TANZIA Profesa Augustine Massawe, Daktari bingwa wa Magonjwa ya Watoto afariki dunia

Lala salama baba. Tunakushukuru sana wa huduma Mungu aliyokuwa amekujalia

Uliitumia vyema karama Mungu aliyoiweka ndani yako

Mwendo umemaliza 💔💔💔

---
Daktari Bingwa wa Watoto Dr Augustine Massawe wa Furaha Medical amefariki Dunia leo Jijini Dar es Salaam. Taarifa kutoka kwa familia ni kwamba Dkt. Massawe amefariki asubuhi hii katika hospitali ya Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa siku kadhaa kwa matibabu.

Pumzika kwa amani Prof Massawe
 
Kwamba na hao wa Ulaya na maeneo mengine wanaoendelea kufa hawana akili?

Unaweza kutoa jawabu la wenye akili wanachofanya waepuke kifo? Hali ni mbaya CDC na FDA wako kwenye mijadala mizito kuhusu Booster kwa waliokwishachanjwa dozi zote, hebu tupe mbadala mkuu.
Kwani ugonjwa gani ambao hauui?Surua,kifua kikuu,ndui,pepopunda,kifaduru na kadhalika zote zina chanjo na zinaua.Kinachotakiwa kufanyika ni binadamu kutumia akili yake optimally.

Sasa hivi Corona ina chanjo na bado inaua lakini binadamu angekaa kimya bila kufanya lolote ingeua zaidi.Kinachotakiwa kufanyika ni kuongeza jitihada zaidi na wala siyo kubeza jitihada zinazoendelea.

Imani bila matendo imekufa.Binadamu wakikaa tu chini bila ya kufanya lolote na kusema kuwa Mungu ni mkubwa sana wataisha wote.Cha msingi ni kuendelea kutumia akili tulizo nazo.Hata mbuyu ulianza kama mchicha,usitegemee Corona ikamalizwa yote ndani ya siku moja.Kila kitu huhitaji muda.
 
Mlishe mwanao chakula bora usisubirie kununua antibiotics. Prof amemaliza mwendo apumzike kwa Amani.

Ametufundishia madaktari wengi sana.

Swali chokonozi wakati ule tulipokuwa tuna mtegemea Mungu kwanza na kuhimizwa hivyo na kipindi cha sasa ambapo tunahimizwa kutegemea barakoa, chanjo na akili zetu wapi misiba imekuwa mingi zaidi? Jibu mnalo nafikiri na mjisahihishe ili pengine huruma ya Mungu na Neema yake ituokoe kama Taifa.

Mungu wa Mbinguni hadhihakiwi hata mara moja. Mtavuna mlicho panda.
Ulikuwa unaishi nchi IPI? Mbona enzi za Magu watu wamekufa sana mpaka barabaran unaokota watu
 
Lala salama baba. Tunakushukuru sana wa huduma Mungu aliyokuwa amekujalia

Uliitumia vyema karama Mungu aliyoiweka ndani yako

Mwendo umemaliza 💔💔💔

---
Daktari Bingwa wa Watoto Dr Augustine Massawe wa Furaha Medical amefariki Dunia leo Jijini Dar es Salaam. Taarifa kutoka kwa familia ni kwamba Dkt. Massawe amefariki asubuhi hii katika hospitali ya Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa siku kadhaa kwa matibabu.

Very sad. Mungu afariji Familia yake.
Amesaidia Watoto wengi sana kuwatibu.
 
2005 nilipata huduma toka kwa huyu mzee pale morocco. Binti yangu aliyezaliwa tu akiwa na siku kama 6. Alikuwa akilia sana muda wote. Akipewa nyonyo ananyonya baada ya muda kidogo analia tena.
Nikampeleka pale. Sitakaa nidharau taaluma ya mtu. Hata akiwa mkuluma.
Mzee masawe akamwambia wife akamue maziwa ajazi kikombe kilikuwa pale. Kukamua kumbe mama maziwa hana na mtoto analia sababu hashibi. Nikaanza kuingia super market kununua mazuwa ya kopo. Kwa sasa ni mkubwa na yupo form two pale St marie Eugen.

Pumzika kwa amani mzee wangu Masawe.
Duh.! Ni kama mzaha hivi...R.I.P Daktari
 
Duh, Pumziko La Amani Apate.

Nimepata sana mafundisho yake kupitia TV.
 
Kwani ugonjwa gani ambao hauui?Surua,kifua kikuu,ndui,pepopunda,kifaduru na kadhalika zote zina chanjo na zinaua.Kinachotakiwa kufanyika ni binadamu kutumia akili yake optimally.

Sasa hivi Corona ina chanjo na bado inaua lakini binadamu angekaa kimya bila kufanya lolote ingeua zaidi.Kinachotakiwa kufanyika ni kuongeza jitihada zaidi na wala siyo kubeza jitihada zinazoendelea.

Imani bila matendo imekufa.Binadamu wakikaa tu chini bila ya kufanya lolote na kusema kuwa Mungu ni mkubwa sana wataisha wote.Cha msingi ni kuendelea kutumia akili tulizo nazo.Hata mbuyu ulianza kama mchicha,usitegemee Corona ikamalizwa yote ndani ya siku moja.Kila kitu huhitaji muda.

Hatujawahi kusikia watu walio uliwa na kuambukizwa na chajo hizo nyingine kwa jinsi ya na chanjo hii ya corona.

Tumeanza kusikia hii ya corona ikituulia wapendwa wetu kwa namna ya kuogofya acha wakiobanwa na matumbo ya kuhara na kukosa nguvu mwilini, kifo kiliwadip/beep baada ya kuchanjwa..
 
Mlimwita 'mjinga/nchi inaongozwa na washamba' kwa maamuzi ya kuhimiza kumtegemea Mungu kwanza na mengineyo. Ngoja tuwaone wajanja wa kutegemea akili zao na si Mungu watakapo tufikisha kama Taifa.
Mi sipo kinyume na taaluma ya mtu lakini approach ya Magufuli ya kututaka tusiipe airtime corona bali tumwangalie Mungu ni sawa na ile ya approach ya Musa jangwani kwamba atengenenze nyoka wa shaba ili wale watakaoinangalia nyoka ile watapona. Watakaokazana kutazama chini ili wasiumwe na nyoka watapukutika.

Hivi vitabu vya dini vina hekima iliyojificha. Tusipuuze. Ngoja tuone huu mziki utaishaje. Nchi yenyewe hii haina hata uwezo wa kuzuia malaria eti inahangaika na machanjo yasiyosaidia hata. Machanjo yenyewe dozi milioni moja kati ya watu milioni 60. Mnaambiwa weka tumaini lenu kwa Mungu mnasema ni ujima na ushamba. Washamba ndio wanaobaki sasa na wenye hekima wanaangamia.

RIP profesa.
 
Hatujawahi kusikia watu walio uliwa na kuambukizwa na chajo hizo nyingine kwa jinsi ya na chanjo hii ya corona.

Tumeanza kusikia hii ya corona ikituulia wapendwa wetu kwa namna ya kuogofya acha wakiobanwa na matumbo ya kuhara na kukosa nguvu mwilini, kifo kiliwadip/beep baada ya kuchanjwa..
Unaweza kuthibitisha kuwa wameuawa na chanjo ya Corona na wala siyo kwa kitu kingine chochote kile?
 
Back
Top Bottom