Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Ndugu zangu,
Saikolojia unasema "ukiona mtu anazungumzia jambo lililomponyoka mara kwa mara ujue bado analitamani" kwa mfano mtu kaachwa lakini kuwa kucha badala ya kufanya kazi nyingine anafatilia maisha ya mtu aliyemwacha ujue suala limemuuma.
Profesa Mussa Assad alipoondolewa "u-CAG" alifungasha na akaondoka kuendelea na shughuli zake mara hii akitumia gari aina ya IST akiwa tofauti na Assad niliyemjua UDSM akitumia Benz jekundu na Nisssan Patrol rangi ya jeshi.
Baada ya "u-CAG" alifanya mihadhara kadhaa ya kitaaluma iliyoandaliwa na taasisi za kiislam na baadaye kuteuliwa kuwa VC wa chuo kikuu cha kiislam.
Kwa vijana msiomjua Prof.Safari si mwanasheria tu bali ni mwanadiplomasia aliyekuwa Mkuu wa chuo cha diplomasia,Kurasini. Alipoondolewa wadhifa wake alijiunga na chama cha CUF na baadaye CHADEMA ambapo alistaafia siasa.
Prof. Assad ana mengi namshauri kuliko kubaki na kinyongo apande jukwaani atoe hoja zake la sivyo anaonesha umma kuwa yeye ni "coward" anazungumza na kumsengenya mtu asiyeweza kumjibu.
Saikolojia unasema "ukiona mtu anazungumzia jambo lililomponyoka mara kwa mara ujue bado analitamani" kwa mfano mtu kaachwa lakini kuwa kucha badala ya kufanya kazi nyingine anafatilia maisha ya mtu aliyemwacha ujue suala limemuuma.
Profesa Mussa Assad alipoondolewa "u-CAG" alifungasha na akaondoka kuendelea na shughuli zake mara hii akitumia gari aina ya IST akiwa tofauti na Assad niliyemjua UDSM akitumia Benz jekundu na Nisssan Patrol rangi ya jeshi.
Baada ya "u-CAG" alifanya mihadhara kadhaa ya kitaaluma iliyoandaliwa na taasisi za kiislam na baadaye kuteuliwa kuwa VC wa chuo kikuu cha kiislam.
Kwa vijana msiomjua Prof.Safari si mwanasheria tu bali ni mwanadiplomasia aliyekuwa Mkuu wa chuo cha diplomasia,Kurasini. Alipoondolewa wadhifa wake alijiunga na chama cha CUF na baadaye CHADEMA ambapo alistaafia siasa.
Prof. Assad ana mengi namshauri kuliko kubaki na kinyongo apande jukwaani atoe hoja zake la sivyo anaonesha umma kuwa yeye ni "coward" anazungumza na kumsengenya mtu asiyeweza kumjibu.