Profesa Juma Kapuya awahoji Watanzania: Mlitaka nioe Bibi?

Profesa Juma Kapuya aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Urambo Magharibi,amefunguka kuhusu ndoa yake aliyofunga Jumapili ya Februari 12 na mwanamke anayejulikana kwa jina la Mwajuma Mwiniko.

Akizungumza na Mwananchi Digital, Kapuya amesema anawashangaa watu wanaomsema kuoa mwanamke aliyemzidi umri kwani wanataka aoe mwanamke anayefanana na bibi yake?
Kapuya amesema umri hauhusiani na mapenzi, hivyo watu wakubali matokeo kwani hajamtorosha shule huyo mwanamke,wala hajavunja sheria, mila, desturi pamoja na dini.

"Unajua mimi nawashangaa sana watu wanaoshangaa mimi kuoa mwanamke niliyemzidi umri,hivi umri unahusiana nini na mapenzi? Na ukiangalia huyu mwanamke mimi sijamtorosha shule, wala sijavunja mila, desturi pamoja na dini, au watu walitaka nioe mwanamke anayefanana na bibi yangu? Nawaambia wakubali matokeo tu waache kusema sema," alisema Kapuya.

Aidha, Kapuya aliongeza kusema, "Yeye sio wa kwanza kuoa mwanamke wa umri huo mdogo chamsingi ni kukubaliana tu, na siwezi tena kuoa mwanamke mwingine kwani mke huyu ni somo tosha, sababu mke wangu wa kwanza anaishi Dar nampenda sana ,huyu ni wa pili sasa natafuta nini tena kuoa? Hapa subirini tu mtoto kutoka kwa huyu mwanamke mnayesema ana umri mdogo,"alisema Kapuya.

Hata hivyo Kapuya amesema kwa mara ya kwanza amekutana na Mwajuma Kaliua, alipokuwa anaenda kufanyia vikao na Kaliua na Urambo sio mbali.

-Mwananchi
Katika hili ninajiuliza mambo kadha
1. Ni kweli lakini haituhusu, kwani hayo ni maisha ya mtu binafsi.
2. Kapuya kama alivyosema siye wa kwanza kuona mwanamke mdogo kwa umri wake. Kwenye imani yake anaruhusiwa kwani hata mtume kati ya wake zake alikuwa na mke mdogo sana kwa umri wa kuolewa.
3. Kwa imani yake bado anatakiwa kuongeza 2 zaidi, maana ameeleza kuwa mmoja yupo Dar na huyu mwingine yuko Tabora.
Ushauri:
- Huwa tunapoteza muda mwingi kudeal na issues ambazo hazina tija kuliko kujadili mambo yasliyo na tija kwa maisha yetu.
- Kwa mfano katika hili tunanufaika na nini, kama hakuna tunachonufaika nacho mjadala huu hautuhusu bali kila mtu apate funzo kwa sehemu yake. Kwa yule anayeona hiki ni kitendo cha fedheha kwa mzee mzima kuoa mjukuu ajifunze kitu aikwepe hiyo anayoona ni aibu na fedheha.
- Yule anayeona ni sawa tu naye ajifunze kutafakari faida na hasara ya tendo hilo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Profesa Juma Kapuya aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Urambo Magharibi,amefunguka kuhusu ndoa yake aliyofunga Jumapili ya Februari 12 na mwanamke anayejulikana kwa jina la Mwajuma Mwiniko.

Akizungumza na Mwananchi Digital, Kapuya amesema anawashangaa watu wanaomsema kuoa mwanamke aliyemzidi umri kwani wanataka aoe mwanamke anayefanana na bibi yake?
Kapuya amesema umri hauhusiani na mapenzi, hivyo watu wakubali matokeo kwani hajamtorosha shule huyo mwanamke,wala hajavunja sheria, mila, desturi pamoja na dini.

"Unajua mimi nawashangaa sana watu wanaoshangaa mimi kuoa mwanamke niliyemzidi umri,hivi umri unahusiana nini na mapenzi? Na ukiangalia huyu mwanamke mimi sijamtorosha shule, wala sijavunja mila, desturi pamoja na dini, au watu walitaka nioe mwanamke anayefanana na bibi yangu? Nawaambia wakubali matokeo tu waache kusema sema," alisema Kapuya.

Aidha, Kapuya aliongeza kusema, "Yeye sio wa kwanza kuoa mwanamke wa umri huo mdogo chamsingi ni kukubaliana tu, na siwezi tena kuoa mwanamke mwingine kwani mke huyu ni somo tosha, sababu mke wangu wa kwanza anaishi Dar nampenda sana ,huyu ni wa pili sasa natafuta nini tena kuoa? Hapa subirini tu mtoto kutoka kwa huyu mwanamke mnayesema ana umri mdogo,"alisema Kapuya.

Hata hivyo Kapuya amesema kwa mara ya kwanza amekutana na Mwajuma Kaliua, alipokuwa anaenda kufanyia vikao na Kaliua na Urambo sio mbali.

-Mwananchi
Dah! Demu wa jamaa kaolewa na huyu mzee....anyway, "MwanaFA unaoa lini?" Bado niponipo kwanza.
 
Hii ya Pro.nimeipenda sana inatuonyesha ni jinsi gani kuna tatizo la waoaji kwenye jamii hivyo mabinti wanalazimika kuolewa na MTU yoyote bila kuweka vigezo zaidi ya kigezo cha kuwa mwanamume.
 
Hakuna uhusiano wowote na kuoa kwake!
Miaka ile iliyopita wakati nakua nilikuwa nikiambiwa mtu kasoma hadi kufikia ngazi ya profesa au dokta namchukulia ni mtu wa hadhi ya juu mno! Siku hizi naona kawaida sana
 
Hii ya Pro.nimeipenda sana inatuonyesha ni jinsi gani kuna tatizo la waoaji kwenye jamii hivyo mabinti wanalazimika kuolewa na MTU yoyote bila kuweka vigezo zaidi ya kigezo cha kuwa mwanamume.
Vigezo vpo, sema vinatofautiana, mf pesa , elimu, ufupi, urefu , dini , nguvu , Sura, tabia , etc, ni ngumu kujua kigezo cha mtu
 
Huyu mzee kuna kipindi alikuwa na band inaitwa Akudo impact. Sijui inaendeleaje?
 
Inashangaza sana namna hili jambo limegeuka la kisiasa wakati ni mapenzi ya wahusika.
 
kuna vitu usipofanya ukiwa mtoto utakuja fanya ukiwa mkubwa... kimsingi yupo sawa lkn sio busara kukato...ba katoto kale ka kugegedwa na mjukuu wake, huo n ufa..
mzee mzima ulikua wapi miaka yote hii leo ndo unaoa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom