji Warioba na ambaye kwa sasa ni Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Kabudi amesema Katiba ya Tanzania ni madhubuti ndio maana imetuvusha tulipopata tatizo kubwa.

Nawasalimu kwa jina la JMT!
===

Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amesema Katiba ya Tanzania ni nzuri, inapaswa kuheshimiwa kwa kuwa imeivusha nchi katika kipindi kigumu.

Alisema uzuri wa Katiba na umadhubuti wake huonekana wakati wa matatizo yasiyo ya kawaida, hivyo inafaa kuheshimiwa.

Profesa Kabudi alisema mabadiliko mengi ya Katiba yalifanyika mwaka 1984, hivyo ni vyema kuendelea kuienzi kwa sasa wakati utaratibu mwingine unasubiriwa.

Kauli hiyo inakuja zikiwa zimepita takribani siku tatu tangu viongozi wa dini nchini kueleza umuhimu wa Katiba Mpya, huku Chadema kupitia kongamano maalumu lililoandaliwa na Baraza la Vijana wa chama hicho (Bavicha), likieleza umuhimu wa suala hilo juzi.

Profesa Kabudi alitoa kauli hiyo jana katika maadhimisho ya saba ya siku ya utetezi wa haki za binadamu, yaliyofanywa na asasi za kiraia nchini pamoja na uzinduzi wa utekelezaji wa mpango wa Taifa wa maendeleo wa miaka mitano wa azaki hizo.

Alisema baada ya Rais John Magufuli kufariki dunia, makamu wake (Rais Samia Suluhu Hassan) aliapishwa kushika wadhifa huo kwa matakwa ya Katiba kupitia Ibara ya 9 na sasa nchi ina Rais mtendaji mwanamke na mwenye uwezo.

“Hili lilikuwepo ndani ya Katiba, limeivusha nchi yetu katika kipindi hiki kigumu na uzuri wa Katiba na umadhubuti wake unauona wakati wa matatizo yasiyokuwa ya kawaida. Tanzania imevuka mtihani huo kwa katiba hii na tumshukuru sana Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kutuwekea misingi ambayo imetufikisha hapa, nchi nyingine za Afrika kwa hili lililotokea ni vita, dhahama na migogoro, sisi salama salimini, Samia Suluhu Hassan amepokewa vizuri na raia wote wa Jamhuri ya Muungano bila maswali,” alisema Profesa Kabudi.

Pia, alisema mbali na hayo, Katiba ya sasa imekuwa msaada mkubwa kiutendaji na inalinda haki za binadamu na utawala bora.

“(Katiba ya sasa) Inalinda haki za kiraia, kisiasa, uchumi na za kiutamaduni na ndiyo maana Serikali imeridhia kwanza Katiba yetu,” alisema.

Katika kongamano la Bavicha, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alitaka Rais Samia Suluhu Hassan kuunda Tume ya Katiba ili kusimamia mchakato wa kupata Katiba Mpya.

Mbowe alisema Watanzania wanahitaji Katiba Mpya, bora na shirikishi, huku akipendekeza makundi mbalimbali ya kijamii yashirikishwe.

Alisema hatua ya pili iwe ni kuunda Bunge Maalumu la Katiba litakalozingatia masilahi ya makundi yote.

Awali, akizindua mkutano huo, Profesa Kabudi alizitaka asasi hizo za kiraia kuacha kutegemea wahisani, bali wajitegemee kutafuta vitu vya kuwaingizia kipato pamoja na kufuata sheria za nchi wanapofanya kazi zao.

“Wakati umefika asasi za kiraia kuanza kufikiria kutafuta njia nyingine za kuziwezesha asasi hizi kifedha kuliko kuendelea kusaidiwa, siwezi kusema tuache kusaidiwa, ila tuanze kufikiria kwenda mbali,” alisema Profesa Kabudi.

“Asasi nyingi bado zinajikita katika dhana ya Serikali kama mvunjifu mkuu wa haki za binadamu na matokeo yake hazielekezi nguvu kubwa katika kupambana na uvunjifu wa haki za binadamu unaofanywa na raia au kampuni na mashirika makubwa ya kiuchumi duniani.”

Mwananchi
Supu Ina nzi
 
Kwa mila na desturi za mtu mweusi hairuhusiwi kuongea wakati unakula. Kwa sasa mzee wa jalalani anakula hawezi kuongea. Akiwa mjumbe wa tume ya katiba mpya alikuwa na akili binafsi sasa zimeondolewa na kuingiziwa za ccm
 
Back
Top Bottom