Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,644
- 218,092
Hiki ni kitendo kilichofanyika bila kuchelewa , hajataka kuleta longolongo ili waseme kuna mafaili yametoroshwa .
Kila la heri Profesa Assad
******
Prof. Assad:
"Hii ni taasisi na makabidhiano ya taasisi yanaenda kwa maandishi, kwa hiyo makabidhiano kwa maandishi yatafanyika Dodoma kwa sababu ndiyo kule makao makuu yetu yalipo"
"Kazi ya CAG ni kusaini ripoti lakini ripoti unachukua wajibu wa kazi ya watu wengi sana, ambao waliifanya maeneo mbalimbali hapa Tanzania, kwa hiyo nukta yangu ni kuwatazama vizuri sana watu hawa"
"Kama kuna yeyote nilimkosea kwenye utendaji wetu wa kazi basi anisamehe na mimi kuna kuna mambo alinikosea nimemsamehe."
"Baada ya hapa mimi nitafanya kazi ya kulima kwa sababu miezi 2 iliyopita nilianza kuwekeza kwenye kulima, wakinihitaji watu wa Mjini nitakuja, kuhusu changamoto ni nyingi nimepitia mnataka niseme hapa nitatia ukakasi hakuna haja ya kutia ukakasi."
"Nimepokea ofisi hii kutoka kwa Uttoh miaka mitano iliyopita naamini sikufanya uharibifu wowote mimi naamini mabadiliko yanaweza kutokea, lakini yatokee kwenye namna ilivyopangwa vizuri."
CAG Kichere :
"Kama kutakuwa na mabadiliko yatafanyika kwa umakini mkubwa ili tusiharibu mfumo wa utendaji kazi."
"Nimefanya kazi TRA najua ugumu wa kukusanya mapato, nimekuja kulinda mapato, tena nitalinda kwa wivu mkubwa sana, sitakuwa na simile kwa watu wanaotumia mapato ya Serikali vibaya."
"Kama kulikuwa na mahusiano hafifu nitaimarisha mahusiano kati ya Ofisi ya CAG na Bunge."