Profesa Assad amebeba funzo kwa viongozi vijana

Tee Bag

JF-Expert Member
Dec 21, 2013
7,200
5,553
PROF ASSAD AMEBEBA FUNZO KWA VIONGOZI VIJANA

Na Thadei Ole Mushi

Nimesoma hii tweeter kuhusu Hawa vijana kukutana na Prof Assad aliyekuwa CAG kukutana naye kwenye daladala naona Kuna funzo kwa huyu mtu.

Vijana ambao ni Viongozi waiombe Hekima ya Mungu Sana na waishi maisha ambayo baada ya kuachia nafasi zao za uongozi wataendelea kuishi katikati ya jamii bila bodyguards wala hofu.

Huyu mzee atakuwa anaishi maisha ya furaha Sana japokuwa kwa jicho la kawaida unaweza fikiria anaishi kwa shida. Ni Viongozi wachache Sana wanaomaliza muda wao wa uongozi na kuweza kuishi kwa furaha.

Wengi huishi maisha ya wasiwasi na hofu, wengi hubakia kuhesabu maovu aliyoyafanya akiwa kiongozi matokeo yake hupatwa na magonjwa ya msongo wa mawazo matokeo yake wanakufa wakiteseka Sana.

Yuda baada ya kufanya Usaliti au Ubaya kwa Yesu alitumikia mateso, mfadhaiko Hadi akaamua kujiua. BASHIRU wa Sudani, Ben Ali wa Tunisia, Mubarak wa Misri, Gagbo wa Ivory Coast na wengineo hawakuwahi kuishi kwa amani baada ya uongozi wao.

Unafikiri katika Viongozi tulionao Sasa kwa ngazi zote Nani unafikiri anaweza kuishi maisha Kama haya baada ya kustaafu?

Ole Mushi
0712702602

FB_IMG_1586066034996.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo mzee hakika anayafuata mafundisho ya dini; ni mnyenyekevu, asiependa makuu, anajishusha (hasa nikikumbuka alivyovuliwa viatu bungeni), hapendi mashindano ( kwa nafasi aliyowahi kushika sio rahisi mtu wa aina yake apande daladala).

Hakika anajua duniani tunapita, hongera kwake, ndio maana Mungu kampa akili nyingi, na pole sana kwa wote waliomfanyia vitimbi wakidhani wanamkomoa, Mungu awasamehe hawakujua walitendalo.

He is simply a class above!.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mijitu pamoja na kuendesha miV8 na kuwa na kila kitu cha kufurahisha nafsi zao bado matendo yao huzifanya nafsi zao kuwa na woga muda wote na mwisho wa siku kuishia kuwa washamba tu...

Prop Assad ni muungwana mwenye amani ya kweli kwenye nafsi yake inayomfanya kuona maisha yote ni sawa..
 
mkuu umesama ukweli ila sio sana, mtu akishakuwa kiongozi tena mwenye nafasi kubwa ni vigumu kuishi maisha ya daladala
kwa mfano tuseme makonda hata asingekuwa mjinga bado angekuwa na maadui kutokana na hiyo kazi yake, tunapaswa kutoa fikra kwamba kila mtu lazima apande daladala au ajichanganye


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna jipya hapo ,yote ni mapito tu
PROF ASSAD AMEBEBA FUNZO KWA VIONGOZI VIJANA

Na Thadei Ole Mushi

Nimesoma hii tweeter kuhusu Hawa vijana kukutana na Prof Assad aliyekuwa CAG kukutana naye kwenye daladala naona Kuna funzo kwa huyu mtu.

Vijana ambao ni Viongozi waiombe Hekima ya Mungu Sana na waishi maisha ambayo baada ya kuachia nafasi zao za uongozi wataendelea kuishi katikati ya jamii bila bodyguards wala hofu.

Huyu mzee atakuwa anaishi maisha ya furaha Sana japokuwa kwa jicho la kawaida unaweza fikiria anaishi kwa shida. Ni Viongozi wachache Sana wanaomaliza muda wao wa uongozi na kuweza kuishi kwa furaha.

Wengi huishi maisha ya wasiwasi na hofu, wengi hubakia kuhesabu maovu aliyoyafanya akiwa kiongozi matokeo yake hupatwa na magonjwa ya msongo wa mawazo matokeo yake wanakufa wakiteseka Sana.

Yuda baada ya kufanya Usaliti au Ubaya kwa Yesu alitumikia mateso, mfadhaiko Hadi akaamua kujiua. BASHIRU wa Sudani, Ben Ali wa Tunisia, Mubarak wa Misri, Gagbo wa Ivory Coast na wengineo hawakuwahi kuishi kwa amani baada ya uongozi wao.

Unafikiri katika Viongozi tulionao Sasa kwa ngazi zote Nani unafikiri anaweza kuishi maisha Kama haya baada ya kustaafu?

Ole Mushi
0712702602

View attachment 1409057

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom